Saturday, November 17, 2012

Hafla ya Kuchangia maandalizi ya Usiku wa Kusifu na Kuabudu yafanyika Peacok Hotel


Paul Mwangosi wa pili akiimba sambamba na marehemu Fanuel Sedekia

Tanzania Praise and Worship Team ni kundi la kusifu na kuabudu linaloongozwa na Mtumishi wa Mungu Paul Mwangosi.Dhumuni kubwa la uwepo wa Kundi hili ni kumwabudu MUNGU katika ROHO na KWELI.Mnamo mwaka 2008 mmbeba maono wa Kundi hili mtumishi Mwangosi ambaye kwa muda mrefu sasa amekuwa akihudumu kama kiongozi wa kusifu na kuabudu katika semina za Mwl Christopher Mwakasege alipata maono ya kuanzisha Kundi litakalokuwa likimsifu Mungu kwa namna ya kipekee.

Ilipofika mwaka 2011 Mtumishi Mwangosi aliwaita marafiki na jamaa kisha akawashirikisha maono yake, Maono hayo yalipokelewa vizuri ndipo ikaundwa kamati maalumu ya kuhakikisha maono hayo ya kuwa na BAND na KUWA NA SIKU MAALUMU ambayo nchi nzima itakuwa ikimsifu na kumuabudu Mungu yanatimia nah ii itaanzia jijini Dar es Salaam na kusambaa mikoa yote. Kwa kuanza mwaka jana 2011 ulifanyika Mkesha ule usiku wa kuamkia siku ya kuadhimisha miaka 50 ya Tanzania, mkesha huu ulifanyika katika kanisa la City Christian Centre(CCC) na kuanzia hapo maono hayo yaliendelea

Kwa Mwaka huu wa 2012 tukio hili litafanyika usiku katika kanisa la City Christian Centre(CCC-Upanga) mnamo tarehe 7-11-2012 ambapo waimbaji mbali mbali wa hapa nchini watahudumu kwa lengo moja tu la kumpatia Mungu Ibada.
Kwa kuwa maandalizi ya mkesha huo yanahitaji pesa, kamati nzima inayoratibu mkesha huon iliyo chini ya Mtumishi Emmanuel Kwayu, iliamua kuandaa Chakula Maalumu kilichoambatana na Harambee.Hafla hii nzima ilifanyika usiku wa jana tarehe 16/11/2012 kuanzia saa 2: 00usiku mpaka saa 4: 00 usiku katika hotel ya Peacok jijini Dar es salaam ambapo watu walijumuika pamoja wakiongozwa na Band ya Tanzania Praise and Worship team.

Hapa chini ni sehemu ya matukio ya hafla hiyo na jipange kuhudhuria siku hiyo
 7-11-2012 kwani ni siku ya kihistoria.

Ukumbi ukiwa tayari kwa Hafla

Shangwe

No Coment

Audience ikienda sawana Praise Team

Simon Jengo Mratibu wa Kamati akieleza jambo katika hafla hiyo

Tanzania Praise and Worship Team Ikihudumu

Tumbo ni Kwa Chakula, na  Chakula ni kwa Tumbo, that is Biblical

Bloggers

Angalia Praise Team Ikihudumu Siku ya Jana

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...