Wednesday, March 14, 2012

Apostle Mwingira aongelea siasa ya Tanzania


Nabii Josephat Elias Mwingira kushoto akiwa na Rais Jakaya Mrisho Kikwete


Saa nyingine najiuliza hivi nchi hii haina Serikali?, lakini nagundua kwamba nchi yeyote selikali yake ikiwa ovu, watu wake wanateseka
Ni aibu kwa wageni kuonekana wana nguvu katika nchi hii, na Raia wanaonekana kama wakimbizi katika nchi yao


Jumapili iliyopita Mtume na Nabii Josephat Mwingira wa huduma ya EPHATA aliongelea kwa kifupi siasa ya Tanzania kabla hajaanza kufundisha somo lisemalo NGUVU YA MUNGU IWEZAVYO KUMSAIDIA MTU AWEZE KUTOKA MAHALI.Katika ibada hiyo iliyokuwa ikirushwa LIVE na kituo cha cha Television cha TRENET kinachomilikiwa na huduma hiyo mtumishi wa Mungu alisema

“Nchi hii sio mali ya Serikali sio mali ya chama cha siasa,ni nchi ya watanzania wenye sura ya kitanzania ambao Mungu amewaweka Tanzania. Awe mjinga,Tajiri Maskini au Mwerevu ni Kwake hapa.Inasikitisha ,ni aibu kwa wageni kuonekana wana nguvu katika nchi hii, na Raia wanaonekana kama wakimbizi katika nchi yao. Na mi nnafahamu sana wanaposikia mi naongea hivi wanatafuta kila namna kunimaliza hawawezi washindwe katika jina la Yesu”

Mtumishi Mwingira aliendelea kusema “Saa nyingine najiuliza hivi nchi hii haina Serikali?, lakini nagundua kwamba nchi yeyote selikali yake ikiwa ovu watu wake wanateseka,lakini Mungu ataiponya Tanzania. Najua kwa machozi yangu, kwa machozi yenu na machozi ya watanzania wengi ambao wanatoa machozi kwa ajili ya nchi hii, Mungu atashughulika na majambazi, wahuni wezi wala rushwa, Mungu atapunguza siku zao, katika kuishi kwao watakufa kwa kilo mbilimbili watakufa kwa presha, watakufa kwa ukimwi,kisukari yatawapunguza mpaka wafe tu,na wataondoka tu”.

Akazidi kusema “Na kwa moyo wangu wote kama Mungu alivyoniambia watawala ambao wanategemea uchawi, kuanzia wachawi na wenyewe watakufa.watanzania wenzagu mzidi kuipenda nchi yetu, mzidi kuiombea nchi yetu Mungu ataibadilisha Tanzania. Katika kufahamu kwangu sijaona chama kizuri,YESU NI MZURI.Tukimpa Yesu maisha yetu Yesu ataibadilisha Tanzania, ninaamini wakati wa Yesu kujitokeza Afrika umefika,wakati wa Yesu kubadilisha tawala za Afrika umefika.Ninaamini kwa MOYO WANGU WOTE, Human right ambazo zinazungumza u-gay hazitotokea Tanzania” alimaliza Apostle Mwingira

3 comments:

  1. SAFI MWINGIRA KAMA NA PASTORS WENGINE TUNGEKUWA NA UJASIRI HUU INGESAIDIA SANA KUFIKA TUNAKOTAMANI KUFIKA

    ReplyDelete
  2. DEAR FRIENDS, THIS IS VEEEERY IMPORTANT PLEASE! PLEASE PLEASE ! ! ! WE NEED TO EXAMINE AND TEST THE CHURCHES AND DENOMINATIONS WE ARE PART OF, TO SEE IF WE ARE ON THE RIGHT TRACK TO ENTER INTO THE KINGDOM OF GOD. IT IS EXTRMELY CRITICAL AND URGENT THAT WE DO THIS EVERYDAY WHILE WE'RE STILL ALIVE. IT TAKES ONE UNFORTUNATE CAR WRECK/ACCIDENT, OR ONE UNFORTUNATE BULLET THROUGH YOUR HEART, HEAD, . . ., ONE UNFORTUNATE KNIFE... STAB INTO YOUR CHEST, HEART, . . . , ONE UNFORTUNATE MASSIVE HEART ATTACK, (YOU NAME IT) - AND WE'RE GONE UNPREPARED!!! CERTAINLY OUR HEAD WILL FOOL US THINKING WE GONNA BE SMARTTER THAN MICHAEL JACKSON, WHITNEY, Singer and Actress, Aaliyah Haughton, SOME OF OUR LOVED ONES, . . . (YOU NAME THEM - OF COURSE WE REALLY HAVE NO PROOF IF THEY HAD T...IME TO GET RIGHT WITH GOD BUT HOPE THEY DID). PLEASE GET RIGHT WITH GOD TODAY WHILE YOU STILL HAVE A CHANCE AND YOU ARE NOT IN A SERIOUS TROUBLE, DEATH, PRISON, DISABLED ON A WHEELCHAIR, ON THE HOSPITAL DEATH BED, GOT CANCER WITH FEW DAYS TO LIVE, . . . . LUKE 13:24 JESUS HIMSELF SAYS "Strive (make every effort "EVERY EFFORT" to enter in at the strait gate: for many, I say unto you, will seek to enter in, and shall not be able." DON'T DELAY THIS THINKING YOU HAVE TIME.
    AND FOR THOSE WHO CALL THEMSELVES "BORN AGAIN", YOU BETTER BE REALL AND LIVE RIGHT - STOP PLAYING YOUR "SECRET SINS" GAMES.

    Yours - PASTOR DONIS NKONE, COLUMBUS OHIO.

    PLEASE WATCH THIS VIDEO OF TEACHINGS ON "SIN"! http://www.youtube.com/watch?v=uFtLgw4Zfvg

    ReplyDelete

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...