Tuesday, November 8, 2011

Kutana na Viongozi wa chama cha MUZIKI wa Injili Tanzania (CHAMUITA)



Wanamuziki wa Muziki wa Injili nchini Tanzania kwa Muda sasa wameunda umoja wao utakaowaunganisha kwa mambo mbalimbali kwa ajili ya kumtumikia Mungu Ndani na nje ya Tanzania. Moja kati ya mafanikio ya umoja huu katika mwaka huu wa 201  ni kuingia studio na kurekodi wimbo wa Video Maalumu unaohusu MIAKA Hamsini ya Uhuru wa Tanzania, zaidi ya Waimbaji 20 wa nyimbo za injili  nchini walishiriki kuandaa wimbo huo.
Viongozi wa Umoja huo(CHAMUITA) ni kama ifuatavyo
Addo november - Rais
Mch Joseph Malumbu - Kaimu
David Robert - Katibu mkuu
Jane Misso - Katibu msaidizi
Stella Joel/John Shabani - Makatibu wenezi
Upendo Kilahiro - Mweka hazina
Max (Mwana mapinduzi) - kaimu mweka hazina

Walezi  wa umoja huo ni pamoja na ni Mheshimiwa Martha Mlata na Promota maarufu wa nyimbo za injili nchini bwana Alex Msama.Katika safu ya viongozi hao wamo pia viongozi wa idara mbalimbali pamoja na viongozi wa chamuita kutoka mikoani.

Rais wa CHAMUITA Mtumishi Addo November

David Robert

John Said Katibu Mwenezi
Mheshimiwa Mbunge wa Viti Maalumu Martha Mlata Mlezi wa Chamuita

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...