Wednesday, February 29, 2012

Mtoto wa Nabii GeorDavie aitwaye Nisher atoa shukrani kwa Baba yake


Nisher
Nisher ni mtoto wa Mtumishi wa Mungu Mh Nabii GeorDavie anayeongoza huduma ya Ngurumo ya Upako yenye makao yake jijini Arusha. kwa muda sasa Nisher amekuwa akijihusisha na muziki(Gospel and Non Gospel Music),toka mwaka huu uwanze ndoto yake ya kuwa na studio kubwa kwa ajili ya kurekodia aina zote za Muziki imekamilika na sasa anamiliki studio ijulikanayo kama NISHER RECORDS iliyoko jijini Arusha.

Kipekee nimeanza kumfahamu Nisher takribani miaka mitatu iliyopita nikiwa mwaka wa pili chuoni pale St Augustine Univ, na hii ni baada ya kuona quality ya Video production ya Ziara na huduma za Nabii Geordavie,nilipouliza who is behind this  unique art nikaambiwa ni mwanaye anaitwa Nisher.Unaweza mjudge Nisher vyovyote but pamoja na hayo Nisher is Talented, hufanya Graphics za viwango vya juu kuanzia Video mpaka Photo Pictures

Baada ya studio yake kuanza kazi studio jijini Arusha huku ikigharimu Kwa haraka haraka zaidi ya 15M inadeal na Video na AUDIO,kwa kutambua mchango wa Baba yake katika maisha yake na katika mafanikio yake Nisher aliamua kurekodi Mini Video Clip kwa ajili ya kumshukuru baba yake kwa hatua aliyomfikisha. Katika Video Clip hiyo, Nisher anasema mafanikio yake yote yanatokana na baba yake.

Nisher akiwa ndani ya Nisher Records
Akasema”Nisher records it has been possible because of my daddy,My Daddy alinisaidia ku-put kila kitu Together Financially pamoja na kwenye maduka (katika kuchagua vyombo) kwa kuwa amekuwana historia kubwa na muziki kuliko mimi,amekuwa akifanya Muziki kwa zaidi ya Miaka Arobaini sasa.Namshukuru sasa baba kwa kunisaidia na kwa kuona kuwa i can do better, i can be a better person, napenda kukushukuru Honestry mbele ya watu wote wanaoangalia Video hii kwamba your my HERO and God Bless you for that, naamini Nisher Records and Nisher Entertainment it will be Big Company” 

Katika Maisha ya wokovu,watu wengi waliookoka huwa wako mstari wa mbele katika kukosoa na kulaunu namna watoto wa watumishi wanavyoishi na namna wanavyouchukulia wokovu.Kwa upande wa pili kanisa linasahau wajibu wake kwa vijana na kubaki kuwalaumu na kuwafanya ndio Hot topic popote pale hususani wanapotoka nje ya mstari.Pamoja na yote hayo Mungu anabaki kuwa Mungu kwa kuwa Habadiriki, na kanisa lapaswa kusimama na kuwaombea watumishi  pamoja na familia zao pasipo kuwanena vibaya.


1 comment:

  1. Marekebisho kaka, hiyo studio ni zaidi ya milioni 150 sio milioni 15

    ReplyDelete

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...