Monday, February 27, 2012

SAUT Wamwadhimisha Bwana katika Campus Night


Lile Tamasha la kusifu na kuabudu lililokuwa likisubiliwa kwa hamu na wanachuo na wakazi wa Mwanza lijulikanalo kama campus Night, ijumaa iliyopita lilifanyika  katika viwanja vya shule ya msingi Nyamalango iliyoko Nyegezi jijini Mwanza  karibu kabisa na Chuo kikuu cha Mtakatifu Augustine(SAUT).Vikundi kama TAFES SAUT,KingDom Worshipers,CASFETA,HHC Praise and Worship Team pamoja na kihaire Band vilimuadhimisha Bwana Viwanjani hapo.

Maandalizi ya  Tamasha hilo yalifanyika  kwa ushirikiano mkubwa kati ya TAFES-SAUT na kanisa la HIGHWAY OF HOLLINES  linaloongozwa na Akofu Eugine Mulisa. Tofauti na Matamasha mengine Tamasha hili lilikuwea la kihistoria kwa kuwa lilikuwa ni tamasha la kwanza kurushwa LIVE kupitia kituo cha redio cha  ALIVE FM ambapo Nyamiti Kanyola mmoja wa watangazaji wa redio hiyo aliongoza jopo la ufundi kutoka ALIVE FM katika kuhakikisha walioko majumbani wanakutana na ngumu za Mungu.

Mtumishi wa Mungu Askofu Eugine Mulisa akifundisha Neno la Mungu kisha akaongoza idadi kubwa ya watu sala ya toba  baada ya kuamua kumpokea YESU kama Bwana na mwokozi wa Maisha yao.Tofauti na Campus Night zilizowahi kufanyika na Maombezi kuwa ni sehemu tu ya Mahubiri, kilichojiri kwenye Concert hili ni Tofauti kwani waliolipuka Mapepo walikuwa ni wengi mno hivyo kupelekea wahudumu na watumishi kuwa na kazi ya ziada katika kufanya huduma ya Maombezi.
Evelyn Andrew New member wa bend ya KingDom Worshiper na mtangazaji wa Kwa Neema Fm akiwa on stage.

Tafes Saut Praise and Worship Team ikihudumu



Mtumishi wa Mungu Askofu Eugine Mulisa akifanya maombezi

Maombezi yakiendelea



Watumishi wakiendelea na maombezi




Kingdom Woshipers on Stage

1 comment:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...