Wednesday, June 27, 2012

My Life Is In Your Hands Lyrics - Kirk Franklin


Kirk Franklin
You don't have to worry
And don't you be afraid
Joy comes in the morning
Troubles they don't last always
For there's a friend in Jesus
Who will wipe your tears away
And if your heart is broken
Just lift your hands and say

Oh
I know that I can make it
I know that I can stand
No matter what may come my way
My life is in your hands

With Jesus I can take it
With Him I know I can stand
No matter what may come my way
My life is in your hands

So when your tests and trials
They seem to get you down
And all your friends and loved ones
Are nowhere to be found
Remember there's a friend in Jesus
Who will wipe your tears away
And if you heart is broken
Just lift your hands and say

Oh
I know that I can make it
I know that I can stand
No matter what may come my way
My life is in your hands

With Jesus I can take it
With Him I know I can stand
No matter what may come my way
My life is in your hands


Jifunze Kumiliki Majibu Ya Maombi Yako 2 -Mwl Sanga



Njia ya nne: Kumiliki muujiza kwa kuwatunza watumishi wa Mungu na kuchangia huduma mbalimbali.

Yoshua 12:1-3 kwenye ule mstari wa pili Biblia inasema “Basi wakamwandalia karamu huko naye Martha akamtumikia na Lazaro alikuwa mmoja wapo wa wale walioketi chakulani pamoja nao.

Hii pia ni habari nyingine inamhusu Lazaro ambaye Yesu alikuwa amemfufua baada ya kuwa amekufa kwa siku nne. Sasa Lazaro aliumiliki muujiza wake wa kufufuliwa kwa kumtunza Yesu pamoja na wanafunzi wake kumi na wawili. Hii ina maana Lazaro pamoja  na dada zake waliingia gharama kwa ajili ya kuwatunza Yesu pamoja na  wanafunzi wake, Kwa siku zote ambazo Yesu alikaa kwa Lazaro, Lazaro alihakikisha hawalali njaa, anawapa mahali pa kulala nk.


Sasa unaweza kumiliki muujiza wako kwa kuruhusu watumishi wa Mungu wakae nyumbani kwako. Huenda wamekuja kwenye mkutano au semina kwa wiki moja au mbili itoe nyumba yako itumike, kufanya hivyo ni kumfanya Mungu aendelee kukulinda wewe na yale aliyokupa maana anajua hutamnyima siku moja atakapohitaji kuvitumia. Wapo wengine wanaomiliki kwa kutoa magari yatumike kipindi chote cha mikutano, unaweza pia  kumiliki kwa kuchangia gharama za mikutano  si lazima pesa lakini hata kufanya kazi mbalimbali katika mkutano huo, huenda  ni  usafi,  kubeba vyombo, kufanya usafi walikofika watumishi, kuombea huo mkutano au semina nk. Nakuambia unaweza ukaona kama ni vitu vidogo lakini ndivyo mujibu ya maombi yanavyomilikiwa bila kujali Mungu amekutendea nini.

Nija ya tano: Kumiliki muujiza kwa kufanya  maamuzi ya kuokoka endapo Mungu alikufanyia huo muujiza kabla hujaokoka, na kuwaambia wengine habari ya Yesu aliyekuponya.

Ukisoma ile sura nzima ya 9 ya kitabu cha Yohana utakutana na habari ya kipofu mmoja tangu kuzaliwa kwake  ambaye Yesu alikuwa amemponya. Ule mstari wa 39 unasema “akasema,Naamini, Bwana akamsujudia” Ukisoma vizuri habari hii utagundua baada ya mahojiano marefu kati ya mafarisayo na yule kijana kuhusu uponyaji wake ndipo Yesu akamwuuliza je unamwamini mwana wa Mungu? Yule kijana akamwuliza ni nani huyo nipate kumwamini? Kwa kifupi Yesu akamjibu unayezungumza naye. Ndipo yule kijana  akasema, naamini Bwana akamsujudia.

Mtu mwingine ni Naamani ambaye tumekwisha ona habari zake, kitendo cha yeye kusema toka leo sitatoa sadaka kwa miungu  ya shamu ila kwa Bwana  ni dalili  ya kuonyesha kumwamini Mungu wa Israel. Hivyo hata leo wapo ambao Mungu anawatendea mambo mengi hata kabla hawajaokoka sasa ili kumiliki  hayo ambayo Mungu amekufanyia mwamini Yesu ndio huo muujiza utadumu. Wapo watu leo wanafunguliwa kwenye nguvu za mapepo huo ni  uponyaji. Sasa badala ya kuwasaidia watu wamwamini Yesu tunawaacha, nakuambia pepo watarudi kwa huyo mtu wenye nguvu zaidi kuliko yule wa kwanza.


Pia ukisoma vizuri habari hiyo hiyo utagundua kwamba huyu jamaa alimiliki uponyaji wake kwa kuwaambia wengine habari za Yesu na kukiri kwamba  mponyaji ni Yesu na si mtu mwingine, nakuambia  kufanya  hivyo ni kujihakikishia kudumu kwa huo muujiza na Mungu ataendelea kuutunza huo muujiza  maana wewe ni chombo chake. Mungu akikuponya au kukubariki usinyamaze kimya waambie wengine habari za Yesu aliyekuponya. Jifunze kutoka kwa mwanamke msamaria. Uponyaji wa nafsi yake ulipelekea watu wengi wa mji wa Samaria kuokoka. Soma kile kitabu cha Yohana sura ya nne mistari 30 ya kwanza utaiona habari hii.

Mpenzi msomaji wangu mpaka hapa naamini utakuwa umepata kitu cha kukusaidia labda nikuambie hivi  siri kubwa ya mafanikio ni kuliweka neno la Mungu kwenye matendo, si unajua imani pasipo matendo imekwisha kufa katika nafsi ya huyo mtu mwenye imani hiyo. Nimeamua  kuandika ujumbe  huu baada ya kuona wana wa Mungu wengi imefika mahali  wanakuta yale ambayo Mungu aliwapa kama majibu ya maombi yao yameshaharibiwa na shetani, wapo waliozaa watoto wao wakafa na walimuomba sana Mungu kuhusu hao watoto nk. Sasa  ni imani  yangu kwamba tangu sasa jambo lolote ambalo Mungu atakupa kama jibu la maombi yako utalimiliki.
Ndimi katika huduma

Mwl Patric Sanga

Sunday, June 24, 2012

Kutoka Magazeti ya Kikristo Jumapili hii kwa Ufupi


Gazeti la

Mtawa aibuka na Tiba ya Ukimwi Mlimani
Mamia ya watu kutoka ndani na nje ya nchi kwa sasa wanamiminika katika kilele cha Mlima Pima ulioko wilayani Rolya Mkoani Mara kwa ajili ya kunyweshwa dawa inayotibu magonjwa sugu ikiwemo na ukimwi,dawa hiyo inatolewa na mtawa wa kanisa katoriki ajulikanaye kama Martha Magdalena Nyangwe anayedai kuoteshwa.Mwandishi wa gazeti la Jibu la Maisha alilazimika kupanda mpaka kileleni alipo mtawa huyo ili kujionea ukweli wa mambo.

Mwandishi wa Jibu la Maisha baada ya safari ndefu alifanikiwa kufika kileleni mwa mlima huo unaokadiriwa kuwa ni mita 400 kutoka usawa wa ardhi.Mwandishi alipomuuliza mtawa huyo dawa hiyo ameitoa wapi alijibiwa  ameoteshwa na bikira Maria(mama wa Yesu) ambaye alimwambia atumie visima viwili vilivyochongwa na Mungu Mwenyewe kuwaokoa wanadamu wanaoteseka na magonjwa.Bi Nyangwe ni mtawa wa shirika la Lejo-Maria lenye asili yake nchini Kenya.

Pindi mtu anapokaribia katika eneo hilo huamriwa kuvua viatu kwa kuwa eneo hilo ni takatifu,mgonjwa hutakiwa kupiga magoti chini, Bi nywangwe huchota maji kwenye kisima kwa kutumia kibuyu kilichokatwa na kuyaweka pembeni, kisha huchukua mkia wa N’gombe na kuuchovya kwenye dawa ya kufukuzia mapepo ili kumuandaa mgonjwa kunywa dawa.Wakati huo wasaidizi wa mtawa wakiwa kama kumi wakiimba nyimbo za kumsifu Bikira Maria, kisha Bi Nyangwe humywesha dawa mgonjwa pasipo kufuata vipimo.

Tahadhari:Katika siku hizi za Mwisho Mengi yametokea na yatatokea, ni Vizuri kama kanisa litasimama katika nafasi yake na kuchambua kulingana na maandiko pasipo kupelekwa pelekwa.


Wainjilisti wasomewa dua ya mauti Lindi
Timu ya wainjilisti kutoka Dar es Salaam wamesomewa dua ya mauti mkoani Lindi na wakasimama katika kumtetea YESU na mwisho wa siku Yesu akajitolea utukufu.Timu hiyo  ya wainjilisti na waimbaji ilitoka jijini Dar es Salaam katika kanisa la TAG Ubungo ambao kwa pamoja walipiga kambi wilayani RUHANGWA mkoani Lindi kwa lengo la kuhubiri injili kwa wiki moja.

Kwa mujibu wa mmoja wa wainjilisti hao Mtumishi Francis Mulinda amesema wenyeji wa eneo hilo walionyesha wazi kukerwa na uwepo wao mahali hapo.Watumishi hao walikuwa na desturi ya kuomba kuanzia alfajiri mpaka saa nne asubuhi kisha kwenda kwenye uinjilisti wa nyumba kwa nyumba.Inadaiwa siku ya kwanza wakati wapishi wakiendelea na kazi yao mara alikuja kijana na kushika kitabu cha dini ya mama mdogo kisha kuanza kukisoma, wao hawakujali kisha wakaendelea na kazi zao.

Kesho yake asubuhi baaada ya maombi alikuja mtu akawauliza Je mko salama? tukamjibu ndiyo akasisitiza ni kweli mko wazima tukamjibu ndiyo.Baadaye walikuja watu wengine kama wanne nao wakaanza kusoma kitabu chao kwa muda kisha wakaondoka.Lakini pamoja na hayo yote timu nzima iliondoka Lindi ikiwa salama huku watu wengi wakifunguliwa akiwemo Bi Habiba ambaye alikuwa ameolewa na jini kwa muda mrefu.


Baraza la Maaskofu wa kipentekoste lasema MIHADHARA inamkera Mungu
Baraza la maaskofu wa  kipentekoste nchini PCT,limeitaka serikali ipige marufuku mihadhara yote inayoendelea nchini kwa kuwa imekuwa chanzo cha vurugu zote zinazotokea kwa sasa hapa nchini.Akizungumza na Jibu la Maisha makamu mwenyekiti wa baraza hilo Askofu Daniel Aweti amesema, serikali inapaswa kupiga marufuku mihadhara yote kwa lengo la kupunguza majanga yasiyo ya lazima.


Gazeti la
Nyakati


Mchungaji asema manabii wengi wanaogopa kashfa
Mchungaji David Mpanji wa jijini Mbeya amesema wapo wachungaji wengi wenye karama za Kinabii lakini hawajitamulishi kama manabii kwa kuogopa kashfa zinazotolewa na watu mbalimbali kuwa hakuna nabii wa Mungu katika dunia hii.Mchungaji huyo amezidi kusema wachungaji hao wanaoogopa kasha wanapaswa kutambua kuwa kukashifiwa ni sehemu ya kupakwa mafuta.

Kwa kuanzia amesema yeye mwenyewe amewahi kukutana na kashfa hizo lakini tangu akutane na kashfa hizo amemuona Mungu kupita kiasi.


Askofu Irene Nzwalla mjane anayehudumia wajane
Katika gazeti la Nyakati safu ya Uso kwa Uso na Mtumishi wako jumapili hii yupo Askofu Irene Nzwala wa kanisa la Hosanna Christian Centre Mision lenye makao yake makuu jijini Mwanza.Mama Irene Nzwala ni mwinjiristi na amekuwa akifanya mikutano ya nje kwa muda mrefu sasa.Mama Nzwala amekumbana na vikwazo vingi katika utumishi wake ikiwa ni pamoja na wengine kupinga kitendo cha mwanamke kuwa askofu au mchungaji ila kwa Neema ya Mungu amelishinda hilo.

Mama Nzwala aliwekewa mikono ya kuwa Askofu mkuu wa Hossana Christian Centre na Askofu mkuu wa kanisa la Evangelistic Assemblies of GOD Tanzania(EAGT) Askofu Moses kulola miaka kadhaa iliyopita.Kupitia kanisa la Hossana Christian Centre mama Nzwala mabaye pia ni mjane amekuwa akitoa msaada kwa wajane na watoto yatima.


Thamani ya Wokovu Wangu - Christina Shusho


Sunday Sermon:Get Connected to Your Altar


Pastor Elihud Mwasenga

GOD wants us to join our hearts with the heart of man of GOD so as we can have one heart with the servant of GOD. Luk 11:17 any kingdom which fighting itself is doomed. stop fighting against your spiritual leaders (fathers) but join them. When you say am a member of this church it means your connected to the vision of that church

2Sam 18:3 Before devil fights you he fights first with your pastor because he knows your leader is your peace, and your shield. In church the first thing to protect is our pastor, a hunter or a soldier has to have weapons like arrows, shield, and guns to assist him. Sons and daughters in the church is like arrows and shield to a pastor, are there so stand in the pastor’s battle.


Many people they expect Pastor to fights for their battle and not them to fight for the Pastor’s battle. Once enemy comes, he first fights with the pastor and not with the church members, you have to pray much for your pastor and for the church leaders because you can’t go beyond your pastor .The more they prosper the more you prosper and are the one to declare your Prosperous.


Mikah 5:4 Those who stay under him they do remain undisturbed, the more they grow the more you grow the more they became stagnant is the same point you will be. GOD is the GOD of formula, if he wants to bless his church he first bless our pastor because in spirit we can’t go higher than our pastor, we share the Grace that God has given him.

Leaders/Pastors has a Prophetic word for you
Genesis 49:1
Leaders or your pastor has a prophetic word for your life, One day in our church we had a vibrant preacher, and he decided to insult our pastor, Our  pastor didn’t speak negative to him, now am talking that man is a mentor. Listen, if you living with a man of God anything your doing to him or her can either promote you or demote you. In the Bible Reuben was rewarded according to what he did to his father. “Ni afadhali ukutane na mtu mwenye silaha kali kuliko kukutana na baba yako mwenye kauli zilizo kinyume na wewe”.

Once pastor stands and say you’re going to prosper and he says this is your YEAR OF LOUGHTER others they don’t take it seriously, they think those are the normal words for pastors. I tell you they will come to pass, those mountains in your life let pastors speaks something to them. If an enemy attacks any area in your life, connect yourself with the man of GOD and that challenge will never stay anymore.


How to be Connected
In order to be connected with your pastor you have to Pray for them, Work with them, share your time and your money with them. Others are scarred once am talking about money, they need me to talk about other things when it comes about money then need me to skip that area as if it is not spiritual. Some they have been instructed by God to get connected to their pastor and they refused, here am not talking about tithe. If you want to be connected and become partaker of Blessings, give your prayers, time, Money, efforts, and everything to your pastor


Thursday, June 21, 2012

Stand Up Gospel Comedy ndani ya City Christian Centre jumapili hii


The King of Stand up Gospel Comedy in Tanzania Prezo Chavala akiwa katika moja ya harakati on stage
Baada ya kufanya Tamasha la KUCHEKA TENA la mwisho pale Landmark Hotel,Ubungo mwezi wa tatu na hatimaye Arusha mwanzoni mwa June hatimaye mkali na muasisi wa christian comedy nchini Tanzania anatua tena jijini Dar es salaam kwa Tamasha lake la nne toka ameanza mwishoni mwa mwaka jana pale Ubungo plaza.

Yaani ni kucheka na kucheka na kucheka tena huku ukimsifu Mungu na kujifunza yapasayo kutenda katika maisha yako ya utauwa.Tamasha hili litawasimamisha Up Coming Comedians wa kutosha katika segment maalum ya OPEN MIC, na wale ambao wamezoeleka kama Richard Chidundo,Gerald Mrema,Josephine na wengine watakuwa sambamba na waimbaji kama

Sarah Shila,
Deogratius, Meshack,
Gee & Seth,
WordAlive
Dar es salaam Gospel Bands,
Golden Eagles and
1st Q dance groups

Tamasha Hilo Litaanza Saa 9:00jion-1:30 Usiku
Ukumbi:City Christian Centre(CCC)
Kiingilio 5000/=
Na 2000/= Tu Kwa Watoto.

Katika SERIES hii bado tuko Msimu(SEASON) wa kwanza na hili Tamasha lijalo litakuwa Tamasha la tatu kwa Dar es salaam  na ni Episode II. Kama ilivyotaarifiwa mapema Tamasha hili la jpili ijayo(24th June 2012) pamoja na mawili yafuatayo kwa hapa Dar(Yaani Tar 23th Sept na 23/30th Novemba-mkesha wa mwisho) yatafanyika katikaukumbi wa CITY CHRISTIAN CENTRE-UPANGA(Mkabala na Mzumbe Dsm)

Tamasha Hili Limedhaminiwa na Great Potentials Ltd,City Christian Centre(Ccc),TouchingVision,Author2readers,Wordalive Church,Olympus Computers And Chavala Ideas Platform.

Sehemu ya umati uliohudhuria Night of Transformation usiku ambao uliandaliwa jijini Arusha na Prezo Chavala
Akielezea mafanikio yaliyopatikana Chavala amesema “Kwa kweli mafanikio ni makubwa sana mpaka sasa ingawa mengine hayawezi kuonekana kwa macho ya nyama ila itoshe tu kusema mafanikio ni makubwa mno;yaani toka kule ambako nilikuwa sitambuliki na watu kwa makusudi walikuwa hawataki kuona umuhimu wa Comedy katika ulimwengu wa kikristo mpaka sasa ambako wengi wameanza kuelewa, wamepokea na wamekubali.

kibali nilichokipata Arusha kwa mfano ni kikubwa mno kiasi cha kushangaza; kwa sasa nina vijana wengi sana ambao wamevutwa na kuona nao wanaweza kumtumikia Mungu kwa vipaji vyao kama vile Comedy,Dance na Mashairi na mengine mengi ya vipaji halisi, hivyo nina wanafunzi wakutosha na zaidi washika dau,wachangiaji na wanaounga mkono ni wengi sana na hata wewe unaesoma hapa unakaribishwa kuwa mmoja wao.

Hosana Inc itakuwepo katika onyesho hili na kukujuza LIVE kila kitachojiri 

Mwl Mwakasege kuhudumu katika CITE SUMMER CONFERENCE 2012 nchini Uingereza


Mwl Mwakasege

Mwl Christopher Mwakasege mnamo tarehe 17-19 August 2012 anatarajia kuwa mnenaji katika Summer Conference 2012 itakayoyanyika nchini UINGEREZA  jimbo la MILTON KEYNES,Kongamano hili  limeandaliwa na umoja wa watanzania wakristo waishio katika bala la Ulaya(CITE).

Kwa mujibu wa mmoja wa viongozi wa CITE Mch Emmanuel Chatawe, CITE SUMMER CONFERENCE 2012  itafanyika katika ukumbi wa


 Oakgrove Leisure centre Brickhill Street Middleton Milton Keynes MK10 9JQ
17/08/2012 Time 2:00pm-9pm
18/08/2012 Time 10am-9pm
19/08/2012 Time 11am-7am


Kwa mawasiliano zaidi

Rev. Chatawe 07944632826 ,
Pas. Kimani 07522050673,
Sis Jane 07522302935 au
Sis. Flora 07916160641

Chakula cha mchana kitatolewa Jumamosi na Jumapili kwa wote watakaohitaji kwa Paund 3(£3.00).Wote mnakaribishwa

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...