Sunday, February 27, 2011

NOTHING BUT THE BLOOD OF JESUS LYRICS

Nothing but the blood of Jesus;
What can make me whole again?
Nothing but the blood of Jesus.

    
Chorus: Oh! precious is the flow
             That makes me white as snow;
             No other fount I know,
             Nothing but the blood of Jesus.

For my cleansing this I see--
Nothing but the blood of Jesus!
For my pardon this my plea--
Nothing but the blood of Jesus!
 Chorus
Nothing can my sin erase
Nothing but the blood of Jesus!
Naught of works, 'tis all of grace--
Nothing but the blood of Jesus! 
Chorus
This is all my hope and peace--
Nothing but the blood of Jesus!
This is all my righteousness--
Nothing but the blood of Jesus!
Chorus


MIKESHA YA LEO NA MTAZAMO WA BIBLIA KUHUSU MAOMBI YA MAPATANO

Maombi ya mikesha msingi wake mkubwa ni mapatano ya watu hao walioamua kutafuta suluhisho toka kwa Mungu Juu ya kile kilicho mbele yao.Kwanza nieleweke kua hapa nazungumzia maombi na sio kuombewa yaani maombezi. Biblia inatuonyesha namna ambavyo baba zetu walifanya wakati wanatafuta majibu yao toka kwa Mungu wakiwa kama timu au kundi la watu. Tunawaona kina shadraki ,Meshak ,Ebednego pamoja na Daniel namna walivyoenda kwa Mungu kwa umoja Daniel 2:17-23 pia tunawaona Paulo na Silasi walivyomlilia Mungu katika taabu yao.
Makamu wa Rais wa Tanzania Mh Omar Gharib Bilal akiwa mgeni rasmi katika moja ya mikesha ya kuliombea Taifa uliofanyika uwanja wa Taifa jijini Dar-es-salaam
Kwa habari ya Kina Daniel kwa pamoja vijana hao waliona uzito wa hoja iliyo mbele yao na wakania kwa dhati kuingia katika maombi. Unaweza kugundua kua vijana hawa hawakujiuliza watajibiwa lini hilo kwao halikuwasumbua bali walijiapiza kua hawatatoka usoni pa MUNGU mpaka wajibiwe. Kwa mtazamo huo ukapelekea akili zao,nguvu zao,nia zao za ndani zilenge kuhakikisha MUNGU anatokeza na kuwapa ndoto na  tafsiri ya yake. Na kwa kadri ambavyo walionyesha kudhamiria kwa pamoja katika maombi yao ndipo MUNGU hakukaa kimya. Mwishoni baada ya kupata jibu toka kwa Mungu na kuliwakilisha ndipo inatoka amri kwa Mfalme Nebukadreza kua asiabudiwe MUNGU mwingine isipokua MUNGU wa akina Daniel.
                                                                          
 Naporudi kanisani leo nakutana na maombi mengi ya mapatano ikiwemo mikesha, hapa naijumlisha mikesha yote ile inayofanywa ndani makanisani iwe ya vikundi vya vijana, wamama, kwaya nk pamoja na ile ifanyikayo nje katika viwanja vya wazi. Watumishi wanaaoanda mikesha hiyo hua na malengo maalumu ambayo mwisho wa mikesha hutaka kuona kila aliyehudhulia kafikia lengo la mkesha huo. Inapofikia hapo pa kuangalia ufanisi wa mikesha yetu leo nakua na maswali mengi kichwani. Kama tumeamua kufanya maombi ya mapatano kwa kifupi hii ni timu, na mara nyingine uzembe wa mchezaji mmoja huigharimu timu nzima.

Hivyo tunapoenda katika mkesha tunaweza kua sehemu ya kuufanikisha mkesha huo au kuudhohofisha. Siamini kama Mungu alikua makini kuisikiliza sauti ya Daniel pekee wakati wale vijana wote wanne walipokua wakiomba. Hivyo kujibiwa kwa vijana hao ni matokeo ya wao wote kwenda mbele za uso wa Mungu kwa pamoja na kwa nia moja wakiwa na dhamira ya dhati kumsihi Mungu asikilize maombi yao. Dhamira ya dhati kutafuta majibu toka kwa Mungu kwa pamoja ndio msingi mkubwa wa Maombi ya mapatano.
Watumishi wakimlilia Mungu kwa Pamoja kama timu
 
Waumini au washiriki wa mikesha hiyo siamini kama hua tuna picha halisi ya lengo la mikesha hiyo na hata kama tunayo basi ni kwa kiasi kidogo mno, nashawishika kusema hatujui nini kilicho nyuma ya mikesha hiyo. Katika maombi ya pamoja kwanza ni mapatano ya kutafuta suluhu toka kwa MUNGU kama tulivyoona kwa kina Daniel.Tunapokua katika mikesha ya namna hiyo binafsi hua inanisumbua pindi nnapojiuliza Je ni wote tuliohudhuria tunahitaji majibu ya maombi hayo kwa dhati?
      
Nachokiona leo, wokovu na maombi ya mikesha vinaenda kimazoea zaidi, ni kama hua tunajisemea kwa kua hua tunaenda kwenye mikesha oookyy basi na leo twende !!!. Tunafanya maamuzi ya haraka haraka ili yafumbue matatiyo yaliyodumu kwa muda mrefu, mwisho wa siku tunaishia kupaka rangi bahari. Ni wazi kua mikesha ya leo ni kama fashion ile kiu ya kwenda kwenye mkesha kwa nia ya kukutana na MUNGU ni ndogo kuliko kiu ya kukutana na marafiki, ndugu jamaa. Hivyo tunajikuta tunaenda mikeshani ili kusocialize na kidoooogo kuutafuta uso wa Mungu. Wapo pia wanaoenda kwenye mikesha kwa sababu tu labda ni viongozi Fulani makanisani au ni viongozi katika kikundi Fulani hivyo cheo ndio mzizi wa uwepo wao mikeshani. Ni watu wachache sana ambao hudhamiria toka wakiwa makwao kua napoenda katika mkesha wa leo ntapaza Sauti yangu kwa MUNGU kwa kumaanisha kama alivyofanya Anna katika 1Sam 10-19.
      
Ni kawaida kabisa leo kuona watu wakienda katika mikesha kama wanakwenda kwenye Burudani, ile hali ya kuugua ndani/mzigo juu lile linalokwenda kutokea kwenye mkesha haipo. Mwanafunzi bora ni yule anayejiandaa kabla ya kuingia katika mitihani na sio anayekurupuka. Kabla ya kwenda kwa  MUNGU pia ni vivyo hivyo ile nia ya dhati tunayokua nayo ya kukutana na MUNGU, huchochea humuweka MUNGU karibu yetu. Daudi akasema nafsi yangu yakutamani kama ayala atafutavyo maji ya mto, hapa nafsi ya Daudi ina kiu naweza sema haja ya kina ya  kukutana na MUNGU nahii ni moja kati ya sababu zilizomfanya Mungu awe rafiki mkubwa wa Daudi.
                                           
Vijana wakiwa katika mkesha
Luka 14:28-30 "Maana ni nani katika ninyi, kama akitaka kujenga mnara asiyeketi kwanza na kuhesabu gharama? " Kabla hatujaenda kwenye mikesha ni wangapi kati yetu wenye desturi ya kukaa chini kwanza na kujiuliza naenda kukutana na nani, Na huyo Mungu anauzito gani kwangu hadi nikaongee nae. Pasipo kujiuliza maswali kama hayo utakuta kwenye mikesha mingi watu wanakua hai wakati wa kusifu na kuabudu ikifika wakati wa kiini ncha mikesha hiyo yaani maombi watu wanapotea kwa kutoka nje kama ni kanisani, na kama ni uwanja wa wazi basi wanaanza kupiga stori.

Ni vizuri tunaposema tunaenda katika mikesha makanisani au viwanja vya wazi kuomba au kwenda kwenye tukio lolote tunalolifanya usiku mzima kwa ajili ya MUNGU tujipange kwa kua katika makusanyiko hayo MUNGU hua yuko serious  kuliko tunavyofikiria. Leo vijana makanisani au vyuoni utakuta wanaenda kwenye Campus Nights kama wanaenda Mlimani city au Nyumbani Hotel (Mwanza) kuangalia sinema. Hata kama ni tamasha la kusifu na kuabudu weka malengo na tamasha hilo Kua ntamsifu Mungu wangu pasipo mzaha kwa kua katika kumsifu yeye ndiko aliko. kadri ambavyo tupatavyo neema ya kua karibu zaidi na Mungu kwa njia ya maombi au kusifu na kuabudu yeye hushuka na kukaa nasi kisha vile vitu vyote ambavyo si vya kimungu(Vimelea) vilivyo kati yetu huondoka. Hii ni kwa kua vifungo hivyo hushindwa kustahimili nguvu ambazo MUNGU hushuka nazo hatimaye tunawekwa huru, ndio mana kunashuhuda nyingi leo za watu kuponywa na nguvu za Mungu au MUNGU kutupatia mahitaji yetu kupitia mikesha pindi tupojipanga sawasawa.

Wanafunzi wa vyuo vya Elimu ya juu toka jijini Dar-es-salaam wakiwa kwenye Campus Night ya mwaka 2009 iliyofanyika katika Uwanja wa Taifa
Kwenye matamasha ya kusifu na kuabudu nako kunahitajika hekima ya Mungu katika kujipanga kabla ya kuhudhuria, kwa kua kuna tofauti kati ya mwanafunzi anayekwenda shule na yule anayekwenda shuleni kusoma. kiini cha matamasha hayo ndicho kitupelekee kuhudhuria na sio kwa sababu msanii Fulani yupo. Tukisema kumsifu Mungu ni lazima msanii Fulani mkubwa awepo ndio tamasha lifanyike au mkesha unoge huu ni ufa mwingine ambao leo unaojijenga katikati ya kanisa. Kimsingi muziki ni sanaa tusipojipanga kabla ya kuhudhuria tutajikuta tunaenda kuburudishwa tu na tunarudi wakavu majumbani kwetu. Leo ukilichukua gitaa la John Lissu tukawapa Twanga pepeta litapiga vizuri tu kwa kua muziki ni sanaa, hivyo muziki wa ki-Mungu unaweza pia kukuburudisha vile vile unaweza kukuweka karibu na MUNGU endapo ukikamia lolote kati ya hayo mawili
Moja ya matamasha ya kusifu na kuabudu
Katika mikesha nguvu za MUNGU na msaada wake huwepo hivyo ni jukumu la mgonjwa kusogea mwenyewe na kutumbukia katika kisima cha uponyaji kwa kua malaika tayari anakua keshatibua maji. Pindi MUNGU anapoleta msaada katikati yetu kisha sisi tukabaki kushangaa au kupiga stori ule msaada uliokuwepo usiku huo unakua hauna maana, hii hali ya kutothamini nguvu zaMungu mara nyingine inaunda ghadhabu ya MUNGU juu yetu. Ni jambo la kawaida leo kuona watu wanaenda mikeshani na matatizo yao na wanarudi nayo nyumbani. Hii haimaanishi Mungu hakuwako mkeshani au mahali pa kusanyiko, kimsingi alikuweko na alikua akitafuta yule anayemtafuta kwa dhati ili ampe msaada ila wakachengana.

Ni vizuri kila anayehudhuria mkesha wowote kwa ajili ya Mungu kabla hajavaa tai,tshirt,sketi,viatu nk maana skuizi kuna mbwembwe nyingi za uvaaji pindi tunapoenda mikeshani tutambue uzito wa yule yunayekwenda kutafuta majibu kwake na tujiulize maswali mengi kuhusu yeye. Kwa kua yeye MUNGU yuko serious sana na Mikesha hiyo kuliko sisi.


V.N Mboya
                                                                                                      

THE OIL CANNOT BUILD GHANA, WISDOM WILL – DR MENSAH OTABIL

Dr Otabil Mensah
The General Overseer of the International Central Gospel Church
Pastor Mensah Otabil has said that though oil has been discovered in the country, it is insufficient to build the nation.

Therefore, he emphasised that wisdom from God is what Ghana needs to channell the oil resource for development.

Pastor Otabil was speaking at the Jubilee 1st Oil Thanksgiving Service at the Dome of the Accra International Conference Centre.

It was on the theme: Through Wisdom A House is Built, and by understanding it is established,” a scripture quoted from Proverbs 23:3-6.

Pastor Mensah Otabil noted that though the oil find is in appreciable quantity, it is quite small to create any dramatic change in Ghana’s economic development.

“Oil is good,” he said, “ but it is not the answer to all [our problems]”.

Pastor Otabil, who is also the Chancellor of the Central University College, said since the oil resource cannot by itself provide the needed capital for development, it is incumbent upon the nation’s leaders to commit it to judicious use for the benefit of all the citizenry.
                                                                             

Central University College owned by Bishop Dr Otabil Mensah

He explained that the revenue can either be invested - which requires that it is put to use for long-term sustained returns - or ingested - spending the revenue anyhow.

Pastor Otabil stated that in the mist of the numerous national demands, it is necessary to prioritise, especially in the education sector due to its crucial significance to development.

“If we continue to provide mediocre education, we will continue to produce mediocre citizens,” he said.

Mr Otabil also touched on the need for all Ghanaians to have a shift in their way of thinking, moving away the archaic way of doing things.

He chided political leaders for their infantile way of tackling issues of national concern with their focus mainly on scoring political points.

“Our politicians behave as if the most important constituency in life is whether the NDC or the NPP wins a debate,” he added.

The man of God also took a swipe at the media for its shallow analysis of developmental issues, insisting that these are not good enough for sustained economic development.

Pastor Otabil reminded the nation’s leaders that good interventions are not good enough but that the choices they make on behalf of the nation is what will make a difference.

“May the God who gave us the oil give us the wisdom to use it wisely,” he concluded.
Thanksgiving service

Accra Comference centre where Dr Mensah gave out his speech

                                                                                      

MAISHA NA HATIMA YA WANAFUNZI WA KRISTO MARA BAADA YA KRISTO KUONDOKA

Jiji la Jerusaleem ambapo Yakobo Mwana wa Zebedayo aliuwawa wakati akihubiri habari za Kristo
Leo katika Hosanna Inc tunapitia maisha ya wanafunzi wa kristo na wajibu waliopewa na kristo baada ya kristo kuondoka. Lengo hasa ni kutuwezesha kujua namna ambavyo waliotutangulia katika wokovu walivyokutana na changamoto ili na sisi tupige mbio zaidi katika kuutangaza ufalme wa Mungu. Hii ni kwa kua tumepokea hiki kijiti toka kwao hivyo na sisi tunayo safari yetu katika kristo YESU. Habari kuhusu Maisha ya Mitume hao na namna walivyosambaa duniani kote mpaka vifo vyao zinapatikana katika vitabu vilivyoandikwa katika kanisa la Kwanza. Schumacher ni Mwanahistoria wa kanisa aliyefanya utafiti kuhusu maisha ya mitume (wanafunzi wa kristo) na hivi ni namna ambavyo mitume hao walivyokuimbana na misukosuko katika kumtangaza Kristo Yesu.

MATHAYO
Mtumishi Mathayo yeye aliuwawa kwa upanga akiwa katika nchi ya Ethiopia

MARKO
Marko yeye alifia katika mji wa Alexandria nchini Misri mara baada ya kuburutwa na Farasi katika mitaa ya mji huo mpaka mauti ilipomfika.

LUKA
Yeye aliuwawa huko nchini ugiriki alipokua akitangaza habari za kristo

YOHANA
Yohana yeye aliwekwa katika kikaango/sinia kubwa lenye mafuta yaliyochemshwa na kwa Neema ya ajabu akafanikiwa kutoka katika mauti iliyokua ikimkabili.Baada ya kutoka katika kisiwa cha Patmo alipokua amefungwa na kufanikiwa kuandika kitabu chaUFUNUO akiwa kisiwani hapo, alikuja kua Askofu wa Edessa ambayo sasa inajulikana kama nchi ya Uturuki.Yohana alifariki nakiwa mzee sana na ni  mwanafunzi wa kristo pekee aliyekufa pasipo mateso.

PETRO
Yeye baada ya kukamatwa akieneza habari za Kristo, aliamriwa asulubiwe kichwa chini miguu juu kama Kristo Yesu, Lakini petro aliwaomba watu hao wamsimsulubishe kama namna ambavyo kristo alifanyiwa kwa kua Petro alisema yeye hana hadhi ya kusulubishwa kama Bwana wake. Ndipo walipoamua kumsulubisha kinyume na Kristo, hivyo Petro akasulubiwa kichwa chini miguu juu mpaka mauti ilipomfika.
Ramani ya jiji la Jerusalem
YAKOBO
Yeye alikua kiongozi wa kanisa la Yerusaremu, alitupwa katika bonde la mita mia moja pale alipokataa kuikana imani ya Kristo.Walipogundua kua hajafa adui zake waliamua kumpiga kwa rungu mpaka kufa. Bonde hilo ni lile ambalo Shetani alimuonyesha Yesu wakati akimjaribu kule nyikani.

YAKOBO MWANA WA ZEBEDAYO
Yeye alikua mvuvi kabla hajaitwa na kristo yeye iliuawa katka jiji la Jerusalem

BATHOLOMAYO
Alijulikana pia kwajina la Nathania ,alikua ni mmishionari katika bara la Asia, Alishuhudia habari za kristo katika nchi ya Uturuki.Aliuawa kwa kukaangwa.

ANDREA
Yeye  alitundikwa msalabani kwa mfumo wa X katika mji wa Patras nchini ugiriki baada ya kuteswa ipasavyo na askari wapatao saba,kasha wakamfunga msalabani with cords to plorong his agony.Wafuasi wake walisema  wakati wanampeleka msalabani,Andrea alisema “Nina uamuzi udumuo na niliutegemea muda huu wa furaha”. Aliendelea kuhubiri akiwa hapo msalabani kwa siku mbili mpaka pumzi yake ya mwisho ilipokoma

THOMASO
Yeye aliuawa kwa kuchomwa na mkuki huko India alipokua katika moja ya safari zake za kiumishieni kwa ajili ya kufungua kanisa.
Geti la kuingilia mji wa Damaskus huko Israel
                                                                                                                                                        

Friday, February 25, 2011

INVESTING YOUR WHOLE HEART IN YOUR PURPOSE

We have to invest all our effort on what we are doing

• God gives us EVERYTHING we need to worship and serve Him.
• God expects us to use EVERYTHING He has given us to Worship Him.
• Worship is a “do something” activity.
• Wholehearted worship produces results and half-hearted worship produces regrets. God always desired our whole hearted devotion to Him. Sin got in the way and made half-heartedness a Giant in out lives. A Giant we need to face and conquer.
• God expects us to respect the level of commitment He wants from us.
• When we do not give God our best, others will not give God their best. Leaders, if you do not give God your best, do not expect those you lead to give God their best either. Parents, if you do not give God your best, do not expect your children to give God their best either!
• When we are committed to doing our best (to defeating the giant of half-heartedness), we:

o Have the greatest influence on others

o Produce our best work for Christ

o We received God’s blessing and reward

o We live and love God with our whole heart

KINGDOM AUTHORITY - DR. MYLES MUNROE


Sunday, February 20, 2011

FILAMU ZA KITANZANIA NA MAUDHUI YAKE KWA KANISA


Kwa siku za hivi karibuni kumekuwako na mafanikio makubwa kwa soko la filamu hususani zile zitengenezwazo hapa hapa Tanzania. Mtazamo juu ya Filamu hizo umebadilika leo hii sio watoto na wakina mama pekee ndio wanapendao kuziangalia bali wababa na wazee pia wako mstari wa mbele katika hilo. Zipo Filamu nyingi zenye maudhui tofauti tofauti na mwisho wa siku huingizwa sokoni ambako wakristo na wasio wakristo hupata nafasi ya kuzinunua na kuziangalia.
                Ni wazi kua kiimaadili ya kikristo zipo filamu za kuziangalia na zipo za kuzirusha kwenye dust bin.Wakristo wengi hupenda kuangalia filamu kama sehemu ya kupumzika na kure-fresh, sasa tatizo linakuja watapata wapi filamu za Kiswahili zenye mafundisho chanya pasipo kukwazika katikati ya filamu hizo!!!. Kanisa la leo halihitaji filamu kama filamu zenye mafundisho ya ki-mungu pekee bali linahitaji filamu zenye UBORA kuanzia kwa wasanii wenyewe wawe na ushuhuda mzuri mbele ya jamii, Production ya viwango vya juu, Ujumbe sahihi kulingana na Biblia na standards za kikristo pasipo mbwembwe tuzionazo leo kwenye filamu zilizopo kuhusu wokovu.
               Kulingana na kuenea kwa sayansi na Teknolojia kanisa hususani la Tanzania halina budi kuichukulia Tasnia ya Filamu kama mkondo mwingine wa kupeleka injili kwa wanzania wenzetu na nje ya Tanzania. Makanisani waandaliwe vijana sio kufundishwa tu kuigiza bali waandaliwe kifikra kuwa hata uigizaji wa Filamu nao ni utumishi. Kama mtu anaweza akaimba na kuyagusa maisha ya watu kwa utukufu wa Mungu,vile vile muigizaji wa filamu anaweza akaigiza na kuyagusa maisha ya watu kupitia uigizaji kwa utukufu wa MUNGU.
               Kwa wenzetu nje, kanisa imeliona hili ndio maana leo kuna orodha ndefu ya waigizaji waliookoka ambao ni mamilionea, tumeshuhudia nchi za wenzetu makanisa yakianzisha makampuni ya Filamu kwa kua wamegundua Filamu ni mfereji mwingine wa kumpitisha kristo katika maisha ya watu. Lengo hapa sio kufanya Filamu kwa kua wenzetu waliookoka nje wanafanya bali tunafanya kwa kua imetupasa kufanya kama sehemu ya utumishi wetu ndani ya Kristo Yesu. Leo hii kijana anaweza asisome Biblia wala kwenda kanisani Mwezi mzima ila akaangalia filamu zaidi ya tano kwa mwezi huo huo. Japokua kwa sasa Tanzania kuna baadhi ya watumishi wameanza kuliona hilo ila juhudi mathubuti ni lazima zichukuliwe ili kulifanikisha hilo.
Jenifer Mgendi ni miongoni mwa watumishi wa Mungu hapa Tanzania walioamua kuanza kutengeneza Filamu zenye maudhui ya kikristo.Mpaka sasa Mgendi ndiye anayeongoza kwa kutoa filamu nyingi miongoni mwa watumishi hapa Tanzania,ameshatengeneza Filamu tatu na zote ziko sokoni ambazo ni Joto la Roho,Teke la Mama pamoja na Pigo la Faraja.
Haris Kapiga Muimbaji wa nyimbo za injiri,Mc Maarufu jijini Dar-es-salaam,na Mtangazaji wa Clouds FM naye ameanza kushiriki kuigiza katika Filamu na Tamthilia zenye mafundisho ya kikristo
Mchungajii Upendo Kilahiro naye ametengeneza Filamu inayohusu maisha ya ukristo
Sarah Mvungi ni miongoni mwa wasanii toka kundi la Kaole Sanaa Group ambaye kwa sasa anajishughulisha na uigizaji wa Filamu na tamthilia,Mbali na uigizaji Sarah ni Nesi na Muimbaji wa nyimbo za Injili
Bishop TD Jakes chini ya kampuni yake ya TD JAKES Co Ltd amefanikiwa kutengenea Filamu zenye maadili na shuhuda za kikristo. kati ya filamu zilizoipa umaarufu kampuni yake ya Filamu ni Filamu ya Not easly Broken na Woman thou at Loosed iliyochezwa kwa umahili na mwanamama Kimberly Elise.
Askofu Thomas Jakes(TD JAKES) licha ya kumiliki kampuni linalotengeneza Filamu,pia hushiriki kuigiza.Hapo juu ni moja ya vipande alivyoshiriki katika Filamu ya Woman thou at Loosed.Hapo alienda kumtembelea gerezani mwanadada Kimberly Elise
Woman thou art Loosed filamu maarufu iliyotengenezwa na Kampuni ya Filamu inayomilikiwa na askofu TD Jakes
Kama umewahi kuiona hii Filamu utakubaliana na Hosanna Inc kua Haichoshi,inamafundisho ya Kikristo yenye kuvutia,ni moja kati ya kazi toka kwa askofu Td Jakes
Jumping the Broom,Filam mpya chini ya kampuni ya TD Jakes inayotarajiwa kuzinduliwa tarehe 6 mwezi wa Tano mwaka huu wa 2011

Miongoni mwa watumishi wa MUNGU waliofanikiwa katika tasnia ya Filamu Duniani huwezi kuacha kumtaja Tyler Perry Chini ya kampuni yake ya Tyler Perry Co Ltd. Ametengeneza Christians Muvies nyingi huku akiwashirikisha watu maarufu katika filamu hizo.
Tyler Perry mkurugenzi na mmiliki wa Tyler Perry Films Co Ltd
Moja kati Filamu zenye mafundisho ya kikristo zilizotengenezwa na kampuni ya Tyler Perry
Moja kati ya kazi mahiri toka kwa Tyler Perry
                                                                          
                                                                                                                                                     

NAJIVUNIA YESU WANGU - THE VOICE




The voice, One among of strong Gospel Group singers in Tanzania which is composed of youth from Adventist Church, they always sing without using any Music instrument(acapella). “Najivunia Yesu wangu” is one among of the tracks found in their First Album.People of GOD this song is so powerful.

DO NOT USE SAUL'S ARMOR

We need GOD Direction in order to attain our Goals
1 Samuel 17:38-40 NIV
 Then Saul dressed David in his own tunic. He put a coat of armor on him and a bronze helmet on his head. 39 David fastened on his sword over the tunic and tried walking around, because he was not used to them.
“I cannot go in these,” he said to Saul, “because I am not used to them.” So he took them off. 40 Then he took his staff in his hand, chose five smooth stones from the stream, put them in the pouch of his shepherd’s bag and, with his sling in his hand, approached the Philistine.

David is about to face the biggest challenge in his life and it may cost him his life. Saul the king has allowed him to fight this battle yet in his mind he is convinced that David does not stand a chance. So, Saul does the most sensible thing to make the situation a little better. He gives David his amour. I am sure Saul had fought many wars and come out victorious using this same amour. David tries it on, but it just does not feel right to him. It feels clumsy and heavy and he cannot move freely with Saul’s amour on.

Just because it worked for so and so in a particular manner, does not mean that it will work for you in the same way. I have seen many people get disappointed because they tried to fight the battles before them by using another person’s armor. We all have our battles to fight and it is up to us to ask God who has called us to fight these battles what weapons to use. Just because God told me to give all my salary and as I obeyed He came through for me financially, does not mean I go preaching to everyone who is facing a financial crisis to do the same.
In John 9:6 Jesus healed a blind man by spiting in the dust and making mud which he applied to the man’s eyes and after the man washed, he was healed! Does that mean that every time we are praying for a blind man we are to do the same and they will be healed? I don’t think so. That was the weapon that God instructed for that particular situation. In Mark 10:52 He heals blind Bartimaeus by just speaking, He does not even touch him.

I remember once in church we were praying for the sick and there was this gentleman who was in line because he was tired of wearing spectacles and he believed God to heal him. There he was, crying out to his God, tears all over his face. We finished praying and the people were going back to their seats but not him. Not without his miracle! He leaned over to one of the pastors and told him that God was saying for him to receive his healing, the pastor was to spit into his eyes. The pastor was taken aback by the request, but the man was fully convinced that God had spoken and so the pastor obliged. The man was head!

What weapons has God given you to fight against the giant before you? Logically it seemed like David stood a better chance against Goliath if he were to fight with Saul’s amour. Saul’s amour was heavy and uncomfortable. God gave David 5 smooth stones and a sling. In the eyes of all it looked like nothing but it got the job done in record time.

The voice, One among of strong Gospel Group singers in Tanzania which is composed of youth from Adventist Church, they always sing without using any Music instrument(acapella). “Najivunia Yesu wangu” is one among of the tracks found in their First Album.People of GOD this song it is so powerful.

Friday, February 18, 2011

TB JOSHUA PROPHERCY ON MUBARAK (EGYPT) RESIGNATION

Before GOD has decided to do something on Earth he always notifies his people, as he did to Merry upon the Birth of Jesus Christ, he spoke with Noah about what he is going to do to the cities of Sodom and Gomorrah, even upon the resignation of Former president of Egypt Hon Hosnni Mubarak he spoke with Prophet TB JOSHUA and his Servant notifies the World.He said ``Am seen a leader RESIGNING because of the plessure mounted on Him``.Here is the Prophecy of TB JOSHUA about Egypt through Emmanuel Television.


Tuesday, February 15, 2011

KWA MPENDWA KUFANYA KAZI ZA PROGRAMU ZA KONDOMU IMEKAAJE?

Care International moja kati ya Mashirika yanayofanya kazi ya kuihudumia jamii ikiwa ni pamoja na kugawa mipira ya kiume na kike pindi inapohitajika na jamii husika.

By Edna

Jamani naomba mnisaidie hapa, na yamkini mchango wenu wa mawazo utaweza kunifanya niache au nifanye hiki kitu kwa ujasiri zaidi.
Nimechaguliwa kuwa focal person wa mambo ya AIDS/HIV miezi mitano iliyopita hapa ofisini kwetu, sasa kuna mlokole mwenzangu mmoja alikuja ofisini kwangu akanikuta niko full package kikazi zaidi na full vifaa kuhusu AIDS/HIV yaani vipeperushi, condoms za kumwaga, n.k akaniambia sasa naona umeamua kuwaambia watu wakazini/wauasherati....nikajaribu kumuelewesha nia yangu lakini bado haikuwa rahisi kwake kunielewa. Nikakaa baadae nikaona yamkini mimi ndio nahitaji kueleweshwa ama yeye ndio anahitaji kuelewa kwahiyo nikaamua niliweke hili kwenu wadau .

1. Hivi kuwapa watu condom ni kuwasaidia au kuwafanya waangamie kabisa, what if your intentions ni kuwasaidia maana hao ambao wanapatikana na maambukizi ni hao hao wa makanisani kwetu na misikitini, tunafanyaje ili kuhakikisha tunawasaidia katika hili ili wakianguka waweze kuanguka salama??
Kuna movie inaitwa MADEA GOES TO JAIL kwa wale ambao wameiona, kuna mdada mmoja MKRISTO yaani mimi ningemwita mlokole, anafanya kazi ya kuhubiri wagerezani, kuwahubiria makahaba(na yeye kabla ya kuwa saved alikuwa kahaba) na wanaokubali kubadilika anawasaidia kupata kazi na kuishi nao. Wengine ambao wanaendelea na ukahaba au madawa ya kulevya anapita kwenye magenge yao(mahali ambao wanafanya huo ukahaba na kula unga) na kuwapa sindano za kujidungia ili wasishirikiane sindano kitu ambacho sio afya na madada poa huwapa condoms. Kwa mawazo yangu sikuona shida katika hilo kwa sababu matokeo positive yalikuwa yanaonekana, kweli makahaba walikuwa wanabadilika baada ya muda na walikuwa wanamkubali kweli labda manabii, mitume, mashehe mniambie au na mimi nilikula tango pori-maziwa yaliyogishiwa??
2. Kuna maswala ya uzazi wa mpango pia, ingawa kwa imani nyingine pia hili nalo ni dhambi, lakini pia condom inatumika kwenye uzazi wa mpango.

3. Pia kuna situations, mfano kama mumeoana na wote mkagundulika mna maambukizi ya virusi vya UKIMWI, mnatakiwa mtumie condom ili kusaidia uenezwaji wa virusi kwenu wote wawili na kuzifanya dawa(kwa wale wanaotumia ART) zisiwe resistant. Au hata kama amekutwa mmoja na maambukizi hayo itabidi hiyo couple wawe wanajisavia wka kutumia condom ili msambazwaji wa maambukizi ya virusi usitokee.
Hebu naomba mnisaidie katika hili wapenzi katika bwana maana SHIRIKA langu pia halina dini.


Edna

                                   xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx



Cements

1. Papaa said...
Je tunasemaje Watumishi wa Mungu wanaowataka dada zetu, wake zetu ana Rafiki zetu wa kike? Nadhani suala la kutaka kufanza zinaa haijalishi wewe ni mwansheria ama daktari, ngoja nikupe Biblical Point of View, Daudi alitembea na Bethsheba lakini Daudi si Daktari, Amnoni na Tamari walibakana si Madktari, Sex ni hulka ya mtu.
Embu kwanza tuache malumbano yasiyo na tija mie napenda hoja Kama Edna anachofanya ni Kibaya ni kibaya how, na kama anachofanyani ni sahihi kwa vipi, tuweke hoja mezani, hakuna anayejua wote tunaelimishana mimi ntasema mbaya sababu moja mbili tatu, mie ntasema ni poa sababu a,b and ila uwe mwangalifu on x, y, and z.

2. Protace said...
Nadhani nimefuatilia vizuri. Sioni shida iliyopo juu ya kazi yake.
Nafasi yake ya kazi kuharibu ukristo wake ni jambo ambalo atakuwa amependa mwenyewe. Unaweza kufanya hiyo kazi na bado ukabaki salama.
Kuandika jambo hili kwenye marafiki huru ni kuonyesha ukomavu wa edna na pengine nia ya moyo maana wapo wengi wanaofanya madadu kimya kimya tuu.
Sote tunajua system ya siasa ya nchi. Je vipi addo ukipewa mlungula( kifurushi ) upeleka kwa mtu na mzee presidar katika kampeni za chama. Utafanyaje au haijawahi kutokea?teeeh teeh natania tu mjomba.
Kila kazi ina mazingira ambayo yanaweza kukukosesha mungu so inategemea ni jinsi gani umejipanga.

Kwa mtazamo wangu ni kwamba politics inaweza kukosesha na mungu kuliko hata hizo kazi zinazohusishwa na condom.
Nakumbuka gamanywa alivyoshambuliwa na walokole kwa kuwa mwenyekiti wa tume ya ukimwi.
Tukumbuke kwamba dunia yote ni ya mwovu na sisi tu mali ya bwana na hatuna dunia yetu wenyewe.

Protace 


Kama wa kristo ni jukumu letu kuangaza,Changamoto zinapokuja kwetu hazijakosea mlango,ziko mahali sahihi kwa kua zina masikio ya kusikia kua yuko mtu sahihi wa kukabiliana nazo
                                                             
3. Dr. Lyatuu said...
Waungwana... labda nianze kwa kusema

Lord is good.
Kwa kweli ni faraja na furaha kuona watu wana uhuru wa kutoa mawazo yao kwa kadri bwana anavyo/ alivyowafunulia. Huwa si rahisi kupata platform kama hii ambayo mtu unajisikia kuwa huru kujieleza kwa kadri unavyofahamu bila kuwa na woga wa "kutengwa".
Ni kazi ya Roho wa Mungu kutufundisha namna tunavyoweza kutumia KILA tulichopewa na Mungu - (ikiwa ni pamoja na akili, maarifa na vipawa tulivyopewa), kujipa na kutoa elimu ya kiroho kwa utukufu wa Mungu aliye hai. Wapendwa wengi wameishia pabaya - often kwa kuwa tu wamejikuta wanakabiliwa na situation ambayo kwa namna moja au nyingine hawana jibu sahihi la nini cha kufanya - kuwawezesha kuvuka walipo. Aidha wapendwa wengi wanajikuta "wanalazimika" kuwa katika situation fulani (mfano kufanya kazi kwenye bar), na kwa kuwa wanajua wapendwa kanisani "hawata nielewa", basi wanaamua na kanisani sasa basi. Matokeo ni kujitenga (hakuna anayewatenga... wanajiengua tu wenyewe taratibu. Matokeo ni kwa shetani kuwashughulikia kwa urahisi zaidi - hasa kwa kuwa wapo wapo tu wenyewe. And so... uhuru kama tulio nao hapa MH ni muhimu (na ninaweza kusema ni lazima) ili kukua kiroho. IN essence that is a part of "fellowship" - that is sharing; contributing & receiving from each one of us - jina la Bwana libarikiwe.

4.Mbeki said... 
 
Matumizi ya mipira ya ngono "condom" Kwanza ikumbukwe kwamba hizi ni kinga za "kupunguza" maambukizi ya magonjwa ya ngono na sio kwamba kinga za "kuzuia" maambukizi kwa asilimia 100. Ngoja niwanyambulie: Tafiti za usahihi wa kondomu au kifaa chochote cha kinga kinapimwa takriban kwa njia tatu kubwa yaani Laboratory studies, Epidemiologic studies na kisha/au clinical trials kisha avearge ya takwimu zinapelekea kufanya uamuzi wa kitu tunaita Theoretical and empirical basis of protection. Kwa hiyo ugawaji wa condomu kitafiti ni njia sahihi ya kuwaambia watu kwamba maambukizi ya magonjwa yote ya ngono kwa njia ya maji maji ya uzazi mfno(gonorrhea, chlamydia, trichomoniasis, and HIV na mimba) na ngozi-ngozi (skin to skin) kama (genital herpes, human papillomavirus, syphilis, and chancroid) zinaweza kupunguzwa kwa kiwango fulani kikubwa tu kulinganisha na kutotumia. Hii ni yamini na kweli. Peleka huuu jumbe kwa watumiaji na wala wasidanganywe au kuogopa wakifanya hivi watapunguza uwezo wa kuambukizwa na kuambukiza na watakuwa salama kimwili na kuendelea kusihi na hivyo kuwa taifa la kesho na leo. Inasaidia PERIOD.!! Usahihi wa Condom kwa Mkirsto: Ngono kama ngono nje ya ndoa ni dhambi, iwe salama au si salama. Iwe na kinga au bila kinga, na huu ni ukweli na wala hapa hatuhitaji kudebate. Je ni sahihi kwa Mkristo kugawa au kutoa elimu ya condom kwa watu; je mimi naweza au huwa naotoa: - Jibu ni kwamba mimi nakupa ukweli maana wewe ni mwanadamu, umepewa utashi na unaweza kujua. sikunyimi maarifa ila si-impose imani yangu juu yako. Na mwisho ntakwambia njia sahihi ya kujikinga asilimia mia moja ni kutofanya. wewe uamue. jibu ni kwamba NI SAHIHI kutoa elimu. Mbona tunajifunza juu ya kutengeneza mabomu, kutengeneza pombe, na hata tunajua njia sahihi ambazio tukifanya tunaua wenzetu. Hata wengine tumejifunza judo, karate kia ni nin? je ni vibaya kusoma au kuongelea juu ya mambo haya?? mbona wakristo wengi tu tunamiliki bastola na bunduki eti tunadai ni ulinzi kwani tunajilinda na nini na si tunajua akija mtu uki-shoot unaua...!! sasa kuua si dhambi? kama hutaki kuua bastola ya nini? kwani unawinda mpaka ununue silaha? Kondomu ni kama binduki, kosa ni jinsi unavyoitumia, Kama ni mwenzangu kama Addo umeoa na unahisi hutaki kutumia njia nyingine za uzazi wa mpango, hewala tumia kondomu inakukinga kwa asilimia zake na wala mimba isiyotakiwa kabla ya wakati haitawapateni. Na "discondant pairs" wenye UKIMWI mmoja na mwingine hana ndani ya ndoa tunawapa condomu kibao ili wajikinge kwa ngono salama wasiambukizane ndani ya ndoa. itawaweka salama na kuwasaidia kutunzana na kulea watoto wao wa baadae. CONCLUSION Elimu yoyote ile chini ya jua si dhambi, dhambini matumizi ya elimu hiyo.. kwa aliye na mahitaji ya elimi ya kondomu, uzazi wa mpango, afya na magonjwa kwa ujumla anione kwa muda wake natoa bure au kwa ada/gharama nafuu/kidogo tu. Na hata machapisho na demonstartion waweza kupata pia. kama unahitaji models za kufundishia pia naweza kukuelelekeza wapi pa kuzipata ili Usije ukawadanganya watu kwa maneno mengi wakaelewa visivyo. My human rights jamani   Mbeki
5. Irene said...
Nakumbuka mpendwa mmoja yeye anafanya kazi Breweries tena section ya kuweka chemicals/alcohol ili hizo liquids ziwe pombe kamili... tena anakagua kama zimekolea. Ni mtumishi mzuri na muhubiri/mwalimu wa gospel.
Alichotuambia yeye ni kuwa huwa anapitia mitungi sijui barrels moja moja na kuziombea kuwa wanywaji waokoke, na pia wafanyakazi wa hapo Breweries waokoke.
Anasema there was a wave of revival huko Breweries as a lot of staff were born again.

Sasa hapo pima mwenyewe... hiyo strategy yake it works or not na pia pima mwenyewe kama je ni hii is just a justification ya yeye kufanya kazi huko?
Angalizo ni kuwa some things may not be sin, but may contradict your faith.
It may not be sin, but my compromise your faith - si wote wana ujasiri wa kupona katika maeneo hayo meaning some may end up back sliding, taratiiibu.
May not be sin but may confuse others who would like to come to Jesus or those newly born again....

Kubwa ni kuwa na uhakika ndani yako kuwa where you are is where God wants you to be.... si Breweries tu, popote, anguko halijali ni wapi unafanya kazi.

Irene

MUNGU HUMPA ALIYE HODARI MSAADA

Popote mtu alipo Nguvu ya MUNGU huwapo uwanjani
Katika maisha ya wokovu baada ya mtu kuokoka tunaanza safari ya maisha mapya ndani ya kristo YESU. Ndani ya safari hiyo kuna vitu ambavyo MUNGU anakusubiria uvifanye ili yeye aje kukusaidia.Lipo tatizo ambalo pengine mtu wa MUNGU analo kabla hata hajaokoka hadi anaokoka na kukaa katika wokovu stil tatizo hilo anakua nalo. Hii haimaanishi kua MUNGU ameshindwa kulitatua au kapungua nguvu, bali MUNGU anamsubiria  aanze kufanya jambo Fulani katika Mungu ili yeye atokee.
       Popote mtu alipo Nguvu ya MUNGU huwapo uwanjani na shetani naye yupo uwanjani pia na majeshi yake, vyote vikimuwinda mwanadamu. Hivyo ufahamu wa mwanadamu humfanya au jenge ufalme wa Mungu au wa kipepo.kwa kua ki Biblia dunia na vyote viijazavyo nchi ni Mali ya Mungu. Hata upande wa giza uko chini Mungu        Zab 24.Pia tunamuona MUNGU akimuita Nebukadreza mtumishi wangu(Yer 27:5) pamoja na kwamba Nebukadreza alikua akifanya kinyume na MUNGU.
      Baada ya kuokoka ukaanza safari katika kristo kisha katikati ya safari ukaanza kufanya vitu vya KIMUNGU  kwa ulegevu wakati upande wa pili/giza wao wako serious wakifanya kazi zao kwa Nguvu automatically unakua mateka wao pindi ukitia mguu katika vita dhidi yao,nasi pia pindi tukifanya kazi ya Mungu kwa nguvu tunakua na nguvu dhidi yao tunapoingia vitani nao tunaibuka washindi nao wanakua mateka wetu. Hii ni kwa kua MUNGU hana upendeleo yoyote afanyaye kwa bidii humpa ushindi
Mdo 10:34.
Tunaposema tunamwabudu Mungu au kumtafuta MUNGU lazima tumaanishe kwa kua ibada hukaa katika mashindano na aliye hodari kiibada Mungu ndio humridhia
Kuyafikia yale malengo aliyonayo MUNGU juu yetu inahitaji bidii kwa kua hicho unachokitaka katika Kristo ili ukipate, mwanadamu huingizwa katika mashindano.Wakati wewe unakitaka upande wa pili nao hujipanga kinyume nasi,lakini MUNGU anabaki katikati kwakua anasema kwenye Zab 89 kua yeye “humpa hodari msaada”.Ina maana kama Mtakatifu leo akiwa nataka cheo kazini akafunga wiki akimlilia MUNGU,na ofisini hapo hapo akawepo mtu mwingine anahitaji cheo hicho hicho yeye akaenda kulala makaburini wiki na akamtoa mwanae kama sadaka  kwa kua Nuru na giza vyote ni vya Mungu hivyo Mungu atampa aliye hodari msaada. Hapa kwa mujibu wa biblia aliyeonyesha kumaanisha ndio MUNGU hua upande wake.
       Tunaposema tunamwabudu Mungu au kumtafuta MUNGU lazima tumaanishe kwa kua ibada hukaa katika mashindano na aliye hodari kiibada Mungu ndio humridhia.Hivyo kufanya ibada sahihi ni lazima turudi nyuma tuone baba zetu kina Ibrahimu,Isaka,Daudi walifanya nini nasi tujipange kwa kumaanisha.Mahali pasipo na Ibada sahihi pana utumwa na Mwanadamu ni kiumbe pekee kilichopendelewa na MUNGU kumfanyia ibada.Ni Matumaini yangu kua jamii ya watu wa MUNGU leo tubadilike na kumaanisha tunachokifanya kwa ajili ya MUNGU.

                                                                                 
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...