Saturday, October 29, 2011

Karama za Romo Mtakatifu 1




Karama ya kupambanua roho

Hii karama mara nyingi inafafanuliwa kuwa ni kuwezeshwa kwa njia isiyo ya kawaida, kuona au kutambua kitu kinachoendelea katika ulimwengu wa roho.
Maono katika akili au macho ya mwamini yanaweza kuwekwa katika fungu la kupambanua roho. Hii karama inaweza kumruhusu mwamini aone malaika, mapepo, au hata amwone Yesu Mwenyewe, kama ilvyotokea kwa Paulo mara kadha (ona Matendo 18:9, 10; 22:17-21; 23:11).

Wakati Elisha na mtumishi wake walipokuwa wanatafutwa na jeshi la Shamu, walijikuta wamenaswa katika mji wa Dotani. Mtumishi wa Elisha alitazama juu ya kuta za mji na baada ya kuona makundi ya askari yanajikusanya, alipata wasiwasi sana. 

[Elisha] Akamjibu, Usiogope; maana walio pamoja nasi ni wengi kuliko wale walio pamoja nao. Elisha akaomba akasema, Ee BWANA! Nakusihi mfumbue macho yake, apate kuona. BWANA akamfumbua macho yule mtumishi; naye akaona na tazama, kile kilima kilikuwa kimejaa farasi na magari ya moto yaliyomzunguka Elisha pande zote (2Waf. 6:16, 17).
Je, ulifahamu kwamba malaika husafiri kwa farasi wa kiroho na magari ya kiroho? Siku moja utawaona mbinguni, lakini mtumishi wa Elisha alipewa uwezo wa kuwaona hapa duniani.

Kwa njia ya karama hii, aaminiye anaweza kumtambua pepo mchafu anayemtesa mtu fulani na kuwa na uwezo wa kutambua ni roho ya aina gani.
Pia, karama hii haiwezeshi kuona katika ulimwengu wa roho tu bali hata kupambanua kwa namna nyingine yoyote katika ulimwengu wa kiroho. Kwa mfano: inakuwezesha kusikia kitu kutoka katika ulimwengu wa kiroho, kama sauti ya Mungu Mwenyewe.

Mwisho – hii karama si “ya utambuzi” kama ambavyo wengine wanazoea kuiita. Watu wenye kudai kuwa nayo wakati mwingine hudhani kwamba wanaweza kutambua makusudi au nia za wengine, lakini si kweli. “Karama” wanayodai kuwa nayo ni sahihi ikielezwa kwamba ni “karama ya kukosoa na kuhukumu wengine.” Ukweli ni kwamba pengine hata wewe ulikuwa nayo kabla ya kuokoka, na sasa kwa kuwa umeokoka, Mungu anataka akuweke huru kutokana nayo moja kwa moja!

Na Shepherd Save Ministry

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...