Thursday, June 16, 2011

Miriam Lukindo Kuizindua ni Asubuhi jijini Mwanza


Miriamu Lukindo
Mwanamuziki Mahiri wa nyimbo za Injili maarufu kwa jina la Miriam Lukindo, jumapili hii ya tarehe 19/06/2011 anatarajia kuzindua album yake iitwayo Ni ASUBUHI katika uwanja wa ccm Kirumba kuanzia majira ya saa tisa mchana. Miriam ambaye ni mke wa mwanasaikolojia  na mtangazaji maarufu aitwaye Chriss Mauki ameshafanya uzinduzi wa kazi yake hiyo jijini Dar es salaam.

Baada ya kuzindua album hito jijini mwanza tarehe 21/06/2011 anatarajia kufanya uzinduzi mwingine katika Visiwa vya Ukerewe. Katika uzinduzi wake huo kanda ya ziwa Miriam ataambatana na Wanamuziki wengine wa injili akiwemo


Upendo Nkone
Joseph Nyuki
Kijitonyama Upendo Group
Martha Mwaipaja




No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...