Tuesday, May 29, 2012

Kanisa Lingine Lachomwa Zainzibar


Rais wa Zanzibar Dr Ali Mohamed  Shein
BAADA ya Kanisa la Assemblies of God kuchomwa moto katika vurugu zilizoanza mwishoni mwa wiki iliyopita, jana Kanisa Katoliki Parokia ya Mpendae nalo limechomwa moto.

Akizungumzia hali hiyo jana, kiongozi wa Kanisa hilo, Ambaros Mkenda, alidai kwamba Kanisa hilo lilichomwa moto na watu wasiojulikana na kusababisha uharibifu mkubwa.

Alidai Kanisa hilo lilichomwa moto jana saa 8.30 mchana na watu wanaohisiwa kuwa wafuasi wa Jumuiya ya Kiislamu ya Uamsho, waliokuwa wakitoka katika Mahakama ya Mwanakwerekwe kusikiliza kesi ya wenzao waliokamatwa juzi.

Mkenda alidai kuwa watu hao waliwazidi nguvu walinzi wawili wa Kanisa hilo na kuvunja lango kuu la kuingilia ndani ya Kanisa na kuchoma moto na waliharibu madirisha na vifaa kadhaa vyenye thamani ya Sh milioni 20.

“Tunasikitika sana na uharibifu mkubwa uliofanywa katika Kanisa letu ambalo lilikuwa tegemeo kubwa kwa wafuasi wapatao 2,000 wa eneo la Parokia ya Mpendae na jirani,” alisema Mkenda.

Mkenda alidai kuanzia juzi, viongozi wa makanisa mbalimbali waliwasilisha maombi yao Polisi kuhusu kupewa ulinzi katika nyumba za ibada, baada ya kupokea vitisho. Hata hivyo, Mkenda alidai ombi lao hilo halikutekelezwa na Polisi na uharibifu mkubwa ukatokea katika Kanisa la Assemblies of God la Kariakoo.

Wafuasi na waumini wa Kanisa hilo walikusanyika nje ya jengo hilo, huku vijana wakishikwa na hasira wakitaka kwenda kulipiza kisasi katika maeneo ya jirani wakidai wanawatambua vijana waliofanya vitendo hivyo.

Mmoja wa waumini wa Kanisa hilo ambaye ni mwandishi wa habari wa Shirika la Utangazaji Zanzibar (ZBC), Susan Kunambi alilazimika kuwatuliza wafuasi vijana wa Kanisa hilo waliopandwa na jazba wakitaka kulipa kisasi.

“Hakuna sababu ya kupandisha jazba na kutaka kufanya vitendo ambavyo vitasababisha hasara na uharibifu ... Kanisa siku zote linahimiza amani na upendo na si chuki,” alisema Kunambi

Polisi walifika haraka katika eneo la tukio na kurusha mabomu ya machozi ili kutawanya makundi ya vijana waliojikusanya na wengine kurusha mawe.

Kamishna wa Polisi Zanzibar, Mussa Ali Mussa alithibitisha kuchomwa moto Kanisa hilo na kusema ulinzi umeimarishwa katika baadhi ya maeneo ya nyumba za ibada yakiwamo makanisa. Baadhi ya mitaa ya Jang’ombe na Mwanakwerekwe njia zimewekwa mawe na vikundi vya vijana waliochoma mipira ya gari na kusababisha moshi mkubwa.



Chanzo: Habari Leo

Monday, May 28, 2012

Lowasa aichangia Upendo Radio Shillingi Milion 10



Rais mstaafu wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania na mbunge wa Moduli Mh Edward Lowasa, jana alikuwa mgeni rasmi katika tamasha maalumu la kuchangia usikivu mzuri wa Radio ya Upendo Fm 107.7 inayomilikiwa na Kanisa la kiinjili la Kilutheri Tanzania(KKKT).Tamasha hilo lililofanyika katika ukumbi wa Diamond Jubelee liliambatana na harambee ya kuchangia kituo hicho cha redio Mhe Lowasa yeye pamoja na marafiki zake walichangia jumla ya shilingi Millioni kumi.Lengo la kamati iliyoandaa tamasha hilo ilikuwa ni kukusanya jumla ya shillingi Million 220..

Katika Tamasha hilo liliwahusisha nyota wa muziki wa injili kutoka ndani na nje ya nchi wakiwemo Sara k kutoka Kenya,Jenifer Mngendi,Kijitonyama Upendo group na vikundi vingine vingi.

Mh Lowasa akiwa na mwanamuziki kutoka Kenya Sarak K katika tamasha la Upendo Radio siku ya jana

Mchungaji George Fute ambaye ni Msaidizi wa Askofu Mkuu wa Kanisa la KKKT,Askofu Alex Malasusa akitoa shukrani kwa Mgeni wa Heshima katika hafla hiyo ambaye ni Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh.Lowasa

Jenipher Mngendi akihudumu siku hiyo

Joshua Kiongozi wa kundi la Kijitonyama Upendo Group akimsifu Mungu ukumbini hapo

MKIRSTO NA UCHUMI - Mwl Mgisa Mtebe


Utangulizi

Mkristo ni nani?
Mkristo ni mtu aliyemwamini Yesu Kristo na kumpokea au kumfanya Bwana na Mwokozi wa maisha yake (Warumi 10:9-10). Haitoshi tu kusema, ‘Mkristo ni mtu aliyemwamini Yesu’, kwasababu Biblia inasema ‘hata shetani naye anaamini na kutetemeka pia’ lakini si mkristo (Yakobo 2:19)
Uchumi ni nini?

Uchumi ni Maarifa ya namna ya kutumia rasilimali (resources) zilizopo au chache (scarce) ili kukutana na mahitaji na matakwa mengi (needs and wants) katika maisha ya mtu/watu.
Ni mapenzi ya Mungu tuyafurahie maisha yetu aliyotupa yeyé hapa duniani kama anavyosema katika kiyabu cha Isaya 1:19 ‘mkikubali na kutii, mtakula mema ya nchi.’ Na kila kitu unachohitaji kwa ajili ya maisha mazuri ya utoshelevu, kipo hapa hapa ulipo.

Mwl. Mgisa Mtebe
Rasilimali zote tunazozihitaji kwa ajili ya Maisha mazuri ya Baraka, tunazo hapa hapa. Lakini wewe kama Mkristo, hautaweza kuyafurahia maisha aliyokuandikia Mungu, uyaishi hapa duniani, kama hutajua namna/jinsi/mbinu/kanuni za ki-Mungu za kufanikiwa kimaisha ili kukutana na mahitaji yako na matakwa yako ya kimaisha.

Tujifunza siri na kanuni za kufanikiwa kiuchumi kwa maisha ya tajiri mmoja, aliyeandikwa katika Biblia, na jinsi alivyofanikiwa sana kimaisha na kiuchumi, japo alianza maisha kwa shida na taabu. Mtu huyu tajiri anaitwa Yakobo. Habari hii utaipata katika kitabu cha Mwanzo 28:1-5; 29: 13-30; 30:25-43; 31:1-3; 32:1-18

Kwa ufupi ni kwamba:
Yakobo alipomkimbia ndugu yake Esau, alifika kwa mjomba Labani akiwa na fimbo tu, lakini baada ya kukaa huko kwa muda, alirudi katika nchi ya Baba zake akiwa tajiri mkubwa mwenye wafanyakazi 1,200 (Matuo mawili = Makundi mawili ya watu 600)  Soma Mwanzo 32:9-12. Fikiri mwenyewe,  mtu mwenye wafanyakazi 1,200 alikuwa ana wanyama wangapi? Thamanisha mali zake kwa fedha ya sasa.

Utakapokwenda kuisoma habari hii, utaona jinsi Yakobo alivyokuwa tajiri, kwa maana alikuwa na uwezo wa kutoa zawadi kwa mtu, kiasi cha punda 200, farasi 200, ngamia 200, ng’ombe 200, kondoo 200 na mbuzi 200. Utajiri huu kwa lugha ya sasa; Punda 200 (kiuchumi, hii inakadiriwa kuwa ni sawa na magari madogo ya mizigo (pickup) 16; yaani punda 12 wanaweza kubeba mzigo wa pickup 1). Kondoo 200 ni sawa na maduka 4 ya nguo, ngamia 200 ni sawa na malori madogo ya mizigo 16, farasi 200 ni sawa na pikipiki 50.

Unaweza kuona jinsi Yakobo wa Isaka alivyokuwa tajiri. Mtu anayeweza kukupa zawadi ya pikipiki 50, maduka 4 ya nguo, malori madogo 16 na magari madogo ya mizigo (pickup) 16; yeyé anabakiwa na kiasi gani cha utajiri? Na kama alianza akiwa mikono mitupu, alitumia njia gani kufikia katika mafanikio hayo ya kiuchumi? Hata mimi nataka kujua. Utashangaa kwamba, Biblia inafundisha uchumi kiasi hiki.

KANUNI ZA KIBIBLIA ZA UCHUMI MZURI

Maono - Kuona Fursa za kiuchumi
Mafanikio hayaji kwa bahati mbaya au nzuri, bali yanapangwa. Ukiona mtu amefanikiwa kiuchumi, ujue aliona kwanza fursa hiyo na akaichuchumilia na kuifuatilia mpaka akafanikiwa. Hivyo muombe Mungu akupe kuziona fursa zilizopo. Tafuta kuona mahitaji mbalimbali ya jamii, huwezi kukosa kuona fursa kadhaa za kiuchumi.

Utakapokwenda kusoma habari hizi, utagundua kwamba, mjomba Labani alikuwa tajiri mwenye shughuli mbalimbali na wafanyakazi wengi sana. Kwa muda mfupi ambao Yakobo alikaa kwa mjomba wake, aligundua kwamba, ataweza kufanikiwa kwa kujishughulisha na kazi mojawapo za mjomba, hivyo akachagua kujikita katika mifugo ya mjomba Labani. Mwanzo 29: 15-20.

Mafanikio hayaji kwa bahati mbaya au nzuri, bali yanapangwa. Lazima uwe na uwezo wa kuona fursa za kiuchumi na kujitosa humo baada ya kufanya upembuzi yakinifu. Ukiona mtu amefanikiwa kiuchumi, ujue aliona kwanza fursa hiyo na akaichuchumilia na kuifuatilia mpaka akafanikiwa. Soma Mwanzo 21:14-19 na Waefeso 1:15-19 utaona umuhimu wa kuwa na macho yanayoweza kuona vitu vilivyojificha. Hivyo muombe Mungu akupe kuziona fursa zilizopo. Tafuta kuona mahitaji mbalimbali ya jamii, huwezi kukosa kuona fursa kadhaa za kiuchumi.

Malengo mahususi – Kujua kwa hakika unataka kufika wapi
Alijua alichokuwa anataka na alikaza uso kutoyumbishwa mapaka apate anachotaka. Hii ni tabia ya kila mjasiliamali aliyefanikiwa. Lazima uwe ‘focused’ usiyumbishwe. Utaiona tabia hii ya Yakobo kwa jinsi alivyojaribiwa katika swala la kupata mke aliyemtaka. Alijua anataka mke, na sio bora mke.

Mjomba Labani alikuwa na mabinti wawili, Lea na Raheli. Aliambiwa kama anataka kumuoa Raheli, atoe mahari ya kufanya kazi kwa miaka 7. Baada ya maiaka 7 akapewa Lea badala ya Raheli. Kwa lugha rahisi, alitapeliwa au alizulumiwa. Akaambiwa, kama vado anamtaka Raheli, afanye kazi tena kwa miaka 7 ndipo atapewa Raheli.

Kama Yakobo angekuwa anataka bora mke, angeridhika na Lea, lakini kwakuwa alikuwa anamtaka Rachel, akalenga ‘kutokupumzika’ mpaka ampate Raheli, bila kuyumbishwa. Akaapinda mgongo tena kwa miaka 7 ili tu kuyafikia malengo yake, na akampata mke aliyemtaaka, Raheli !!!    Mwa 29:16-18.

Ni muhimu sana kwa mtu kuwa na makusudio ya moyo (Malengo).
Malengo hufungulia nguvu za Mungu (Msaada wa Mungu)
‘Nawe utakusudia neno, nalo litathibitika kwako; na mwanga utaziangazia njia zako’ (Ayubu 22:28)
Malengo hukupa nidhamu ya kimaisha (Descipline)
‘Pasipo maono, watu huacha kujizuia (yaani hukosa nidhamu, au msimamo - huyumba-yumba)   (Mith 29:18).

Yeremia 1:5-10; Mungu alimtenga Yeremia kuwa Nabii tangu tumboni mwa mamaye, Je wewe ulitengwa uwe nani? Tafuta kujua mpango wa Mungu kwako. Usipopatia wito wako, kuna hatari ya kutofanikiwa katika baadhi ya vitu unavyohangaika kuvifaya. Mungu anabariki kazi zake, si kila kazi. Ni muhimu uutafuta uso wa Mungu ili ujue mpango wa Mungu juu ya maisha yako.  Yeremia 29:11-13,  Zaburi 32:8


Mipango Mizuri – Kuwa na njia za kukufikisha katika malengo yako
Mwanzo 30:25-36; Ili kufikia mafanikio na maisha mazuri, mtu wa Mungu si tu kwamba anahitaji kuwa na maono na malengo tu, bali pia anahitaji kuwa na mipango mizuri ya kumfikisha katika maono na malengo yake. Jiulize, ni kwa njia gani nitaweza kufikia kule ninakotamani kufika? Hizo njia utakazopata, ndio tunaita mipango.

Katika habari hii ya Yakobo, unaona anapanga kuwachukua wanyama wa mjomba na kwenda nao umbali wa siku tatu (3) na kukita kambi ya mifugo huko. Na utaona anapanga kukaa huko kwa miaka mitatu (3). Hizi namba unazoziona hapa, ni mipango madhubuti. N mawazo ya mtu aliyefanya uchunguzi wa eneo zuri la kuweka kambi ya mifugo na ni mawazo ya mtu aliyepiga mahesabu kuona, ni baada ya muda gani atakuwa ameweza kutengeneza faida.

Mipango mizuri itazaa matokeo mazuri. Mipango mibaya itazaa matokeo mabaya. Kwahiyo, tafuta namna ya kutengeneza mipango mizuri, ikibidi tumia wataalam wa mipango. Fanya Fisibility study  na tengeneza a good Business Plan. Yakobo alijitenga mwendo wa siku 3 na akakaa nyikani muda wa miaka mitatu. Huu ni Mpango wa Shughuli (This is a  business plan au activity plan). Baada ya miaka kadhaa, Yakobo alikuwa mtu mwenye mafanikio na utajiri mkubwa, leo tungemuita ‘Milionea’ mkubwa. Kumbuka; Mipango mizuri itazaa matokeo mazuri. Mipango mibaya itazaa matokeo mabaya.

Itaendelea toleo líjalo

Mwl. Mgisa Mtebe,
P. O. Box 837, Dar es Salaam.
Simu: (+255) 0713497654.
Barua pepe (Email): mgisamtebe@yahoo.com:
Tovuti (Website): www.mgisamtebe.org

Picha yetu Jumatatu Hii:Mr and Mrs Rwakatare


Pichani anaonekana Mchungaji Dr Getrude Rwakatare kulia akiwa na mumewe wakati wa harusi ya mtoto wao wa mwisho Bw Mutta Rwakatare alipokuwa akifunga ndoa siku ya juzi jumamosi tarehe 26.05.2012.Ndoa ilifungwa katika kanisa la Mikocheni na Harusi ilifanyika katika ukumbi wa Mlimani City.

Maharusi Mr and Mrs Mutta Rwakatare


Picha kwa hisani ya Uncle Jimmy

Sunday, May 27, 2012

Kanisa la TAG na Gari la Mchungaji Vyachomwa moto Zanzibar



Usiku wa kuamkia leo mjini Unguja mtaa wa Kariakoo kumefanyika tukio la kusikitisha ambapo watu wasiojulikana wamelichoma moto Kanisa la TAG lililopo mtaani hapo pamoja na gari la mchungaji wa kanisa hilo Mchungaji Dickson Maganga.Jambo hili limetokea siku ya leo tarehe 27.05.2012 ambayo ni siku maalumu ya maombi kwa dunia nzima huku dhima ya mwaka huu ni kuombea ukristo katika nchi za Kiislamu.

Kanisa la Tanzania Assemblies of God (TAG) liliopo mtaa wa Kariakoo mjini Unguja limechomwa moto jana usiku wa kuamkia leo na watu wasiojulikana

Gari la Kiongozi wa Kanisa la Tanzania Assemblies of God (TAG) Bishop Dickoson Maganga lililochomwa moto na watu wasiojulikana usiku wa jana katika eneo la Kariakoo nje ya kanisa hilo ambapo uharibifu wote unaelezwa kuwa umegharimu shilingi millioni 120. Picha/ZanzibarYetu




Saturday, May 26, 2012

Mitazamo ya watu mbalimbali baada ya Gazeti la AN NUUR Kuandika “HATUNA IMANI NA BARAZA LA MITIHANI”



Gazeti la AN NUUR Saut ya Waislamu ni gazeti la Kiislamu na toleo yake la Jana 25.05.2012 lina kichwa cha habari kisemacho “HATUNA IMANI NA BARAZA LA MITIHANI” Yameelezwa mengi humo ndani kama hints za picha hapo juu inavyoonyesha lakini ili kubalance story ime-ibidi Hosanna Inc kuwa katikati na kupost maoni ya watu kuhusu hicho kilichoandikwa katika gazeti hilo.

Baada ya kutoka gazeti hilo jana ijumaa, blogger na mwanahabari mkongwe nchini Dr Majid Mjengwa anayemiliki blog ya www.Mjengwa.blogspot.com aliiweka habari hii kwenye blog yake.Mjengwa ambaye pia ni muislamu  alijaribu kuweka wazi mtazamo wake kwa kusema waislamu “tumezidi kulalamika sana” na akaeleza mengi.Baada ya Mjengwa kutoa  mtazamo wake, watu wengi kutoka dini zote waislamu kwa wakristo wametoa mawazo yao juu ya hilo na hapa ninayaweka kama yalivyo.

Mchangiaji wa Kwanza
Allah'u Akbar!haya ndugu Waislamu wa Alnuur mnalo? Yaani pengine ukiongea wewe muislamu msomi wa PhD tena wa chini ya baraza hilohilo wanalolalamikia Waislam wenzio wanawezakukuelewa, ingawa jiandae pia kuitwa Qafir. Pole, ila ukweli watausoma tu hata kimyakimya. Nimesoma chuo chenye mfumo wa kiislamu, nilichokishuhudia huko ni majungu kila baada swala ya Ijumaa kitu ambacho hutakaa ukikute makanisani (msikiti ulikuwa chuoni).,na hao ni wasomi unaodhani labda kwa elimu waliofikia majungu misikitini kuwasengenya wasioamini dini yao wangeachiwa mashehe ubwabwa wa mitaani, ila wapi!!

Siri ya shule za wakristo ni Mungu, Nidhamu na Bidii na Kazi full stop! Majungu ni mwiko, NECTA mnawasingizia tu, hata awekwe imam apaongoze mtalalamika tu. Kukata mzizi wa fitina nashauri ndugu waislam wapeleke kwa wingi watoto wao shule za kikristo waone matokeo.

Na tatizo jingine naona ni la kihistoria, hivyo malalamiko hayawasaidii, leo kila kanisa kwa mfano Katoliki lina shule za awali na japo msingi, na karibu yote yalikuwa na shule za msingi zikataifishwa na serikali( hili ni sawa kabisa), ukizingatia serikali hy ilikuwa chini ya mkristo mwenzao, ila lengo ni elimu kwa wote, hadi vyuo makanisani (vingi vya ufundi mbalimbali), acha mahospitali. Yaani tutaona kanisa limewekeza toka zamani ktk elimu na maendeleo, waislam majungu na kulalamika hata misikiti ni nadra kukuta uliomalizika kujengwa(tafiti)kama ni wa ghorofa unaishia katikati kwa chini juu nusunusu kisa kugombea pesa za ujenzi toka Uarabuni.

Wapatikane waislam 10 kama wewe wakaelimisha wenzao wakaamka tukapumzika na kelele za miaka nenda rudi bila kujibidiisha kufika walipo wenzao

Mchangiaji Mwingine
Watoto wa mama wa kambo kulalamika jadi yao

Mchangiaji Mwingine
kaka umeongea point kali sana, kama waisilamu wamesoma basi nadhani wamesikia, ujinga wa kulalamika kila siku hadi sasa rais muisilamu makamu yakhe sasa mnataka nini jamaniiiiii??? au mnataka maisha kama ya ndugu zenu waaarabu ya kuuana kila siku wakati wote waarabu na ni waisilamu?

Mchangiaji Mwingine
Huna uisilamu wowote na ungekuwa muisilamu usingeandika maneno hayo.Kwani hujui kama waisilamu wanachakachuliwa mitihani tokea enzi hizoooooooooo.Unajifanya muisilamu ili kumdhalilisha muisilamu????Inna lillahi wainna ilaihi raajiun kwani kafa mtu hapa???Huyo mhariri anajua anachokiandika kwahiyo kama unaweza nawewe kafanye kazi ya uhariri.

Mchangiaji Mwingine
Bora mwislamu ndiye katoa mada hii make angekuwa mkristu,hapa kungewaka moto.waambie ndugu labda wataelewa.

Mchangiaji Mwingine
Acha unafiki mada yako jinsi ulivyoiandika ni dhahili lengo lako kuponda waislam na uislam wenyewe, unajiita eti mwislam, may be mwislamu wa birth certificate.ajabu hata hujui nani alieanzisha historia ya kutumia namba kwenye mitihani.finally ww si mwislamu umeamua kujifanya mwislamu mnafiki tu wewe.

Mchangiaji Mwingine
Mi ni muislam kamili.NImekuwa nikijiuliza kwa nini shule kama alharamain,kinondoni Muslim au shule yoyote ya kiislam haipo kwenye 10 bora za kitaifa?hivi mnafahamu ubungo Islamic primary inaishia drs la ngapi? Hivi mshajiuliza sie waislam tuna hospital kubwa ngapi za maana Kama KCMC au bugando maana hata Zanzibar hakuna na kule dini yetu in asilimia 95?mshajiuliza mbona viongozi wetu waislam walioko serikalini au hata wasomi wenzetu wakiislam Kama maprofesa hawawapeleki watoto wao kwenye shule zetu za kiislam? Hata aw Kikwete alimpeleka kifungilo/mazinde hata Kawawa?NAOMBA WAISLAM WENZANGU TUTAFAKARI HAYO MASWALI HAPO JUU NDIPO TULALAMIKE

Majid Mjengwa

Mchangiaji Mwingine
SASA NYIE RAIS MWISLAM, MAKAMU MWISLAMU,WAZIRI WA ELIMU MWISLAM, KATIBU MKUU ELIMU MWISLAMU,NAIBU WAZIRI TAMISEMI ANAESHUGHULIKIA ELIMU MWISLAM.......BADO TU MNAONEWA KWENYE MITIHANI??SASA MTAJIKWAMUA VIPI KAMA HATA HAO MLIOWWAWEKA KOTE HUKO HAWAWASAIDII?????

HIVI USHAJIULIZA KWANINI HATA WAISLAMU HAWAPELEKI WATOTO WAO KWENYE CHUO CHENU CHA KIISLAMU CHA MOROGORO?PAMOJA NA KUPEWA MAJENGO LAKINI HAKUNA KITU MNAFANYA PALE ZAIDI YA MAJUNGU.NDUGU ZANGU ELIMU HAINA UJANJA NI KAMA MPIRA WA MIGUU HUKUSOMA NA KUANDALIWA VEMA USITEGEMEE KUFAULU.HIVI ZILE SHULE ZENU ZA KIISLAMU DAR KWANINI WANASOMA WATOTO WA WAISLAM WALIOHOI,WALE WENYE UWEZO WOTE WATOTO WAO WAKO ST.MARIAM,ST.FRANCIS,MAZINDEJUU,KIFUNGILO NK?AU 

KWANINI SHULE YA FEZA INAFAULISHA VIZURI PAMOJA NA KUWA NI YA WAISLAMU (WAISLAMU WA ULAYA WALIOSTUKA LAKINI SIO WA USHENZINI MIDDLE EAST)?MKIANZISHA SHULE AU CHUO MNAANZA NA UBAGUZI WA DINI WENZENU WAKIANZISHA SHULE ANASOMA YEYOTE BILA KUWEKEWA ULAZIMA WA DINI ILA MAADILI.MTALALAMIKA SANA FANYENI TAFITI MTAJUA KINACHOWAMALIZA,MTAISHIA NAFASI ZA KISIASA WAKATI WENZENU WAMEJAZANA KWENYE NAFASI ZA UTENDAJI NA KULE NDIO MAISHA YANAELEWEKA KWA MUDA MREFU DUNIANI KULIKO KWENYE SIASA AMBAKO NI WACHACHE NA KWAMUDA MFUPI.

SOMENI WAUGWANA WAARABU WAMEKAA ZANZIBAR PALE MIAKA NA MIAKA HAKUNA SHULE INAYOELEWEKA ZAIDI YA VIJIWE MAARUFU VYA KAHAWA NA MAJENGO CHAKAVU.HALAFU HUKU KUANZA KULILIA ELIMU ZA MAKAFILI MUDA SI MREFU MTALILIA NA KITIMOTO NYIE....SIMJIFUNZE ELIMU YENU ILE YA RIVASI?

Mchangiaji Mwingine
Mtoa mada aweza kuwa muislamu jina lakini sio muumini, kwani hata kwenye Quran imeandikwa kuna waislamu na waumini.

Mimi nakuomba badala ya kuanzisha zogo na kashfa kwanini usitumie hiyo elimu yako kuwasaidia kuappeal ili hiyo mitihani yao isahihishwe upya na indipendent board? Maana haiyumkiniki ikawa wakristo tu ndio wana akili na uwezo wa kufaulu na wengine hawana.

Hao bwana kiboko yao wakienda shule nje ya nchi majority wanavyotokota, kuandika kitu kikaeleweka hawawezi, wanaishia kutulipa pesa tuwaandikie kazi zao. Tulizeni ball tutamwaga siri zenu bure humu na tudegree twenu feki twa kubebwa kuanzia papers mpaka dissertation. Ndio maana nchi iko stagnant haiendelei na kujidai na usomi wenu, miaka nenda miaka rudi hamna cha maana mnachofanya wala mlichovumbua.

Na asimame hapa mmoja wenu aseme kagundua japo dawa ya kuzuia watoto kuharisha seuze ya kutibu malaria!! Give us a break acheni matusi na kashfa wakati na nyie vichwani hamna kitu!!

Mchangiaji Mwingine
Asante mtoa mada mimi nilibadirisha dini nikaingia Uislam lakini jamani kilasiku kulalamika kama watoto wadogo hawana hoja na ndio maana mimi sisomagi hili gazeti hata wanangu nimewambia wasiyafate hayo mambo yasiyokuwa ya msingi kazi kulalamika tu bila sababu asante mwislamu mwenzangu

Hosanna Inc inaamini tunaweza tofautiana dini, mitazamo juu ya mambo mengi yanayoendelea katika nchi yetu tulivu.Cha msingi ni kudumisha AMANI YETU na kuheshimu misimamo ya makundi na dini mbalimbali tulizonazo hapa nchini.

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...