Tuesday, August 23, 2011

Christina Shusho aibuka Mwanamuziki Bora wa Kike wa Nyimbo za Injili Afrika mashariki na Kati



Mwana mama kutoka Tanzania Christiana Shusho ameibuka kuwa mwanamuziki Bora wa Kike wa Muziki wa Injili kwa nchi za Afrika mashariki na kati katika Tuzo ziitwazo East Afrika Music Awards (EAMA`S) zilizofanyika jumamosi iliyopita jijini Nairobi nchini Kenya.

Katika tuzo hizo Tanzania Tuliwakilishwa na wanamuziki wa injili wapatao wawili ambao ni Christina Shusho, Upendo Nkone ambao kwa pamoja walikuwa wakiwania Tuzo ya Mwanamuziki bora wa kike wa injili kwa Afrika mashariki . Pia kwa upande wa Makundi tuliwakilishwa na Mwanza Gospel Choir ambao wao walikuwa wanawania tuzo ya Kundi bora la muziki wa injili kwa Afrika mashariki. 

Christina Shusho
Mashindano hayo yaliyojumuisha aina mbalimbali ya muziki ukiwemo wa injili huku yakishirikisha jumla ya nchi nane ambazo ni Tanzania, Kenya, Uganda, Burundi, Rwanda, Ethiopia, Sudani pamoja na Kongo Kinshasa(DRC) na kuonyeshwa moja kwa Moja na Kituo cha ITV.


Yafuatayo ni majina ya washiriki waliokuwa wakiwania Tuzo hizo na wenye rangi ya nyekundu ndio washindi huku kwa upande wa wanaume walipatikana washindi wawili.

Gospel Category

Best Male
 
1. Cedric Bangy - "Segneur" - Burundi.
2. Dominique Ashimwe - "Nditabye" - RWANDA
3. Dawit Getachew - "Etebikihalehu" - ETHIOPIA
4. Wiseye Willie - "Buye Gigitare" - BURUNDI


Best Gospel Female

1. Christina Shusho - "Unikumbuke" - TANZANIA
2. Gaby - "Amahoro" - RWANDA
3. Alice Kamande - "Upendo Ule ule" - KENYA
4. Upendo Nkone - "Haleluyah Usifiwe" - TANZANIA


Best Gospel Group

1. Nef Thalem Assegid - " Nebse" - ETHIOPIA
2. Mwanza Gospel Choir -Nivema" - TANZANIA
3. B.M.F - "I live for you" - KENYA


Best Gospel Collabo

1. Emmy Kosgei ft. Lynn. "Omegeu Rerein" - KENYA
2. Mbuvi Ft. Kambua - "Kivevelo" - KENYA


1 comment:

  1. waimbaji wa kiume mpo wapi huku tanzania?

    ReplyDelete

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...