Saturday, March 31, 2012

The VOICE warekodi Live DvD Album



Usiku wa jana  kuanzia saa tatu usiku katika ukumbi wa Jumba la Makumbusho unaotazamana na chuo cha usimamizi wa Fedha (IFM) jijini Dar es salaam. Kundi maarufu la muziki wa injili liimbalo kwa mtindo wa Akapela lijulikanalo kama THE VOICE, lilikuwa likirekodi LIVE DVD Album. Kwa yeyote Yule aliyefika ukumbini hapo atakubaliana na Hosanna Inc kuwa vijana hawa wanavipaji vya tofauti katika kumtukuza Mungu.

Kundi hili linaloundwa na vijana watano ambao kati yao wanne wanatoka katika familia moja,lilianza kuimba nyimbo ya kwanza iliyopokelewa kwa shangwe ukumbini hapo iitwayo KWENYE MAVUNO, kisha wakaimba nyimbo yao maarufu NAJIVUNIA YESU WANGU ambayo waliimba kwa lafudhi ya Kimasai.Kabla The Voice hawajapanda jukwaani Mc wa shughuli hiyo Minister Godwin Gondwe, aliwakaribisha wageni wote waalikwa kisha shughuli akaanza.Hii ni moja kati ya Live DvD album ambayo ikitoka hutakiwi kuikosa.

The Voice wakiwasalimia mamia ya watu waliojitokeza ukumbini hapo
 Jembe!!!, hawa jamaa wako Vizuri,  ndivyo alivyokuwa akikiri Sam Papaa Katikati ya watu hapo  wakati shughuli ikiendelea.

The Voice wakiendelea kumtukuza Mungu ukumbini hapo

Sehemu ya Umati uliohudhuria tukio hilo

Kulia ni Kijana anaitwa Josiah ambaye ni pekee asiye kuwa ndugu wa damu katika kundi hilo,Huyu Mkaka anaimba sauti ya nne ipasavyo.

Live Recording Ikiendelea

Hapa The Voice wakiimba pamoja na mmoja wa wapiga-solo mahiri nchini Bro Sam Yonanyuma mwenye Gitaa


Kiongozi wa kundi la The VOICE Bro Obedi, akimtambulisha mama yao Mzazi(The First Lady of The Voice), kwa umati uliokuwepo ukumbini hapo



A new World Order - Bishop Jamaal Bryant


Thursday, March 29, 2012

Manny Pacquiao asema Mungu amesema naye kwenye ndoto na Kumwambia aachane na ndondi


Manny Pacquiao akiwa na moja kati ya mikanda ya ubingwa aliyowahi kuitwaa

Kwa baadhi ya watu Jina Manny Pacquiao(33) linaweza kuwa geni masikioni mwao,Mheshimiwa Manny Pacquiao ni raia wa nchi ya Ufilipino na ni mbunge  wa bunge la nchi hiyo.Ulimwenguni kote Manny Pacquiao amekuwa maarufu sio tu kwa sababu ni Mbunge nchini mwake bali ni uwezo wake wa kurusha makonde mazito na ufundi wa hali ya juu wa kukwepa makonde.Manny pacquiao licha ya ubunge amefanikiwa kuchukua mikanda mingi ya mchezo wa ngumi duniani

Jummane iliyopita Manny ambaye ni mkatoriki alihudhuria Bible study  kanisani kwao kwa nia ya kujifunza Biblia .Akiwa katika Bible study aliwaambia wenzake kuwa Mungu amekuwa  akiwatumia yeye,Basketballer Jeremy  Lin pamoja na Tim Tebow  kwa kuwa anawahitaji kwenye ufalme wake.

Katika mahojiano yake siku kadhaa zilizopita na kituo cha redio cha DZMM cha nchini ufilipino,Manny alisema kuwa Mungu alimtokea kwenye ndoto na kumwambia aachane na Mchezo wa ngumi,Pacquiao akaendelea kusema na hapa namnukuu "I will not stay long in boxing because he said(GOD), 'You have done enough. You have made yourself famous but this is harmful," Pacquiao said”.

Manny Pacquiao  kushoto akiwa ulingoni

 

 


Wednesday, March 28, 2012

Ndoa ya Sphumele Mbambo mmoja wa wanakwaya wa Joyous Celebration


Sphumele Mbambo ni mmoja kati ya wanamuziki mahiri wa Joyous Cerebration,na hapa unaweza kujionena siku maalumu katika Maisha yake alipokuwa akifunga ndoa huku akipata sapoti kubwa kutoka kwa wanakwaya wenzake wa Joyous.

Sphumele Mbambo akiwa Jukwaani

Sphumele Mbamboakiwa na Mumewe

Mmoja wa viongozi na muanzilishi wa Joyous Celebration Jabu Hlongwane kushoto, akiwa na maharusi.  

Maharusi wakiingia kweye gari maalumu




Nini Motive ya Kushiriki kwenye Gospel star search ?


Rebeca Malope moja kati ya matunda ya Gospel star seach nchini Afrika ya kusini

Kwa mtu anayesoma Biblia ataona kuwa kiutumishi Eliya hakumtoa Elisha(hakumfanya Elisha akubalike mbele za Mungu) isipokuwa kiu ya Elisha kutaka kumpendeza Mungu ilimfanya Mungu amuwezeshe Elisha kuvaa viatu vya Eliya.Kabla Mungu hajampa huo uwezo Elisha, Mungu  alimuandaa Elisha  kwa muda mrefu akiwa chini ya Eliya.Kwa Level aliyokuwa nayo Elisha, hata kama Eliya angeendelea kuwepo Elisha asingeutupa wokovu na Utumishi bali angedumu katika utumishi.

Ni rahisi kuamini  kuwa Eliya alikuwa ni lift kwa Elisha kiutumishi,lakini ni Lazima tuende mbali na kujua kuwa kabla Mungu hajaridhia jambo hilo alihakikisha kuwa ameshamfunda Elisha kwa viwango vya juu kiasi cha kujiridhisha kuwa Elisha anaweza kuvaa viatu vya Eliya.Ndio maana Elisha alipoichukua nafasi ya Eliya, nafasi hiyo haikumpa taabu,haikumfanya apoteze utukufu wa Mungu bali aliendelea kumtumikia Mungu kwa uaminifu.

Wiki hii tumeshuhudia kamati ya inayoandaa Gospel star seach kwa mwaka 2012 ikithibitisha kuwa mwaka huu kutaendeshwa zoezi hilo.Kurudi kwa Tanzania Gospel  Star seach  baaada ya miaka saba ya ukimya, kunaweza kutafsiriwa kuwa ni kurudi kwa tumaini katikati ya wanamuziki wa injili hususani ambao kiu yao kubwa ni kutoka(Nikimaanisha kufahamika).Kwa wanamuziki wanaochipukia ni lazima wajue suala la kutoka ni lingine na suala la kufanya makusudi ya Mungu ni lingine.

Hivyo kabla underground singer wa gospel hajachukua fomu ya kushiriki Gospel Star Seach ni lazima ajiulize nini Motive ya uamuzi huo,na hili litamsaidia kuweza kubeba gharama za uamuzi huo.Ni vizuri kwa washiriki wenye nia ya kutoka kutambua kuwa GOSPEL STARSEACH haimtoi mtu,bali kiu ya dhati ya mtu kutaka kufanya makusudi ya Mungu ili kuziponya roho za watu ndio humfanya Mungu kushuka na kumuinua mtu huyo(kumtoa).

Baadhi ya Washiriki wa Tanzania gospel Music Awards ya mwaka 2005

Toka enzi za akina Daudi Mungu hu-deal na watu walio curious kutaka kufanya makusudi ya Mungu huku ya kwao wakiyaweka kando kwanza. Watu hawa hawalali,hawapumziki,hawatulii mpaka kusudi la Mungu litimie.Na Mungu anapokuja kumuinua mtu wa aina hii uwe na uhakika kuwa wakumshuha hapo juu hayupo mpaka yeye mwenyewe avulugane tena na Mungu.

Kwa wanaochukua fomu za mashindano hayo kwa ajili ya kutoka, ni bora watambue kweli wanaweza kushika nafasi za juu na kutoka  ila posibility ya kushuka chini ni kubwa na life span yao hapo juu ni ndogo.

Wapo watumishi ambao kweli hizi starseach ziliwatoa kulingana na maagano yao na Mungu, lakini wapo ambao waliwahi kushiriki katika Mashindano hayo na kushika nafasi za juu kwa lugha ya haraka haraka tunawezasema wametoka.Ukichunguza vizuri utagundua kuwa wanawezasema wametoka lakini ukweli unabaki pale pale kuwa wamekuwa maanderground sugu.Kimungu hatuhitaji kutoka, bali tunahitaji GODS FAVOUR  ili kugusa maisha ya watu kwa utukufu wa Mungu. Ndio maana kuna wagonjwa wa ukimwi wamepona kupitia Nguvu ya Mungu iliyomo ndani ya Nyimbo ya Miliam Kakete iitwayo “Natamani Kufanana Na wewe”

Ile kiu ya kutaka kutoka miongoni mwa washiriki waTanzania  Gospel starseach ikiwa kubwa kuliko kiu ya kutaka kumtumikia Mungu,huko mbele hata mshiriki huyo akija kutoka ni lazima atakuja kuharibu mahali.Ni sawa na mchungaji anayetaka kanisa lake lijae watu, huku hatumii muda mwingi kumtafuta Mungu, kumkuta mtumishi huyu akitumia nguvu za giza sio jambo la kushangaza, kwa kuwa Motive yake haikuwa Kingdom bali recognition.

Barani Afrika kuna wanamuziki wengi wa Muziki wa injili ambao wamefahamika sana baada ya kushinda kwenye kwenye hizi starseaches au auditions.Na wanamuziki wengi wakubwa wamekuwa wakitumiwa kama majaji katika mchakato mzima wa kuwapata washindi wa Mashindano hayo.Miongoni mwa wanamuziki wa injili waliopata kujulikana sana baada ya kushinda kwenye starseaches na auditions ni pamoja na

Ucheagu(Uche Double Double)
Rebecca Malope
Nkhululi Bhebhe(Joyous-Tambira Jehova)

Ruth Lyanga kushoto, mdogo wake na muimbaji Lyanga George,Ruth ni mmoja wa walioshiriki katika  gospel star seach ya mwaka 2005 akiwa na umri mdogo sana kipindi hicho.kwa sasa ni mmoja kati ya Viongozi wa Tafes katika chuo cha Mtakatifu Augustino(SAUT)

Kushoto ni dada Aneth Kushaba aliyeshiriki Tanzania gospel starseach mwaka 2005, kwa sasa yuko mjomba Band katikati ni Nuruelly(Tumeagizwa Upendo) ni moja kati ya lulu ambazo kanisa bado linazihitaji


Ucheagu mmoja kati ya matunda ya Gospel star seach nchini Afrika ya kusini


Tuesday, March 27, 2012

Unautumiaje Upako Wa Mungu Juu Yako?



Mathayo 21:28-32 – Ukisoma andiko hili utaona habari  baba mmoja aliyekuwa na wana wawili, akamwita yule wa kwanza akamtuma aende kwenye shamba lake la mzabibu ili akafanye kazi za huko. Huyu kijana alikubali aksema nitaenda lakini hakwenda, babaye akamwendea yule wa pili akmwagiza kama wa kwanza, huyo wa pili akasema sitaki badaye akatabu akaenda.


Yohana 1:12 inasema “Bali wote waliompokea aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale waliaminio jina lake”. Soma vizuri huu mstari tena, Biblia haisemi wote waliompokea walifanyika kuwa wana wa Mungu, kama wengi tulivyozoea kusema au kuomba, bali inasema aliwapa uwezo wa kufanyika wana wa Mungu, hii ina maana suala la kufanyika mwana litategemea wanautumiaje ule uwezo/ au upako ulioko juu yao.
Hebu tujiunze hili somo kwa kuwatumia hawa vijana wa Mathayo 21: 28 32;
Kijana wa kwanza;
  • Alipewa uwezo/upako wa kumsaidia katika shughuri ile aliyokuwa ametumwa na babaye.
  • Lakini yeye hakutambua kwamba ndani yake kuna wezo/upako.
  • Alikubali kwa kinywa kwamba naenda lakini hakwenda kama alivyokiri.
  • Hakuwa tayari kutekeleza agizo la babye licha ya kuwezeshwa .
  • Hii inatufundisha kwamba alikosa unyenyekevu na utiifu kwa babaye.
  • Tunajifunza pia kwamba alishindwa kuutumia uwezo aliopewa na  babaye.
Babaye hakurudi kumuuliza kwa nini hukwenda shambani?. Hii ni kwa sababu kubwa mbili, moja jibu alilolitoa lilionyesha anaujua wajibu ila hataki kuutekeleza (kiburi) i.e alikosa unyenyekevu na pili alishindwa kutumia  uwezo aliopewa babaye, hivyo babaye akaamua ahamishie kwa mwingine.  Na hichi ndio kitu kilichotokea kwa Sauli na Daudi. Mungu alihamisha upako toka kwa Sauli na kumpa Daudi kwa sababu Sauli alishindwa kuutumia vizuri upako wa Mungu uliokuwa juu yake kama Mfalme.

Kijana wa pili.
Kitendo cha kukataa kwake kwenda na kisha kutubu na kwenda kinatufundisha kuwa;
  • Makosa huwa yanafanyika, mtu akitubu Mungu anasemahe.
  • Tunapotubu makosa tuliyofanya, Mungu yuko tayari kusamehe na kututuma tena.
  • Kuna upako wa ziada wa kukusaidia kutekeleza agizo hadi likamilike.
  • Huyu kijana alimpenda babaye na aliujua wajibu wake ndio maana mwishowe alienda.
Kwa nini licha ya kuamua kwamba ataenda shambai alirudi kwa babaye alirudi  kutubu?
  • Asingefanya kazi kwa amani.
  • Kazi isingekuwa na mafanikio mazuri.
  • Hivyo alirudi kuomba upako/uwezo/nguvu tena maana asingeweza bila upako huo.
  • Alihofu baba yake angeweza kumpa upako huo mtu mwingine.
Jifunze yafuatayo toka kwa vijana hawa;
  • Mungu anapokupa uwezo/upako/nguvu za kufanya jambo fulani hakikisha unatumia vizri huo upako.
  • Kama awali umeshindwa kuutumia vizuri, omba rehema, na kisha usirudie tena makosa uliyofanya awali.
  • Upako unahitaji mahusiano yako na Mungu yawe mazuri na ndivyo kazi yako itakavyokuwa rahisi na yenye mafanikio.
  • Ukiweza kuutumia vizuri upako ambao Bwana ameweka juu yako kwa ajili ya kusudi lake tegemeana na nafasi yako hapo ndipo unafanyika mwana wa Mungu yaani unakuwa umefanya mapenzi ya muumba wako.

Kilio cha Mungu ni pale anapoona watu wake aliowapa uwezo kwa ajili ya kazi hapa duniani wanajisahau na kuanza kuifuatisha namna ya dunia hii. Wamesahau kwamba na Shetani naye amewapa uwezo watu wake ili kuhakikisha kwamba makusudi yake yanafanikiwa. Kumbuka kuwa Mungu na Shetani ni falme/kambi mbili tofauti siku zote. Kufanikiwa kwa makusudi ya kila falme kunategemea matumizi ya upako ambao kila mfalme anauachilia kwa watu watu wake.

Natoa wito wa kila mmoja kusimama kwenye nafasi yake, tukikumbuka kwamba muda wa Bwana wetu Yesu Kristo kurudi umekaribia, hivyo tumia upako na nguvu zake vizuri kwa kazi yake. Kama ni Mchungaji, Mwalimu, Mtume, Nabii, Mwimbaji, Mwombaji nk tumika kwa bidii, Je atakapokuja  Bwana wako atakuhesabu kama mtumwa mwaminifu au la?. Biblia inaposema mtumwa mwaminifu inamaanisha mtumwa ambaye anafanya sawasawa na mapenzi ya Bwana wake.

Kanisa tuache kulumbana na kugombana, kumbukeni kwamba ili Shetani aweze kututawala ni lazima atugawanye. Hivyo tusikubali kugawanywa na Shetani, bali kila mmoja aingie shambani kwa ajili ya kazi ya Bwana.  Na ndio maana alisema mavuno ni mengi lakini watenda kazi ni wachache. Hakuwa na maana ya kwamba hakukuwa na watu , watu walikuwepo lakini walishindwa kuutumia upako/nguvu zao vizuri. Kwa hiyo uwepo wao haukuwa na maana kwa Bwana wao. 

Maana/thamani ya uwepo wao ingekuwepo kama wangeutumia uwezo/upako/nguvu walizopewa vizuri ili kuhakikisha makusudi ya Bwana wao yanatimia.
Naamini ujumbe huu mfupi utaamsha nia ndani yako ya kusimama na kujipanga kwa upya kuutumia vizuri uwezo/upako wa Mungu juu yako.

Na Patric Sanga.

Yahweh's Kingdom Treasury Investments, Holdings and Securities


Monday, March 26, 2012

Watumishi wa Mungu wakiwa na Kombe la UEFA



Leo tarehe 26/03/2012 kombe maarufu la mpira wa miguu kwa bara la Ulaya almaarufu kama UEFA Champion Cup limeingia nchini. Pichani ni watumishi wa Mungu Mtume Fernandes na mkewe ambao walikuwa miongoni mwa wageni waalikwa wakipiga picha na kombe hilo.Waziri mkuu Mh Mizengo Pinda alikuwa ndiye mgeni rasmi katika hafla ya kulipokea kombe hilo nchini.

Picha Yetu Jumatatu Hii: Rais Kikwete akifungua Mkutano Mkuu wa Kanisa la TAG

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwahutubia wajumbe wa mkutano mkuu wa kanisa la Tanzania Assemblies of God(TAG) katika ukumbi wa Chimwaga chuo Kikuu cha Dodoma.Rais kikwete alifungua mkutano mkuu wa kanisa hilo uliofanyika mkoani Dodoma Julai 13/17/2010

Kilichojiri Dar es salaam Pentecost Church(DPC) siku ya jana Katika Jumapili ya Kusifu na kuabudu kwa mwezi March


Pastor Safari akiwaongoza Rivers of Life

Tofauti na Umoja wa wakristo wa Madhehebu ya Kiprotestant(CCT),ule wa maaskofu wa kikatoriki, na umoja wa maaskofu wa makanisa ya kipentekoste, Kwa muda mrefu hapa nchini,  ni nadra kukuta umoja wa waimbaji,wainjilisti,wachungaji,mitume na manabii kutoka madhehebu mbalimbali wakikaa pamoja na kufanya jambo katika ufalme wa Mungu pasipo kulivunja  au kutofautiana.

Kanisa la Dar es salaam Pentecost Church(DPC) lililoko Kinondoni jijini Dar es salaam kwa muda mrefu limekuwa na utaratibu wa kuwa na ibada ya kusifu na kuabudu katika kila jumapili ya Mwisho wa Mwezi.Chakujivunia  kama kanisa la Tanzania, ni ile Chemistry inayofanyika mahali hapo(DPC) ambapo watu mbalimbali hufika pamoja pasipo kujali madhehebu kwa nia ya Kumwabudu Mungu kila jumapili ya Mwisho wa Mwezi .

Katika jumapili ya jana ya tarehe 25/03/2012, baada ya maombi ya kufungua ibada hiyo ya kusifu na kuabudu kabla ya wenyeji Rivers of Life Praise and Worship Team kuanza kumwadhimisha JEHOVA, Vikundi mbalimbali vilipata nafasi ya kuhudumu wakiwemo na Tanzania Praise and Worship Team wanaoongozwa na Mtumishi Paul Mwangosi ambaye kwa muda mrefu sasa amekuwa akiongoza Praise Team katika huduma ya MANA inayoongozwa na Mwl C.Mwakasege.

Tanzania Praise and Worship Team walipanda madhabahuni na kuimba nyimbo mbili ikiwemo “Yahwee Wewe ni Mungu wa Ajabu” na baada ya kumaliza zikasikika sauti za warudieeeee!!!!

Tanzania Praise and Worship Team wakiwa Madhabahuni

Baada Tanzania Praise and Worship Team,walipanda jukwaani Vijana wa kundi la THE VOICE wazee wa Acapela.The Voice walianza kuimba wimbo wao uitwao “Kwenye Mavuno” Wimbo huu wa Kwenye Mavuno, kwenye Mavuno, Tutashangilia .... ni wiimbo ya Tenzi ,ila the way walivyo u-fix ki-akapela ni Lazima kwa yeyote anayewasikiliza kukiri kuwa Nyumbani mwa Bwana kuna skills toshelevu.Baada ya wimbo huo ndipo walipoimba wimbo wao maarufu wa “Najivunia Yesu Wangu amenipa uwezo” wimbo ambao wamekuwa wakiuimba kwa takribani miaka kumi na tano na hii ni kwa mujibu wa kiongozi wa kundi hilo.

Baada ya The Voice, Mch Safari alipanda madhabahuni na kufundisha Neno kwa ufupi ambapo alisema kuna watu huenda kwenye matamasha ya kusifu na kuabudu kwa ajili ya kuondoa kama sio kupunguza stress, na wengine huenda kwa ajili ya Mungu kukutana na shida zao,na wapo ambao huenda kwa ajili ya kukutana na jamaa zao.Mch Safari akasema cha msingi tunapaswa  kukutana na Mungu kama Baba yetu na kuwa na deper relashionship with him na sio kuyaweka mbele matatizo.Baada ya Neno kwa ufupi ndipo Rivers of Life wakapanda jukwaani na kuanza na wimbo wa My Redeemer Lives  aliou-lead Pastor Safari mwenyewe.

sehemu ya umati uliokuwepo DPC siku ya jana

 Baada ya Pastor Safari kumaliza kulead My Redeemer Lives, alielekea moja kwa moja kwenye kupiga Keyboard(Korg) ndipo mtumishi wa Mungu Bro BALE alipolead wimbo wa “Yu Hai Jehova”,wakati Bale akilead wimbo huo huku akipiga Keyboard nyingine(Korg), John Lisu alikuwa akipiga lead gitaa.Shangwe zilizidi mara baada ya Bro Bale kuimba wimbo wa “Katikati ya Wafalme hakuna Mungu kama wewe”.Baada ya Bale, alifuata John Lisu na watumishi wengine ambao kwa pamoja walipeleka Sifa na utukufu kwa Mungu.

Wakati  sifa na kuabudu zikiendelea watu wengi walizama kwenye maombi, muda ulipozidi kusogea Pastor Safari alitanabaisha kuwa wale wa mbali wanaweza kuondoka ila tutaendelea kuwepo usoni pa Mungu.Hadi Hosanna Inc inaondoka kanisani hapo majira ya saa moja na robo usiku, watu wengi walikuwa wakibubujika kwenye maombi.Kwa Mwezi ujao ibada hii itafanyika tarehe 28/04/2012.


Sunday, March 25, 2012

Flora Mbasha na Mumewe watembelea Ubalozi wa Marekani na Idhaa ya habari ya Voice of America(VOA)


Flora Mbasha na Mumewe wakihudumu nchini Marekani

Wakati imeonekana kama ni kawaida kwa wanamuziki wa nyimbo za Duniani kwenda na kufanya matamasha katika bara la ulaya na America, hivi karibuni wanamuziki wa injili kutoka Tanzania Flora Mbasha na Mumewe Emmanuel Mbasha wamekuwa nchini Marekani wakimtumikia Mungu kwa njia ya uimbaji.Ziara hiyo iliyoanza takribani wiki moja iliyopita ambapo ijumaa iliyopita kwa pamoja waliweza kutembelea Makao makuu ya kituo cha habari  cha  Voice of America(VOA) yaliyoko Woshington DC.

Pamoja na kutembelea idhaa hiyo, watumishi hao walipata mualiko wa kutembelea ofisi za Ubalozi wa Tanzania nchini Marekani mualiko ambao ulitoka katika kwa Balozi wa Tanzania nchini humo mama Mwanaidi Maajar.

Flora Mbasha na Mumewe wakiwa Makao makuu ya Voice of America (VOA)

Flora Mbasha akiwa na Khadija Riyami mmoja wa watangazaji mashuhuri wa VOA

Flora Mbasha akiwa katika studio za VOA pamoja na Producer Dwayne na sound Engeneer Shedrack

Flora Mbasha akiwa na Balozi wa Tanzania nchini Marekani mama Mwanaidi Maajar

Flora Mbasha na Mumewe Emmanuel Mbasha wakiwa mbele ya ubalozi wa Tanzania nchini Marekani

Hosea akasema Mungu ataturudishia miaka ile iliyoliwa na Ntununtu, Madumadu, Parale...



 Wakati watumishi hao wakifanya ziara ya kumtumikia Mungu nchini Marekani, mwaka jana mwishoni  waimbaji wengine wa injili nchini Upendo  Nkone,Upendo Kilahiro na Christina shuho kwa pamoja walikuwa nchini Marekani wakimtumikia Mungu.


Upendo  Nkone,Upendo Kilahiro na Christina shuho walipokuwa nchini Marekani mwaka jana

Sunday Sermon: The Importance Of Meditation



Pastor Chris Oyakhilome
For a long time, many of God's children equated meditation with just thinking or pondering over the Word. However meditation is much more than thinking deeply on a subject. That is just one aspect of meditation; there's more to it revealed in God's Word.

Meditation is one of the godly exercise that you must practice for a life of dominion and glory. It is a vital activity for every child of God, and its power cannot be overemphasized.

In Joshua 1:8, the Bible says "this book of the law shall not depart out of thy mouth; but that shalt meditate on it therein day and night, that thou mayest observe to do according to all that is written therein: for then thou shalt make thy way prosperous, and then thou shalt have good success.

Three levels of meditation


The word "meditation" in the verse of scripture above is translated from the Hebrew word "hagar" which means to "imagine; mutter". It also means to "roar". This immediately tells us that there are three levels of meditation, each of which is vital.


The first level of meditation is to visualize God's Word as you study it. This means to ponder or think quietly on God's Words in picture. As you keep these pictures in your mind, the Word will be driven into your spirit and will take root there.


The second level of meditation is to mutter God's Word. This means to speak God's Word under your breath, to yourself, over and over again. As you do this, the Word will become personal to you. It will go beyond the written page, beyond the reading of your mind and intellect, into your spirit. It will becomes God's Word to you, and not some distant words written in the Bible.


The third level of meditation is to roar God's Word! At this stage, you shout God's Word out loud. In the book of Isaiah 31:4, the Bible says, "For thus hath the Lord spoken unto me, like as the lion, and the young lion roaring on his prey, when a multitude of shepherds is called forth against him, he will not be afraid of their voice, nor abase himself for the noise of them..."

In this verse of scripture, the Bible beautifully translated the same Hebrew word "hagar" as "roar". The purpose of this kind of meditation is to drown every other thoughts in your consciousness, including thoughts that the devil may try to bring and cause the Word of God in your spirit to rise. When you begin shouting God's Word to yourself like this, some other folks may think something is wrong with you, but continue. The Bible says "...for then thou shalt make thy way prosperous, and then thou shalt have good success".



The power of meditation

Meditation drives the Word into your spirit. It takes the Word from your mind into your spirit. In your mind, you can still reason out the Word of God; but when it gets tour spirit, it becomes real and personal to you. That Word may not have any scientific explanation, but you just know that it is reality, and there is nothing that can take it from you.

Also, it is important to understand that meditation is what gives you rhema. Rhema is the spoken Word of God. It is the "now" Word of God for your situation, and you receive it by meditating on the written Word, which is logos. Logos has the ability to produce results in you and to deliver an inheritance to you, but it will not make you enjoy your inheritance. The Word that changes things is rhema. With rhema, there is no condition in your body that cannot be changed.

Another powerful result of meditation is that it will make you the Word! This is God's purpose for giving you His Word, so we would become the Word.


As you practice meditating consistently on God's Word, you find that you will begin to think, talk, and act like God. Your whole life will become a reflection of the Word.


When this happens, it will be impossible for any sickness to remain in your body, because the Word would have permeated your entire body system and taken charge of your being. Understand that the Word has the divine energy to affect everything about your life including your physical body. Proverbs 4:22 says "For they (the Word) are life unto those that find them, and health to all their flesh".

There may be a situation in your body that you desire a change;find someplace where you can be alone and meditate on God's Word. You may not feel like it; especially when your body is telling you something different, but do it. The Word is sure to prevail over that situation, and causes you to walk in victory always!



Pastor Chris Oyakhilome
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...