Monday, April 4, 2011

Uzinduzi wa Album ya Kwaya ya Uinjilisti Lumala(EAGT)

Jumapili iliopita kwaya ya Uinjilisti Lumala(EAGT) toka jijini mwanza ilifanikiwa kuzindua album yao ya tano iitwayo "Mwacheni Mungu aitwe Mungu". Mkuu wa polisi jijini Mwanza Mh Simon Siro ndiye aliyekua mgeni rasmi huku vikundi mbalimbali vya uimbaji vikisindikiza uzinduzi huo wa aina yake. Tofauti na kwaya nyingi ambazo hufanya uzinduzi katika kumbi kubwa, Kwaya ya uinjilisti Lumala chini ya Mchungaji kiongozi wa kanisa hilo Mch Daniel Kulola wao walizindulia album yao katika viunga vya kanisa hilo pasipo kiingilio na umati mkubwa wa watu ulihudhuria kutoka pande mbalimbali za jiji la Mwanza.

Mch Daniel kulola pamoja na Mr Mutashi na mkewe wakifuatilia uzinduzi huo

Jerusalem Band jukwaan
Kwaya ya uinjilisti ikiwajibika jukwaani

Kazi ilikua pevu kwa muda wote


Mch Daniel kulola akiteta jambo na Mtumish Richard ambaye ni Regional Manager wa Benki ya NIC kuhakikisha mambo yanakwenda sawa

Sehemu ya umati uliojitokeza uwanjani hapo

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...