Tuesday, February 21, 2012

Benjamin Dube kuachia His New DvD called Healing in His Presence




Nguli wa Muziki wa injili nchini Afrika ya Kusini  Pastor Benjamini Dube ndani ya wiki hii anatarajia kuachia album yake mpya ya DVD HEALING IN HIS PRESENCE. Dube anasadikika kuwa mmoja ya wanamuziki wa injili wenye mafanikio makubwa nchini humo, DvD hii itakuwa ni muendelezo wa Dvd zake nyingine zilizopewa jina Hilo hilo la IN HIS PRESENCE japokuwa hulibadilisha kwa kuliongezea neno kadri aonavyo Vema.

Benjamin Dube ambaye ziara yake na Kekeletso Phoofolo(KEKE) ilifanikiwa kumtangaza keke vilivyo na hatimaye kukubalika nchini humo na nje ya nchi hiyo, mwaka jana alipata nafasi ya kuja nchini Tanzania kwa Mwaliko wa wa Pastor Isack Malonga wakati wa event ya R.I.O.T. Hapa chini ni album yake ya mwisho iliyoitwa WORSHIP IN HIS PRESENCE kabla yah hii mpya iitwayo HEALING IN HIS PRESENCE.



1 comment:

  1. your worship blesses pastor keep the gud spirit nd let Gof be the leader

    ReplyDelete

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...