Saturday, May 28, 2011

Namna ya kumpigia kura C.Shusho kwenye Tuzo za Afrika (AGMA)



Africa Gospel Music Awards (AGMA) ni Tuzo kubwa zinazowahusisha wanamuziki wa Injili Barani Afika. Tuzo hizi za zenye jumla ya kategori ishirini, ndani ya kategori zote  Christina Shusho ndiye Mwanamuziki pekee toka Tanzania aliyefanikiwa kuingia kwenye kinyang`anyiro cha kuwania tuzo ya “Mwanamuziki Bora wa Injili Afrika Mashariki’. Katika kategori hiyo aliyomo wamo pia

Best Artist From E. Africa
1.         FABRICE NZEYIMANA
2.         ALICE KAMANDE- KENYA
3.         EXODUS-UGANDA
4.         CHRISTINA SHUSHO-TANZANIA
5.         BLESSED SISTERS-RWANDA
6.         GEN. MANASSEH MATHIANG-SOUTHERN SUDAN
7.         JOY NKUNDIMANA-BURUNDI 
8.         JULIANI KENYA    
9.         EMMY KOSGEI-KENYA
10.       MOSES \"QQU\" ODHIAMBO       
11.       DADDY OWEN- KENYA  
12.       MARVELLOUS

Namna ya Kupiga Kura

Ili kupiga kura unapaswa kuingia kwenye tovuti ya (AGMA) iitwayo www.africagospelawards.com kisha Click sehemu iliyoandikwa VOTE.

Baada ya kuclik vote, utakuja ukurasa mwingine utakaokukupa option 1. kuandika barua pepe yako(email addres), 2.Kuhakiki barua pepe yako (unaiandika email yako mara ya pili) 3. Unajisajili(unaclick-Register).

Ukimaliza taratibu hizo wao watakutumia barua pepe kwenye barua pepe yako. Ukiifungua barua pepe hiyo iliyotoka kwao utakutana na neno CLICK HERE TOVOTE na ukishaclick itakuja orodha ya kategori zote ishirini na utaclick YES kwenye jina la Mwanamuziki unayemchagua kwa kategori husika.



AGMA wameamua kutumia upigaji kura kwa njia ya Email ili kupunguza uwezekano wa mtu mmoja kupiga kura mara nyingi. Ni matumaini yetu Hosanna Inc kuwa watanzania watampigia kura Christina shushu sio tu kwa sababu ni Mtanzania mwenzetu, bali kwa sababu anastahili kupokea Tuzo hiyo.

Christina Shusho

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...