Wednesday, June 29, 2011

Nguvu ya Maombi - Pastor Ibra Munanka


BWANA YESU asifiwe mpendwa!
Nakukaribisha katika ukurasa huu tena ili tujifunze maana ya maombi. hili neno "maombi" si neno geni miongoni mwa wakristo au wasio wakristo.Kwa haraka haraka tunaweza kusema, maombi yanafanywa na mhitaji au mtu aliyegundua kuwa amepungukiwa! na hapo inaonesha kuwa anahitaji msaada!

Miongoni mwa wanadamu, karibu kila mtu hujiona amepungukiwa, hata yule anayefikiri amefanikiwa sana, ahitaji msaada wowote, bado anajihisi amepungukiwa akubali au akatae. ndio maana kila mtu bado anataka kwenda kazini, hata kama bado anaonekana nazo pesa nyingi kiasi gani. 

vile vile kila mtu amepungukiwa, kwani hakuna mtu anayeishi bila kuhitaji huduma kadha wa kadha, hauwezi kukaa eneo moja ulilo lala au kukaa ama kusimama wiki au mwezi mzima, lazima utahitaji kuamka, kusogea. na pia huwezi tu uka kaa kimya kipindi chote, lazima utatamani kuzungumza na wengine. Bwana Yesu Kristo anasema "nyinyi hamwezi neno lolote" (Yohana 15:5b).
 
 Mambo muhimu ya kuangalia 
Ni vyema tuelewe kuwa, si wanadamu wamepanga kuomba, ila ni Mungu ndie anayepanga na kuwa na kiu kuwa sisi wanadamu twende mbele zake kuomba. Tazama Isaya 1:18=20, Mungu anasema " Haya njoni tusemezane..Dhambi zenu zijapokuwa nyekundu kama sana, zitakuwa nyeupe kama theluji; zijapokuwa nyekundu kama bendera zitakuwa kama sufu. Kama mkikubali mtakula mema ya nchi; bali kama mkikataa mtaangamizwa kwa upanga; maana kinywa cha BWANA kimenena haya". 

Mpendwa wangu, kwa maneno hayo tunaona kuwa maombi ni mazungumzo, mawasiliano kati ya Mungu na mwanadamu. Yeye (Mungu), anasema, na mwanadamu anasema, wote katika hali ya kusikilizana.

Cha kujiuliza hapa, Siku za leo, wanadamu wengi tunapoingia kwenye maombi, ni sisi tu  tunapokuwa ktk maombi, mara nyingi huwa tunamwambia Mungu mahitaji yetu au kumshukuru! Je, huwa tunamsikia na yeye akijibu au kuzungumza au kutueleza mambo kadha wa kadha? kama sivyo ni kwa nini hatumsikii?

Tuonane wakati mwingine tena!
Pastor Ibra Munanka
+255713714453
Tanzania

Command To Obey

Jesus not only offered this man a choice, but he commanded him to do something. He did not help him to his feet and fold up his mat for him. The man had to initiate to get up. Jesus would then do the rest. Jesus did not say, “I will put you in the pool.” That was what the man expected someone to do for him. God works beyond our expectations and in different ways. 

In this command Jesus was expressing to him that he was above and beyond the healing pool.

He has all the power in the world to heal, but there must be some faith on the part of the man. So he gave him an opportunity to exercise that faith. He told him to do three things, “Rise, take up and walk.”

Will Jesus save a man automatically without some response on the part of the man? No, but the moment a man sees himself as a lost sinner Jesus saves him. Jesus was not just asking him if he wanted to walk again. He used a word for whole that basically means, “fullness or wholesomeness.” Jesus was offering this man more than a strong pair of legs. He was offering him spiritual as well physical wholeness; he was offering the forgiveness of sin.

This man had a choice to make. Many people want the results of sin erased, but they do not want to give up their sin. They do not want to be made truly whole. They do not want the pardon that God offers them. This happens sometimes on the human level. Have you ever heard of any criminal who refuses an offer of clemency?

One of the strangest cases on record was that of George Wilson, who was sentenced to be hanged in 1829 by the state of Pennsylvania for mail robbery and murder. Before the sentence could be carried out, President Andrew Jackson pardoned George Wilson. The presidential pardon was sent to the governor of Pennsylvania and then to the warden of the penitentiary where George Wilson was incarcerated.

There the message was given to the condemned man. Wilson stunned everyone by refusing the pardon even though he knew it meant that the death penalty would be carried out. The officials did not know what to do. They could not just take Wilson to the front door of the prison and push him outside. It was a real legal tangle. 

The case ended up in the U.S. Supreme Court. In rendering the court’s decision, Chief Justice John Marshall said, “A pardon is a piece of paper, the value of which depends upon its acceptance by the person implicated. If it is refused it is no pardon.” As a result, George Wilson was hanged even though a pardon had been offered. He had made his choice.

A person can die and go to hell even though Jesus stretches out his arms to that person and asks, “Would you like to be made whole?” Pardon that is refused is no pardon. We must activate our will and receive what Jesus offers. Do you really want victory? You need not persuade our Lord to give it to you but must certainly permit him to do so.

Monday, June 27, 2011

Picha Yetu Jumatatu Hii

Pichani wanaonekana wanamuziki wa kikundi cha Mwanamama Rose Muhando wakiwa jukwaani katika mji wa nakuru nchini Kenya.Hii ilifanyika mwaka jana mwezi wa nane wakati wa ziara ya Rose Mhando nchini Humo iliyoitwa "THE NIBEBE TOUR"

Huima Band wafanya Tamasha jijini Mwanza


Kundi kongwe la muziki wa injili jijini Mwanza maarufu kama Huima`s Band lililo chini ya kanisa la FPCT, jumapili ya jana lilifanya Tamasha la kusifu na kuabudu katika ukumbi wa NYUMBANI HOTEL ulio katikati ya jiji la Mwanza. Tamasha hilo la kipekee liliambatana na tukio la kurekodi LIVE video ya album yao mpya. Kazi ya kurekodi video hiyo ilifanywa na kampuni maarufu kwa kazi hizo iitwayo MBC HOTMEDIA.
Huima ni moja kati ya makundi yaliyofanikiwa kuanzisha utaratibu wa kufanya matamasha na kuimba LIVE bila kutumia Playback. Huu ni mwanzo mzuri wa uimbaji uliotukuka kwa utukufu wa MUNGU.
Hapa ilikuwa mida ya sa nane mapema kabisa watu wakianza kuingia na huima wakijipanga tayari kwa shughuli
Kazi ikaanza ilikuwa ni patashika

Huima Band sio muziki tu hata Dressing code walijipanga

Watu waliacha viti, hahaaa Mungu ni mwema kwa wote wamchao

Sunday, June 26, 2011

Ephraim Sekeleti fears Piracy on his Work


Ephraim Sekeleti on one among of the Television interview in UK
The talented Gospel singer from Zambia Ephraim sekeleti has released his new song known as Uniguse Bwana, this is one among of the songs from his new album which is called ACHA KULIA. Before he launch that album he has been Thinking much on how to avoid his work from being pirated, he said to his fans all over the world I was born a gospel singer and whoever has pirated my swahili cd and added a secular song on my album that is anointed of God, may God deal with that person, father you know how much i love gospel deal with these people”

Below is Uniguse Bwana Video, You can easily view it.

Sunday Sermon......God Can Use Anyone



Despite of our weaknesses, but still GOD has got his good plans for us, what you have to know is that no matter your right or wrong you have to bow down before GOD and make him your everything. Our former spiritual leaders everyone had his weakness, no one who was perfect, but still GOD used them to change the life of other people. 

Read the list of the following people of GOD in the Bible plus their weaknesses. GOOD ENOUGH to learn here is that no matter what kind of weakness we posses but it is not an excuse for GOD to use us.
  • Moses stuttered.
  • David's armour didn't fit.
  • John Mark was rejected by Paul.
  • Timothy had ulcers.
  • Amos' only training was in the school of fig-tree pruning.
  • Jacob was a liar.
  • David had an affair.
  • Solomon was too rich.
  • Abraham was too old.
  • David was too young.
  • Peter was afraid of death.
  • Lazarus was dead.
  • John was self-righteous.
  • Naomi was a widow.
  • Paul was a murderer.
  • So was Moses.
  • Jonah ran from God.
  • Miriam was a gossip.
  • Gideon and Thomas both doubted.
  • Jeremiah was a bullfrog;
  • Just kidding -- he was depressed and suicidal.
  • Elijah was burned out.
  • Martha was a worry-wart.
  • Mary may have been lazy
  • Noah got drunk, and that's not all.

Don’t let a sin which you have commit to make you far from your GOD, but in any situation run unto him and you will be secured.

Mboya V.

Saturday, June 25, 2011

Upendo Kilahiro: Nilikataa uraia wa Canada, Afrika Kusini

Upendo Kilahiro
Upendo Kilahiro ni Mtumishi wa Mungu ambaye Sanjari na mumewe, humtumikia Mungu kwa njia ya uimbaji. Awali kabla ya kuhamia rasmi jijini Dar es salaam kwa sababu za Kihuduma, kabla ya hapo alikaa na kuishi kwa muda mrefu jijini Arusha. Katika huduma yake ya uimbaji kuna kipindi alipata fursa ya kwenda nchini Afrika ya kusini. Akiwa huko, alikokaa kwa muda mrefu alifanikiwa kufanya huduma katika maeneo mbali bali ya nchi hiyo na aliweza kukubalika sana nchini humo.

Wakati wa harakati hizo za kihuduma wengi wa Raia wa Afrika ya kusini akiwemo mwanamama Rebeka Malope waliwahi kumuomba abadili uraia wa Tanzania na kuchukua uraia wa Afrika ya kusini ili aweze kufanya kazi zake kwa uhuru zaidi nchini humo lakini Upendo alikataa kata kata.

Kutokana na msimamo wake huo Malope alimuomba upendo kuwa msemaji wake katika ukanda wa Afrika Mashariki kazi anayoifanya mpaka sasa.  Hali  hiyo ilijitokeza tena alipokuwa ameenda nchini Canada Kihuduma., akiwa huko wenyeji wake na raia wengine nchini humo walimshauri vivyo hivyo lakini Upendo anasema “mimi niliwaambia kuwa ni Mtanzania na sitoweza kuisaliti nchi yangu hata kama ipo vipi”

Tofauti na uimbaji, Upendo Kilahiro amekuwa mstari wa mbele katika kuisaidia jamii ya watanzania wenye hali duni kimaisha na hii ilipelekea shirika la Afya ulimwenguni (WHO) kumchagua kama balozi wa shirika hilo nchini Tanzania kwa mwaka 2009.

Upendo kwa kushirikiana na Taasisi ya Christian Directory & Consultancy, alifanya tamasha kubwa la muziki wa Injili lililofanyika mkoani Arusha, lililokuwa na lengo la kuchangisha fedha za kuwasaidia wagonjwa wa Taasisi ya Saratani ya Ocean Road, ambalo lilikwenda sanjari  na utambulisho wa Albamu yake iitwayo ‘Asante Yesu’

Usijisumbue wala kuhangaika katika kufanya uamuzi wowote

Mwl Christopher.Mwakasege akiwa madhabahuni akifanya huduma
Katika kufanya maamuzi mazuri maishani, ni vizuri kuwa makini mno kwa kuwa uamuzi wowowte utakaouchukua ni mbegu, na mbegu hiyo unaipanda kwa kuufanyia kazi uamuzi huo. Hivyo usiwe na uamuzi ambao hauko tayari kuvuna kutokana na matokeo hayo.

Katika maisha kuna maamuzi mengi ambayo huambatana na mahangaiko na usumbufu mwingi ndani ya MOYO wa mtu.Lakini maamuzi mengine huwa hayana mahangaiko wala usumbufu, na kwa sababu hiyo unajikuta unayanya kirahisi.

Usije  ukaingia kwenye mtego wa kuona maamuzi yaliyo magumu ndio ya kumshirikisha Mungu pekee, nay ale yaliyo mepesi ndiyo unayoyaamua bila kumshirikisha Mungu. Neno la Mungu linatuambia hivi “ Msijisumbue kwa neon lolote, bali katika kila neno kwa kusali na kuomba,pamoja na kushukuru, haja zenu na zijulikane kwa Mungu.” ( Wafilipi 4:6).

Yesu Kristo aliwahi kusema Hivi, “…..pasipo mimi ninyi hamuwezi kufanya neno lolote”(Yohana 15:5). Hii inamaana ni pamoja na kufanya maamuzi!. Hatuwezi kufanya maamuzi mazuri pasipo msaada  na Uongozi wa bwana Yesu.

Ndiyo maana tunaambiwa hivi”Basi nyenyekeeni chini ya mkono wa mungu ulio hodari, ili awakweze kwa wakati wake, huku mkimtwika yeye fadhaa zenu zote, kwa maana yeye hujishughulisha na mambo yenu” ( 1Petro 5:6-7)

Hebu linganisha maneno hayo na haya ya Mithali 3:5,6 yanayosema “ Mtumaini Bwana kwa Moyo wako wote wala usizitegemee akili zako mwenyewe, katika njia zako mkiri yeye, naye atanyoosha mapito yako”

Ukijua haya utajizoesha  kumwomba Mungu kila siku ili aongoze maisha yako, kwa maneno Mengine utakuwa na maana ya kwamba unataka aongoze maamuzi yako. kumbuka maisha ya mtu ni mtiririko wa maamuzi yake mwenyewe naya watu wengine.

Mwl C.Mwakasege

Thursday, June 23, 2011

OVERCOME YOUR FEARS BY WISEMEN JOHN CHI


Replete with a spiritual aura, following melodies released by the choir and hosting a congregation agog for the day’s service, the auditorium readily welcomed Wise Man John Chi who came in with a message of God entitled, Overcome Your Fears. Psyching up his listeners for the sermon, the wise man celebrated the joy of being at peace with God. In his words, the peace of conscience from God produces eternal joy.

Wisemen John Chi

Daniel never feared the lions’ den because he had absolute confidence in God. Being thrown into a dry pit was not a good thing but Joseph never feared it because of his absolute trust in God. What is your lions’ den? What is your dry pit? He rhetorically assured his listeners of God’s omnipotence. Scaling up their faith further, the wise man enjoined them to never for a moment doubt that God’s ability cannot put them over. As his proof text, the wise man opened the Bible to Romans 8:15 and averred that God does not give a spirit of fear but that of sunshine.

He regretted that many people have surrendered to their fears while their spirits hunger for a miracle. To the people of the world, he continued, trouble is a poison but to God’s people it serves as a tonic to enhance our aspirations. Troubles and aspirations serve to move us closer to God. The way and manner you react to your situation matters. Prophet Elisha’s spiritual reaction to his situation is instructive to many Christians. His word to his servant is equally instructive.

His servant’s focus was more on the immediate surroundings than what God had to say about their situation. Elisha’s voice was not only of faith but also of finality. Do not fear the troubles of this world; instead, trust in the glory of God. There is a superior realm that controls both the visible and the invisible worlds.

This being the case, you will see appointment in disappointment. Fear and insecurity dominate a life without faith. Fear prevents one from making important decisions in life. We need to pray that God open our understanding like Elisha’s. In the midst of trouble, the Holy Spirit will lead you to victory.

Friends On Friday Events Yasubiriwa kwa Hamu

07/01/2011 6:30 pm
07/01/2011 11:00 pm
Africa/Dar es Salaam
Venue: 
Atriums Hotel at Sinza Africa Sana Area
Description: 
Live Performance ya "The Whispers Band" Wazee Wa "Nina Baba Yangu Asiyeshindwa Kamwe" wakipiga Miziki Ya Jazz, Miriam Lukindo wa Mauki akifanya "Live Performance" Ya South African Music Test, Christina Shusho "Live Performance" ya Slow Music test and "Zuku", President Chavalla akifanya Live Performance ya Comedy, underground Musicians kama Sarah Shilla atafanya "Live Performance", Chris Mauki atafanya Live Talk Show kwenye eneo la Mahusiano, Prosper Mwakitalima ataongoza Talk "Why Most Of Christians Businesses Collapses" Show Nzima Itasimamiwa na Ma-Mc Papaa Sebene (Samuel Sasali) na Mc-Luvanda.(Antony Luvanda)....Hii yote ni Katika FRIENDS ON FRIDAY.
 
Mbali ya Yote, This will be a like a "Candle dinner" chakula cha usiku Kitatolewa Bureeeeee, a food and not just a snacks and soft drinks, Mazeeee ni Chakula, Networking, Live Performance and Talks,ni Katika FRIENDS ON FRIDAY.
 
Tunatengeneza Mtandao wa Wafanyabiashara, Wanataaluma na Wajasiriamali "USISAHAU" Business Card yako. It have never happened in the Christian World, But This Time, Live Band, Talks, Business Networking and Full of Entertainment at Atriums Hotel Sinza Africa Sana. Come and Sell Yourself for Free. Haya yote kwenye FRIENDS ON FRIDAY. Ijumaa ya tarehe 01 Julai, 2011 saa 12.30 jioni Mpaka Baadae.
Njoo Ukiwa umevalia Chochote kinachoonekama chenye rangi Nyekundu.
 
Kwa Mawasiliano Zaidi kuhusu Event Hii na Ununuzi wa Tickets, Wasiliana na Wadau wafuatao.
 
Papaa (Samuel Sasali) 0713 494110
Chris Mauki 0713 407182
Antony Luvanda 0715088461
Prosper Mwakitalima 0713 905118
Protace Godwin 0767832891
James Temu 0713 763939

Tuesday, June 21, 2011

Lazima uisome Hii: Mahakama ya Ulaya yaingilia kati kuhusiana na Haki za wakristo


Serikali ya Uingereza imeambiwa iweke bayana kuhusu kama haki za wakristo na ukristo zimewekwa kando na Mahakama ya sasa ya nchi hiyo. Ombi hilo limeombwa na Mahakama ya haki za binadamu barani Ulaya katika mji wa Strasbourg kwa niaba ya wakristo wane ambao wameadhibiwa kutokana na kuonyesha imani zao kwenye vituo vyao vya kazi.


Wakristo hao wameamua kwenda kwenye mahakama ya Bara la ulaya kutokana na rufani yao ya kupinga kuadhibiwa kutupwa mbali na mahakama ya Uingereza. Wakristo hao wa kwanza ni Nadia Ewedia ambaye yeye ni mfanyakazi wa shirika la ndege la Uingereza(British Airways), Nadia alipigwa marufuku kuvaa msalaba kwenye sare zake za kazi.

Kituo cha sheria cha Kikristo nchini Uingereza(Christian Legal Centre) kimeamua kuwasaidia wakristo wawili ambao nao wameadhibiwa na mahakama ya nchini Uingereza. Wakristo hao Gary McFarlane na Shirley Chaspin kila mmoja amekutwa na masahibu tofauti.

Gary McFarlane ambaye ni mshauri wa mambo ya Mahusiano ambaye alifukuzwa kazi kutokana na kugoma kutoa ushauri kwa ndoa ya mashoga ambao walikuja kwake kutaka ushauri. Shirley Chaspin ambaye kitaaluma ni nesi , yeye alifukuzwa kazi  kwa kuwa alikatazwa kuingia kwenye wodi za hospitali aliyokuwa akifanyia kazi huku akiwa amevaa mkufu shingoni(necklace) wenye alama ya Msalaba. Baada ya kugoma kuvua msalaba shingoni Shirley aliondolea kazini.

Mtu wa nne ni msajili wa  wa zamani wa ndoa ambaye aliadhibiwa na Baraza la Kaskazini la jiji la  London mara baada ya kukataa kufungisha ndoa ya jinsia moja.

Mkurugenzi wa kituo cha sheria cha kikristo Bw Andrea Minichiello Williams amesema  “inaonekana wazi kuwa mahakama ya uingereza haiitendei haki imani ya kikiristo, kama ombi letu kupitia mahakama ya bara la ulaya likifanikiwa, hii itabadilisha hali nzima iliyopo na kuwapa uhuru wakristo kwenye vituo vyao vya kazi”

Mapema mwaka huu mahakama ya Ulaya iliiruhusu nchi ya Italia kuendelea kuweka alama ya msalaba kwenye madarasa ya shule za nchi hiyo mara baada ya mabishano makali kisheria kati ya wanasheria wa nchi hiyo na wale wa mzazi mmoja mmama aliyekuwa akidai uwepo wa misalaba madalasani unaondoa haki yake ya kumfundisha mwanae kuhusu Imani ya mwelekeo mwingine tofauti na ukristo.


Source: Christian Post 

Historia ya Mwanauziki wa Injili K` Basil

Kashumba Basil (K` Basil)
Basil Kashumba ni Kijana aliyezaliwa Mwaka 1978 Mkoani Kagera katika wilaya ya Bukoba, toka kipindi akiwa mdogo alikuwa akipenda sana muziki na tofauti na wanamuziki wengine pamoja na kupenda sana Muziki aliyamudu vyema masomo yake darasani.

Bidii yake kimasomo ilimfikisha Chuo Kikuu cha Dar es salaam (UD) ambako alihitimu shahada ya Jiografia na Mazingira. Akiwa chuoni  UD ndipo alijijengea jina kubwa kupitia muziki wa Duniani(Circular Music). Watanzania wengi wamefanikiwa kumfahamu vizuri K Basil mara baada ya kutoa nyimbo yake ya Riziki aaakiwa na Mwanadada Stara Thomas ambaye naye kwa sasa inaaminika kuwa ameyakabidhi maisha yake kwa Kristo.

Stara Thomas naye inaaminika kwa sasa ameokoka
Pamoja na mafanikio aliyokuwa nayo kwa kipindi chote hicho, K Basil anasema maisha yake yalitawaliwa na na taabu nyingi. Pombe ndio ilikuwa rafiki mkubwa na kiongozi wa K Basil. “Nilijaribu kuacha Pombe lakini ilishindikana, nilkuwa mlevi kupindukia na mara nyingi nililala Bar mpaka nikawa kero kwa Rafiki zangu.”

Achilia mbali ulevi na uzinzi anasema siku moja akiwa amelewa aliwahikupata ajali mbaya ya gari, na katika aliwahi kutupwa jela mara kadhaa kutokana na mikasa ya hapa na pale.” Nimepitia misukosuko mingi nay a Ajabu lakini sasa  nimekuwa mtu huru, mwenye amani, upendo na Faraja kutokana na kumtegemea Mungu”

Katika vurugu zangu zote hizo “siku moja nikasikia Sauti ndani yangu ikiniambia yanipasa nibadilike, niliamua kumshirikisha dada yangu kile nilichokiskia toka ndani na nikamwambia kuwa nahitaji kuombewa. Niliamua kwenda kanisani ambako niliongozwa sala ya toba  na huo ukawa mwanzo wa safari yangu mpya ya maisha”

Kwa sasa ninafanya Kazi ya Mungu kwa Moyo mmoja na ninaendelea na huduma ya uimbaji, ninamshukuru Mungu kwa mafundisho niliyopata kupitia kwa Mchungaji wangu Josephat Gwajima wa Kanisa la Glory of Christ maarufu kwa jina la Ufufuo na Uzima lililoko kawe jijini Dar es salaam.

Basil anasema baada ya kumrudia Mungu na kusimama imara katika wokovu n wakati wake mwafaka kuwarudisha kwa kristo watu wengine waliopotea katika ulimwengu wa anasa na dhambi kama ilivyokuwa kwake. Hivi sasa amezindua album yake iitwayo “YESU ANANIPENDA” yenye jumla ya nyimbo kumi zikiwemo Namjua, wakatina bahati, Wewe ni Baba, Rudisha, Utukuzwe, Moyo, Tunasonga Mbele, Mama na Ahsante Yesu iliyobeba jina la album.

Tarehe 5/12/2010 Basil alifunga ndoa na Perida Mdegela ambaye wanaishi naye kwa furaha mpaka hivi leo. Anasema anamshukuru Mungu kwa kuwa kwa sasa akili imetulia. Aidha Basil alipoulizwa anazungumzia vipi wokovu wa Mwanamuziki Stara Thomas Basil anasema “Kwa hakika hizi ni Habari Njema ingawa sijui ni nini kilichomuongoza, nafikiri kuungana naye tena kufanya nyimbo ya Injili”.
Basil akiwa na mkewe Pelida Mdegela
 Kwa sasa Basil ni mmoja wa wachungaji katika kanisa la Glory of Christ akimtumikia Mungu chini ya Askofu Gwajima. Hosanna Inc inamtakia kila la Heri  Basil kwenye safari yake ya wokovu tukiamini Basil ni moja kati ya vitendea kazi katika ufalme wa Mungu kwa ajili ya Kuujenga na Kuuimarisha Mwili wa Kristo hapa Tanzania na duniani kwa ujuma.

Jane Misso - Omoyo



Monday, June 20, 2011

Uzinduzi wa Album ya MIRIAM LUKINDO Ni Asubuhi Katika Jiji la MWANZA

Mwanamuziki Mahiri wa Nyimbo za Injili Maarufu kama Miriamu Lukindo, jana katika uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza amefanikiwa kuzindua album yake iitwayo Ni Asubuhi. Uzinduzi huo wa kipekee ulifanyika kwa udhamini Mkubwa wa Haak Neel Production ambao walikuwepo na timu yao nzima kutika Dar es salaam.

Miriamu na Haak Neel Production wamefanikiwa kufanya kile kitu ambacho wengi wa mapromota wameshindwa, kwa Mara ya Kwanza Mwanza Tamasha limefanyika LIVE pasipo Playback. Kwa hili ni pongezi kubwa Miriamu. Miriam alikuja na timu yake ya wapigaji wa vyombo pamoja na watu wa back-vocal toka Dar es salaam na kiukweli walionekana dhahili wamejipanga kwa ajili ya kufanya Live kitu ambacho walifanikiwa.

Katika hali ya kuonekana kama mazoea ya Playback, mara wanamuziki wengine kama Martha Mwaipaja, Upendo Nkone, Neema Mwaipopo walipokuwa wakiimba kwa Playback wakazi wengi wa Mwanza walionekana kurespond kwa kuchangamka, ila Pindi Miriamu na Crew yake walipopanda Jukwaani na Kupiga LIVE. wakazi wa Mwanza walionekana kumshangaa Miriam Kuanzia Vocal Capacity aliyonayo, timu yake ya kumback pamoja na Crew ya wapigaji ambayo kiukweli jamaa walishangaza watu kwa uwezo wao wa kuchezea vyombo. Kwa huu ni Tamasha la kwanza la muziki wa injili kwa Ubora jijini Mwanza.


Kikosi kazi cha Miliamu Kikishuka garini tayari kwa shughuli

Miriam Lukindo akiwa Jukwaani 

Kijitonyama Upendo Group walikuwepo kumsindikiza Miriam

Neema Mwaipopo ha haaaa Raha Jipe Mwenyeweeeeeeeeeeee

Upendo wa Yesu Wanizunguka ilikuwa ni Patashika Upendo Nkone alipopanda Jukwaani

Ilikuwa ni Patashika

Miriam Na Kundi lake wakiwa Jukwaani

Miriam On STAGE, ilidhihirika wazi kuwa huwezi mtenga Miriam na KUABUDU,hapo ilikuwa mwanzoni kabisa mwa tamasha akiimba Amen Amen 
Miriam Lukindo akiimba Ni Asubuhi

Crew ya wapiga Vyombo, wa Kwanza kulia ni Bro Amani ambaye ni MUSIC DIRECTOR Miriam, Miriam anasema ni ngumu yeye kuimba pasipo amani kuweka mambo sawa. Kwenye Drumz anaonekana Bro Kapama akiwajibika

Crew Nzima ya Haak Neel Ikiwajibika

Edward Lowasa, atabiriwa na TB Joshua?

Mbunge wa Monduli Mh Edward Lowasa akiwa kwa TB jOSHUA kama anavyoonekana kwenye Emmanuel TV, 12 June 2011

Gazeti hili limepata ushahidi wa maandishi ya mkono wa Beatrice mwenyewe yanayoonyesha kuwa amekuwa mfuasi muhimu wa Lowassa kiasi cha kushawishi wengine kujiunga katika mtandao wake.

Akiandika kwa Pindi Chana, mbunge wa Viti Maalum (CCM), tarehe 14 Februari mwaka huu, Beatrice alieleza mambo matatu katika ujumbe wake kwa Chana.

Kwanza, kumshukuru Chana kwa kukubali kulinda kura zake. Pili, kumshawishi kumuunga mkono Lowassa. Tatu, kumweleza juu ya ulokole wake na “mtumishi aliyepakwa mafuta” kutoka Nigeria.

Beatrice anamwambia Chana kuwa Lowassa ndiye kampeni meneja wake. Hii ilikuwa katika uchaguzi wa makamishina wa Bunge; nafasi aliyogombea na kushinda.

“Mungu ni wa ajabu, (Lowassa) ameniombea kura pasipo maelezo. Ameandaa lunch na dinner (vyakula vya mchana na usiku) ambako amekuwa akiniombea kura. Ana njia za ajabu za kufanya mambo. Ahsante kwa kukubali kuhesabu kura,” inasema sehemu ya ujumbe huo.

Chana, ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati Kuu (CC) na Halmashauri Kuu (NEC) ya CCM, ndiye alihesabu kura za Beatrice kwenye uchaguzi wa kutafuta makamishina wa Bunge.

Ni kwenye ujumbe huo ambamo Beatrice anatoboa kuwa siri ya ushindi wake ni Lowassa aliyekuwa kampeni meneja wake.

Katika kusisitiza hoja yake, Beatrice anasema, “Nimezungumza na TB Joshua wa Emmanuel TV Nigeria aliyenipa unabii kuwa rais ajaye Tanzania ni Edward Lowassa, nikamuambia haiwezekani kwani amechafuka sana.”

Anasema Joshua alimjibu, “…alikuwa amechafuka sasa amesafishwa kwani katubu. Akaniambia his past is over (maisha yake ya nyuma si kitu). Akaongeza kwa kusema, wewe Beatrice ningeangalia your past (maisha yako ya nyuma) pengine nisingekuombea kabisa. Akasema my past is over (hajali maisha yangu ya nyuma),” inasema sehemu ya ujumbe huo wa Beatrice.

Hata hivyo, Beatrice hakueleza katika waraka wake kwa Chana maisha yake ya nyuma yalikuwa vipi. Wala hajaeleza alifanya nini, hadi kuamini kuwa kama Nabii Emmanuel angeyatazama, basi asingemuombea.

Kuvuja kwa taarifa hizi kumekuja wiki tatu baada ya Lowassa kuchaguliwa kuwa mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge, Ulinzi, Usalama na Mambo ya Nje.

Mume wa Beatrice, William Shelukindo alikuwa mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini ambayo iliongoza harakati za kuundwa Kamati Teule ya Bunge iliyochunguza mkataba tata wa Richmond.

Ni taarifa ya kamati hiyo iliyosababisha Lowassa kujiuzulu wadhifa wake wa waziri mkuu, Februari 2008.

Kwa mujibu wa watu waliokaribu na Beatrice na kwa ushuhuda wake mwenyewe, mwanasiasa huyo ameamua kujisalimisha kwa Lowassa kwa kile kinachoelezwa kuwa “Lowassa ndiye rais ajaye wa Tanzania.”

Aidha, kupatikana kwa taarifa hizi kumekuja huku kukiwa na juhudi kubwa zinazofanywa na Lowassa na kundi lake kutaka kujisafisha kwa lengo la kujitosa katika kinyang’anyiro cha urais mwaka 2015.

Miongoni mwa mikakati aliyojiwekea Lowassa na kundi lake ni kujitokeza katika maeneo yote muhimu na kutoa kauli ambazo zitafanya wananchi waanze kumkubali kuwa ni kiongozi anayefaa.
MH Lowasa akiwa na Familia yake Mkewe Regina Lowasa na Binti Yao
Katika kutekeleza mkakati huo, Januari mwaka huu, Lowassa alijitokeza kuzungumzia vurugu zilizotokea mkoani Arusha zilizotokana na mvutano katika uchaguzi wa meya wa jiji hilo kati ya CCM na CHADEMA.

Katika mnyukano huo, watu watatu walipigwa risasi na polisi na kufariki dunia baada ya polisi kutumia nguvu isiyo ya kawaida kuzima maandamano ya CHADEMA.

Kauli hiyo ya Lowassa ilikuwa tofauti na msimamo wa Katibu Mkuu wa CCM, Yusuf Makamba aliyemtaka kuwasilisha maoni yake katika vikao vya chama badala ya kutumia vyombo vya habari.

Kauli nyingine ya Lowassa ilihusu nyongeza ya viwango vya mishahara kwa wafanyakazi, kutokana na kile alichoita mfumuko wa bei kuwa mkubwa.

Bali wiki moja iliyopita, Naibu Katibu Mkuu wa vyama vya wafanyakazi nchini (TUCTA), Nicholas Mganya alimtuhumu Lowassa kwa kutoa kauli hiyo akisema ana ajenda ya siri nyuma yake.

Mgaya alisema TUCTA haihitaji msaada wa Lowassa katika kusimamia madai yao. Alisema “mbunge huyo wa Monduli inaonekana ana ajenda yake mgongoni.”

Hatua nyingine ya Lowassa katika kujikarabati kisiasa ni kugombea na kupata nafasi ya Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama.

Lowassa amekuwa pia akihudhuria hafla nyingi, hasa za madhehebu ya Kikiristo (KKKT) ambao anaonekana akitoa maoni mbalimbali kama ilivyokuwa Jumapili iliyopita ukumbi wa Dimaond Jubilee kwenye uzinduzi wea albamu ya moja ya kwaya za injili.

Kwenye kusanyiko hilo, Beatrice naye alikuwepo. Lowassa alimtaka asome maoni ya gazeti la The Citizen juu ya ushirikina uliokithiri nchini; jambo ambalo Lowassa alizungumzia kwa urefu.


MwanaHALISI lilipowasiliana na Beatrice ili kupata maoni yake juu ya ushwahiba wake mpya na Lowassa, mahojiano yalikuwa kama ifuatavyo:

Mwandishi: Tusaidie maelezo kidogo juu ya ujumbe uliomwandikia Mheshimiwa Pindi Chana kumjulisha kuwa uliambiwa Edward Lowassa atakuwa rais. Ni kweli?

Beatrice: Barua ameandika nani na umeipata wapi?

Mwandishi: Hii barua fupi – memo ndani ya Bunge, uliposema Mheshimiwa Lowassa ambaye amesimamia vizuri kura zako za ukamishna wa Bunge.

Beatrice: Sina taarifa hiyo. Wala siikumbuki. Unajua ndani ya Bunge tunaandikiana mambo mengi, tena mengine ya utani tu. Na mimi na Mheshimiwa Chana sote ni “walokole,” tunafanyiana utani sana.

Mwandishi: Kwani mheshimiwa Shelukindo, mkiwa ndani ya bunge kuna utani mwingi, kwamba huwa mnaandikiana utani sana?

Beatrice: Kabisa, unajua tunaandika mambo mengi. Na kama unaandika kwa utani kwa mwenzako inabaki hivyo ni utani tu. Sasa tatizo hao wanaowaletea mambo haya wanatumia mambo haya kutafuta mipango yao ya kufikia mwaka 2015.

Alisema, “Mimi najua hakuna anayenibeba ndugu yangu. Mimi ni very solid (ngangari), sibebeki. Nakwambia, mbona mimi nina nguvu nyingi mimi mwenyewe; sihitaji kubebwa. Najua wanajaribu kuonyesha tunabebwa, lakini huo ni ujinga wao wa kufikiri.

Mwandishi: Mheshimiwa Shelukindo, kwani nyie waheshimiwa huwa mnatafutana (kufitiniana)?

Beatrice: Hiyo inafanyika sana, watu wakishakuwa na mambo yao wanatumia wengine kutimiza dhamira zao. Lakini mimi ninafikiria wananchi. Nimeshaamua kwamba Beatrice nashughulikia shida za wananchi jimboni. Ninatafuta njia za kuwaondolea umasikini, njaa na mambo kama hayo. Sasa wengine wanatafuta tu pa kunishika.

Mwandishi: Kwa hiyo Mh. Lowassa ndiye alikuwa kampeni meneja wako katika kutafuta ukamishna pale bungeni, au siyo Mheshimiwa?

Beatrice: Lakini kama anafanya kazi ya kampeni vizuri; ni vizuri tu. Isipokuwa kila mtu anajichukulia mwenyewe alivyo. Mimi ni mtu wa kazi sihitaji kusimamiwa hivyo. Na hebu tujadili hili; unajua kaka nyinyi mnafanya kazi kubwa. Sasa hii kusikia, sijui MwanaHALISI hivi, sijui hivi, pengine kuna watu wanachomekea vitu vyao. Tunapenda kazi yenu.

Mwandishi: Mheshimiwa nakushukuru sana.

Beatrice: Karibu sana tutafanya kazi pamoja.

Akiwa Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini, mume wa Beatrice, William Shellukindo, alikuwa na msimamo mkali dhidi ya watuhumiwa wakuu wa ufisadi nchini na hiyo ndiyo inayoelezwa kuwa sababu ya kushindwa kwake ubunge katika mchakato wa ndani ya CCM.
 


Shellukindo alikuwa mbunge wa jimbo la Bumbuli mkoani Tanga kwa zaidi ya miaka 20, alishindwa katika kura za maoni na January Makamba, mtoto wa katibu mkuu wa CCM anayetajwa kuwa mfuasi wa mtandao wa Lowassa.
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...