Sunday, July 31, 2011

Fanuel Sedekia - Nishike Mkono



Sunday Sermon: DEALING WITH DELAY



In April 2010, clouds of ash spewed by a volcano in Iceland closed airports across the UK and Europe for 5 days. Nearly 100,000 flights were canceled and millions of passengers around the world found themselves in an enormous holding pattern on the ground. People missed important events, businesses lost money, and no one knew when it would end.

When our plans fall apart and there is no remedy, how do we deal with frustration and delay? Isaiah 26:3-4 is an anchor for our souls in every storm of life: “You will keep him in perfect peace, whose mind is stayed on You, because he trusts in You. Trust in the Lord forever, for in [Jehovah], the Lord, is everlasting strength.” Whether we’re facing annoying inconvenience or heartbreaking loss, this rock-solid promise is worth memorizing and repeating every night when we close our eyes to sleep.

Today, when plans are shattered, do our minds dwell on the circumstances or on the Lord? During frustrating delay, can we still trust the loving heart of God? In the hymn “Like a River Glorious,” Frances Havergal so beautifully expressed what we long for.

Calvary Temple

Friday, July 29, 2011

My God is good Lyrics


Ucheagu akiimba Double Double akishirikiana na kundi la Joyous Celebration
Writer Joyous Celebration (Uchechukwu Agu)
Year 2009

Hey, my God is good o! (Hey, my God is good o!) (2x)

 Everything na double double o (na double double o)
 Everything na double double o (na double double o)
 Promotion na double double o (na double double o)
 Your money na double double o (na double double o)
 Your house o, double double o (na double double o)
 Your cars, double double o (na double double o)

Somebody scream, Hallelujah

 In the morning when I wake up,
 I will sing my praise unto You my Lord
 I will shout, I will dance to You
 You have been my help, forever and ever

 Hey, my God is good o! (Hey, my God is good o!) (2x)
 Somebody scream
 Take it as high as you want it
 Double, double...

 Hey, your God is good o! (Hey, your God is good o!) (2x)
 Let me hear you shout
 Are you ready? Let's go

Nzambe wa moyo
Nzambe wa moyo

Woza
Are you ready? now, let's go

Ekele kele, ahhh, nzambe wa moyo
Yekele kele, ahhh, nzambe wa moyo

Shuka chini, chini tena, shuka chini, chini tena

Loue, loue, loue (loue)
Loue, Yesu, loue (loue)

Hey, your God is good o! (Hey, your God is good o!) (2x)

Let me hear you make a joyful noise unto the Lord!

Shuka chini, chini tena, shuka chini, chini tena

© Joyous Celebration
Media:

Makala Maalumu: kumbukumbu ya safari ya kundi la Christ ambassadors kutoka Rwanda kuja Tanzania na kuwapoteza wenzao watatu katika ajali ya Gari.

Kundi la Ambasadors of christ choir Rwanda kabla ya ajali
Ambassadors of Christ Choir ni kwaya ambayo kwa sasa inafanya Vizuri sana na nyimbo zake zimekuwa Gumzo hapa nchini. Kundi hili lenye maskani yake nchini Rwanda katika jiji la Kigali hivi sasa limetimiza miezi takribani miwili tangu baadhi ya wanakikundi hicho kufariki dunia tarehe 9/05/2011  walipokuja nchini kwa mualiko wa kwaya ya Acasia Mwenge SDA ya jijini Da es salaam.

Baada ya kupata Mualiko huo, tarehe 5/05/2011 Kundi hilo lilianza safari ya kuja jijini Dar es salaam kwa ajili ya Uzinduzi wa DVD ya kwaya ya Acasia ambao ulipangwa kufanyika katika ukumbi wa PTA ulio katika viwanja vya Sabasaba jijini Dr es salaam.

Ambassadors of Christ walifanikiwa kufika Dar es salaam tarehe 6/05/2011. Kundi hili liliweza kushiriki ibada ya sabato siku ya jumamsi ya tarehe 7/5/2011 na lilialikwa katika Interview katika kituo cha Redio cha Morning Star Adventist Radio of Tanzania kilichoko jijini Dar-es salaam  kwenye kipindi kiitwacho “LULU ZA INJILI”  ambacho hungozwa na Bro Emmanuel Maduhu.

Wakiwa Redioni hapo, kundi hili lilivutia wasikilizaji wengi hasa kwa uwezo wao wa kuimba Live. Tarehe 8/05/2011 ndio siku iliyokuwa ikisubiriwa kwani ilikuwa siku Maalumu kwa kwaya ya Acasia Mwenge SDA Kufanya uzinduzi wa dvd yao ya Pili iitwayo “MNAZARAYO” katika ukumbi wa PTA.

Kundi hilo likiimba wakati wa uzinduzi wa dvd ya acasia choir katika ukumbi wa PTA jijini Dar es salaam
Watu kutoka kona tofauti tofauti za jijini Dar walifurika kutaka kuwaona vijana hawa Live wakiwa jukwaani wakimtukuza Mungu. Muda uliwadia na ndipo vikundi mbalimbali vya injili vilitangulia kuimba wakiwemo Voice of Victory wakifuatiwa na Triumph Generation pamoja na Harvesters vyote vya jijini Dar es salaam.

Muda uliwadia ambapo ukumbi mzima ulizizima kwa furaha na vifijo pindi Ambassadors of Christ walipotajwa kuwa ndio wanafuata kupanda jukwaani. Taratibu huku ala ya nyimbo yao maarufu iitwayo Twapaona vijana hawa walipanda jukwani na ukumbi mzima ulizidi kupiga kelele za furaha.

Miongoni mwa nyimbo ambazo Ambassadors of Christ walizimba Live siku hiyo ni pamoja na Kazi Tufanye, Yesu Ndiye Njia, Twapaona, Kuna Siku, Huyo ni Yesu, pamoja na nyimbo yao maarufu iitwayo Kwetu Pazuri. Watu wote waliofika ukumbini hapo walibarikiwa na kazi za kundi hili kwa utukufu wa Mungu.

Kuhusu Ajali

Baada ya kumaliza huduma tarehe 8/05/2011, kundi zima la Ambassadors of Christ lilianza safari ya kurudi Kigali asubuhi ya tarehe 9/05/2011 kwa njia ya basi. Walipofika Wilaya ya Kahama mkoani shinyanga mnamo saa tatu usiku walikutana na Lorry likiwa limepaki barabarani likiwa halina reflector yeyote. Dreva wa gari la kundi hilo hakuweza kulina lorry hilo na pindi alipoliona na  kutaka kuliovatake  ndipo lorry lingine lilikuwa likija kwa kasi hivyo wakakutana uso kwa uso na ajali ikatokea.

Hali ya Gari la kundi hilo baada ya ajali
Baada ya ajali hiyo iliyotokea  kilometa kadhaa kabla ya kufika Rwanda, wanakwaya watatu wa kundi hil Filbert Manzi, Gatare Ephraim pamoja na mtanzania Amos Fares  ambaye nayee ni muimbaji wakundi hilo aliyekuwa mbele akielekeza njia walifariki papo hapo.

Muda mfupi baada ya ajali hiyo kutokea serikali ya Rwanda ilituma Helkopta ya Jeshi la ulinzi la nchi hiyo [RDF] pamoja na Ambulance mbili kwa ajili ya kusafirishia wagonjwa kutoka Kahama kwenda Hospitali ya Mkoa wa shinyanga. Baada ya kufika Hospitali ya shinyanga wahanga hao waliweza kupata huduma ya kwanza na hatimaye walikimbizwa nchini Rwanda katika Hospitali iitwayo King Faisal kwa matibanu zaidi.

Helkopta ya Jeshi la ulinzi la Rwanda iliyofika kwenye eneo la ajali
Kwa msaada wa Mungu majeruhi wane wa ajali hiyo walipata nafuu na hatimaye kurutuhusiwa kutoka Hospitali. Taratibu za mazishi zilifanywa ambapo Marehemu Filbert Manzi aliyekuwa mmoja wa vingozi wa kwaya hiy na pia mtangazaji wa kitu kimoja cha Redio nchini Rwanda, pamoja na Gatare Efraimu ambaye alikuwa ni muanzilishi na kiongozi wa kwaya hiyo wa walizikiwa nchini Rwanda, wakati Mtanzania Amos Fares yeye alizikiwa nyumbani kwao  mkoani Kigoma.

Zifuatazo ni baadhi ya matukio ya kundi hilo wakati wakiimba jijini Dar na baada ya ajali hiyo.

Majeruhi
Pichani ni kijana Marc Ndizaye kabla na baada ya ajali ila yeye aliruhusiwa baada ya matibabu
Baadhi ya Majeruhi kabla na baada ya ajali
Waliotangulia
Hawa ndio watumishi waliopoteza maisha kufuatia ajali hiyo

Hili ndio kava la Album yao ambapo kushoto mstari wa juu vijana hao watatu Ephraim, Filbert, na Mtanzania Amos hawako nasi tena


Miili ya marehemu Ephraimu na Filbert ikiwa nchini Rwanda

Miili yao ikiwa kanisani

Ephraim ambaye alikuwa kiongozi na muanzilishi wa kwaya hiyo
Philbert Manzi katika siku za utumishi wake chini ya jua
Safari ya Mwisho ya Philbert Manzi

Hatimaye muda huu uliwadia na kuacha simanzi zito

 Mungu anabaki kuwa Mungu kwa lolote afanyalo juu yetu kwa ajili ya Utukufu wake

Hii ni kazi yao iitwayo NI VEMA ambayo inafanya Vizuri sana hapa nchini

 


Friends on Friday Kurindima tena jijini Dar es salaam


Wednesday, July 27, 2011

Mch Danel Kulola na Masanja mkandamizaji waiteka wilaya ya Nzega kwa injili


Mch Daniel Kulola akiwa na Masanja Mkandamizaji
Kwa Takribani wiki moja Mtumishi wa Mungu Daniel kulola akiwa pamoja na Msanii maarufu nchini Kutoka kundi la Ze Comedy Masanja Mkandamizaji  waliiteka wilaya ya Nzega mkoani Tabora kwa Injili ya Yesu Kristo.

Katika mkutano huo uliomalizika jumapili iliyopita Mch Daniel Kulola ndiye aliyekuwa akihubiri injili na huku msanii Masanja ambaye kwa sasa ameokoka alikuwa akiimba na kufanya comedy zilizowavuTa watu wengi wafike kwenye mkutano huo na hatimaye kumpokea kristo.

Hosanna Inc ilifanikiwa kuongea na Mch Daniel kulola wakati wakiwa wilayani hapo na akaiambia kuwa Kazi iliyofanyika Nzega ni Kubwa na watu wengi walimpokea Kristo kama Bwana na Mwokozi wa Maisha yao.

Hii ni approach mpya kufanywa na kanisa katika kuwavuta watu wengi wafike kusikiliza Neno la Mungu, kwa kuwa kwa miaka ya hivi karibuni watu wengi wamekuwa hawana muitikio mzuri wa kuhudhuria kwenye mikutano ya Injili.

From Altar: The Purpose and Power of the Resurrection



As we all celebrate this wonderful day and enjoy ourselves with friends and family we are reminded that mankind's redemption was sealed forever around 2,000 years ago on this day. The Word of God gives an account of how Jesus' grave was found on the dawn of the first day of the week when Mary Magdalene and the other Mary went to look at it. 

The account in Matthew 28 tells of how they encounter an angel and then Jesus himself. In Luke 24:46,47 Jesus explains to the disciples  that it was written that "The Christ will suffer and rise from the dead on the third day and repentance and forgiveness sins will be preached in his name to all nations, beginning at Jerusalem".

Jesus here points back to the scriptures, in this case he had mentioned the Law of Moses, the Prophets and the Psalms as pointing towards what He had to accomplish and how it was to be accomplished. In order for there to be redemption for mankind by the forgiveness of sins and repentance, which is the act of turning away from doing what is wrong in God's sight, the Messiah needed to suffer and die so as to rise from the dead on the third day. 


Isiaiah 53 tells of the work of the Messiah, being despised and rejected by men, but taking up our infirmities and carrying our sorrows! Isiaiah 53:3 tells of how he was 'pierced for our transgressions and crushed for our iniquities' and that His punishment is the one that brought us peace!

Surely now we can sing with confidence that 'there is power, power, wonder working power in the blood!'. In verse twelve of Isaiah 53 we are told that 'he bore the sin of many, and made intercession for the transgressors'. So though we were all cursed by one mans disobedience (Adam), we are all blessed by one mans obedience-Jesus!. Verse 10 of the same chapter in Isaiah tells of how it was 'the Lord's will to crush him and cause him to suffer'. Jesus, while praying in the garden and struggling with the pending tribulation He was about to go through, eventually declares: 'Not my will, but yours, be done' (Luke 22:42). What an act of obedience!

The resurrection power of God was only able to function when Jesus obeyed the Father's will to lay His life down and suffer for us. By going through with this act of obedience, He reveals God's plan for mankind's redemption by first proving that God has the ultimate power over life and death and that all who believe in Him can experience the same benefits of the purpose and power of the resurrection. 


The promise of redemption from sin and it's ultimate power, death, is what makes this day special.  By redeeming us, we have now become sons through faith in Him (Galatians 3:26, 4:5,6, 2 Cor 6:18, Eph 1:5) and have the full right to display His power and glory and have dominion restored to us. 

When you read of all the accounts leading up to His death and the eventual resurrection, you realise that all other miracles pale in comparison! If God raises the dead, then surely He can heal us and deliver us from the evil one! 'For the message of the cross is foolishness to those who are perishing, but to us who are being saved it is the POWER of God' (1 Cor 1:18).

Have a power filled day as you remember the work of the cross!

Be blessed! Be filled with power! Be a good witness of the resurrection!


By John Kagaruki

Monday, July 25, 2011

Zimebaki Siku 24 kabla ya kufanyika Tuzo za Muziki za Afrika mashariki na kati


Zile tuzo zijulikanazo kama East Afrika Music Awards [EAMS], zinatarajia kufanyika Tarehe 20/08/2011 katika jiji la Nairobi. Tuzo hizo ambaz kwa hapa nchini zimedhaminiwa na vitu vya ITV na Radi 0ne, zimehusisha aina mbalimbali za Muziki

Katika kategori za Gospel ambazo Hosanna Inc inapenda kuziongelea, wanamuziki Christina Shusho, Upendo Nkne pamoja na kundi la Mwanza Gospel Singers wanaiwakilisha Tanzania katika tuzo hizo.Nchi zinazoshiriki katika Tuzo hizo ni Tanzania, Uganda, Kenya, Burundi, Rwanda, Congo, Kinshasa, pamja na Somalia.

Wakati umefika kwa watanzania kuwapigia kura watanzania wenzao  ili kuweza kufanikisha ushindi kwa watanzania hao. Hii ni kwa kuwa uwezo wanao na wanamtumikia Mungu katika viwango vya juu kwa utukufu wa Mungu.

Zifuatazo ni taarifa zaidi juu ya kategori ya Hiyo

GOSPEL CATEGORY

Best male

1. Cedric Bangy - "Segneur" - Burundi.
2. Dominique Ashimwe - "Nditabye" - RWANDA
3. Davoit Getachevu - "Tebiaihanehu" - ETHIOPIA
4. Wiseye Willie - "Buye Gigitare" - BURUNDI

Best Gospel Female

1. Christina Shusho - "Unikumbuke" - TANZANIA
2. Gaby - "Amahoro" - RWANDA
3. Alice Kamande - "Upendo Ule ule" - KENYA
4. Upendo Nkone - "Haleluyah Usifiwe" - TANZANIA

Best Gospel Group

1. Nef Thalem Assegid - " Nebse" - ETHIOPIA
2. Mwanza Gospel Choir -Nivema" - TANZANIA
3. B.M.F - "I live for you" - KENYA

Best Gospel Collabo

1. Emmy Kosgei ft. Lynn. "Omegeu Rerein" - KENYA
2. Mbuvi Ft. Kambua - "Kivevelo" - KENYA


Ephraim sekeleti kutua nchini mwezi Ujao

Ephraim Sekeleti
Mwanamuziki anayekubalika sana nchini Tanzania akitokeaa nchini Zambia aitwaye Ephraim Sekeleti, anatarajiwa kuja nchini Tanzania mwezi ujao[August]. Sekeleti ambaye nyimbo zake kama Ndani ya Jina, Uniongoze,na Huu Mwaka  zimempa umaarufu sana hapa nchini. 

Sekeleti aliiambia Hosanna Inc ijumaa iliyopita kuwa ujio wake huo utakuwa sambamba na kuitambulisha albium yake mpya iitwayo “Acha Kulia

Sekeleti alizidi kusema kuwa album yake hiyo ambayo mkimsingi ni ya Pili kwa upande wa album zake alizoimba kwa Lugha ya  Kiswahili inajumla ya nyimbo kumi na mbili[12] na Katika nyimbo zote hizo kazifanya akiwa nchini zambia.

Hosanna Inc ilitaka kujua kama kuna wanamuziki wa injili kutoka Tanzania ambao wanajulukana nchini ZAMBIA. Katika kulijibu swali hilo Sekeleti alisema  Zambia wanamjua sana Rose Muhando na wengine kidogo. Mpaka sasa Ephraimu Sekeleti ameshatoa wimbo mmoja uitwao Uniguse Bwana ili kuitambulisha album yake hiyo mpya.

Picha Yetu Jumatatu Hii


Pichani ni Mtumishi wa MUNGU kutoka nchini Tanzania aitwaye Mheshimiwa Nabii Geo Davie a. Hapo ni katika moja ya ziara zake nchini.

Sunday, July 24, 2011

Sunday Sermon: Namna Ya Kumtumia Roho Mtakatifu Kama Msaidizi Kupitia Kazi Zake


Yohana 14:16-18 … Nami nitamwomba Baba, naye atawapa Msaidizi mwingine, ili akae nanyi hata milele; ndiye Roho wa kweli; ambaye ulimwengu hauwezi kumpokea, kwa kuwa haumwoni, wala haumtambui; bali ninyi mnamtambua, maana anakaa kwenu, naye atakuwa ndani yenu”.

Katika somo hili nataka kuandika juu ya kazi za Roho Mtakatifu na kukuonyesha namna unavyoweza kumtumia Roho Mtakataifu kama Msaidizi kupitia kazi zake. Labda niseme kwa lugha hii, kama unataka kuona msaada wa Roho Mtakatifu kwenye maisha yako, ni lazima kwanza uzijue kazi zake, maana kazi zake ndizo zinazotuonyuesha maeneo ya msaada wake, kazi zake ndizo zinazofafanua kwa namna gani Roho Mtakatifu ni Msaidizi.

Roho Mtakatifu ni nani?
Roho Mtakatifu ni Mungu, mwenye nguvu zote, maarifa yote, anayepatikana kila mahali. Yeye anayo nafsi na ameamua kuishi ndani ya mwili wa mwanadamu. Kusudi kubwa la ujio wake ni kuwa Msaidizi wa mwanadamu kwenye ulimwengu huu wa mwili, ili kumsaidia kuishi katika mapenzi ya Mungu.

Roho Mtakatifu amemamua kuishi ndani ya mwili wa mtu kwa sababu, Mungu hana namna ya  kutawala kwenye ulimwengu wa kimwili bila kuwa na mwili wa damu na nyama, kwa kuwa yeye ni Roho (Yohana 4:24). Hivyo hana budi kuingia kwenye mwili wa mtu na kufanya makao yake hapo, ili kutawala na kumuongoza mwanadamu katika mapenzi yake. (Yohana 14:23, Yohana 14:18, Ufunuo 3:20, 1Wakorinto 3:16-17, 6:19).

Kinachotusaidia kujua kwamba Roho Mtakatifu ana nafsi, ni tabia zake, maana kwenye kila nafsi kuna hisia, nia, kumbukumbu, akili nk. Baadhi ya sifa na tabia za Roho Mtakatifu ni;
1.      Anapatikana kila mahali (Omnipresence), Zaburi 139:7,
2.      Ana maarifa/anajua yote (Omniscient, Intelligence), 1 Wakorinto 2:10-11,
3.      Mwenye nguvu zote/wa umilele (Omnipotent), Mwanzo 1:2,
4.      Mtakatifu, Luka 11:13, ana hisia (Waefeso 4:30, Mwanzo 6:3) – Wala msimuhuzunishe Roho wa Mungu…, Roho yangu haitashindana na Mwanadamu milele, ana nia (will), 1Wakorinto 12:11 – Hutenda kazi kama apendavyo.

Kazi za Roho Mtakatifu
  • Kufundisha, Mwalimu (Yohana 14:26) … Atawafundisha yote…
  • Kuongoza, Kiongozi (Warumi 8:14, Yohana 16:13) – Atawaongoza awatie kwenye kweli yote, wote wanaoongozwa na Roho hao ndio … Mfano (Matendo ya Mitume 13:4, Acts 8:29)
  • Ni mfunuaji wa mambo/mafumbo/siri za Mungu (1Wakorinto 2:10) – Lakini Mungu ametufunulia sisi kwa Roho. Maana Roho huchunguza yote. Usipoteze muda kumtaka Mungu akufunulie siri zake, wewe mwambi Roho Mtakatifu hiyo ndiyo kazi yake.
  • Muombezi (Warumi 8:26) – Roho hutuombea kwa kuugua kusikoweza kutamkwa.
  • Mtoa/mpasha habari za mambo yajayo (Yohana 16:13f) – Na mambo yajayo atawapasha habari yake.
  • Ni msemaji wa mambo ya Mungu/Yesu (Yohana 15:26, 2 Petro 1:21) – Yeye atanishuhudia (he will speak about me), Wanadamu walinena yaliyotoka kwa Mungu wakiongozwa na Roho Mtakatifu.
  • Ni mtetezi/msemaji wa mambo yetu (Marko 13:11) – Kwa maana si ninyi msemao, bali ni Roho Mtakatifu.
  • Ni mkumbushaji wa yale uliyojifunza au uliyoagizwa na Mungu (Yohana 14:26)… Atawakumbusha yote niliyowaambia.
  • Kutia/kuwapa nguvu watu wake nguvu/uwezo (Matendo1:8) – Lakini mtapokea nguvu akisha kuwajilia juu yenu Roho Mtakatifu…
  • Kuuhakikisha (convict, make aware, sadikisha) ulimwengu kwa habari ya dhambi, haki na hukumu (Yohana 16:8) e.g unajuaje kwamba kuna hukumu? Warumi 8:16
Naam kazi hizi za Roho Mtakatifu zinatufikisha mahali pa kujua kwamba jukumu lake kubwa ni kuwa Msaidizi wa mwanadamu. Kufanyika msaada wa mwanadamu katika mambo hayo hapo juu pale mwanadamu atakapohitaji msaada huo.  Hivyo ni jukumu lako kumpa nafasi kwa kuboresha mahusiano yako na yeye ili akusaidie. Hata hivyo Roho Mtakatifu kuitwa Msaidizi haina maana kwamba ndio umvunjie heshima, bali fahamu kwamba, Roho Mtakatifu ni Msaidizi kwa namna ambayo bila yeye mimi na wewe hatuwezi kutenda neno lolote.

Kazi hizi zinatupa kujua kwamba Roho Mtakatifu yupo tayari kutusaidia katika kila eneo la maisha yetu. Ni jukumu letu kumpa  nafasi hiyo na kutambua kwamba bila msaada wake sisi hatuwezi lolote. Watu wengi leo hawaoni msaada wa Mungu kwao kwa sababu ya kutokumpa Roho Mtakatifu nafasi ya kuwasaidia katika maisha yao na pia kwa kutokujua maeneo ya kumtumia Roho Mtakatifu kama Msaidizi.


Je, unahitaji msaada wa Roho Mtakatifu eneo gani la maisha yako?, ni ndoa, kazi, madeni, huduma, kanisa, utawala nk mpe nafasi akusaidie, akufundishe na kukuongoza katika kweli yote. Kumbuka yeye ni Mungu ambaye ni Mwalimu na Kiongozi pasina yeye mimi na wewe hatuwezi neno lolote. Unataka kumjua Mungu, kuwa na maombi yenye matokeo mazuri na kufanikiwa katika maisha yako kiroho na kimwili pia mwambie Roho Mtakatifu akusaidie.

Msaada wa Roho Mtakatifu hauna mipaka maadamu unahitaji msaada katika yale ambayo ni mapenzi ya Mungu. Hivyo haijalishi unapita katika jambo gani mpe nafasi Roho Mtakatifu akusaidie. Na ili uweze kuthamini msaada wa Roho Mtakatifu jifunze siku zote kufikiri kwa dhana kwamba bila msaada wake wewe huwezi lolote, na kwa sababu hiyo utaona umuhimu wa yeye kukusaidia katika maisha yako.

Usisubiri mambo yako yaharibike au usiachague mambo unayofikiri magumu ndio umshirikishe akusaidie, yeye anataka kuwa Bwana wa maisha yako, akusaidie kwa kila kitu hata mambo madogo kabisa kwenye maisha yako. Kina-muumiza Mungu kuona watoto wake chini ya jua wanahangaika katika maisha yao, wakati yeye amemleta Roho Mtakatifu ili awasaidie katika maisha hayo. Tumia vizuri fursa ya Roho Mtakatifu sasa maadam anapatikana, kuna wakati hatapatikana.

 Neema ya Kristo iwe nawe
 Na:Patrick Sanga

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...