Monday, January 30, 2012

Picha Yetu Jumatatu Hii: Prophet Eubert Angel Akihudumu


Pichani anaonekana mtumishi wa Mungu Prophet Eubert Angel wa kanisa la Spirit Embassy la nchini Zimbabwe akifanya maombezi.Prophet Angel ni mmoja kati ya Ma Prophet vijana ambao wanakubalika sana Barani Afrika kwa utumishi wao.

Dr Mwakyembe Amshukuru Mungu Baada ya Kupona


Josephat Gwajima wa kanisa la Ufufuo na Uzima lilloko Kawe Tanganyika Pakers akimkaribisha Dk Harrison Mwakyembe Mbunge wa Kyela na Naibu Waziri wa Ujenzi katika ibada iliyofanyika jana kanisani hapo.
Dk. Harrison Mwakyembe alifika kanisani hapo na kutoa  ushuhuda akimshukuru mungu kwa kumbariki na kuendelea kumpa nguvu juu ya afya njema, Mwakyembe ambaye alikuwa amevalia kofia na Glovu katika mikono yake, ameongeza kwamba tangu alipokuwa ameondoka kwenda nchini India kwa matibabu Oktoba 9 mwaka jana hakuwahi kuvaa viatu, lakini leo amevaa, hivyo akamshukuru mungu kwa miujiza yake.

Waziri wa Afrika Mashariki Samwel Sitta akiongea katika ibada hiyo kisha akamkaribisha Dk Harrison Mwakyembe
Dr Mwakyembe aliongozana na wabunge kadhaa kwenda kanisani hapo akiwemo Waziri wa Afrika Mashariki mzee Samwel Sitta,kwa upande wake Mzee Samwel Sitta amesema Mwakyembe amekwenda kanisani hapo ili kutoa ushuhuda kuhusu ugonjwa wake kwa ujumla.

Source:John Bukuku

Sunday, January 29, 2012

Kauli za watumishi wa MUNGU Kwenye Mitandao Jamii wiki hii

 Kutoka mtandao wa Twitter




Pastor Rick Warren

 
Rick Warren
Today, be the living expression of Jesus' kindness to everyone - with your words, smile, eyes, & hands.

Bishop jamalbryant


The people who are mad about what you've achieved.....have no power to stop what you are destined to accomplish!

CeCe Winans


It's time to go higher in God!!! Let's elevate our minds so that we can continue to give God more. He wants our best!!!


Kutoka mtandao wa Facebook

   

Bishop TD Jakes

‎Forgiveness is a BIG idea! It takes a person who thinks big ideas, rather than comparatively small thoughts, to introduce and practice forgiveness effectively. God saw the grand scheme of things and knew it was going to take an equally grand plan of forgiveness to bring each of us back to Himself. Have you accepted God’s BIG idea?

Pastor Isaac Malonga


"Do not try to Imitate what God is doing, before you Imitate His Heart" - Bishop Tumwidike”.

Dada Mary Damian-Strictly Gospel


  









Mary Damian
Mwaka mpya umeshaanza na maisha yanaendelea...hekima ya Mungu ikawe juu yetu kutambua fursa zitakazotokea...ni wakati wa kufanya maamuzi, kuyaendea maono na kuifanya kila siku iwe nzuri...Nawatakia heri wandugu!


 Mada kutoka Facebook Group la wajoli

                         

"Mnaposali msipayuke payuke ili watu wawasikie........"Je ni sawa kusali kwa sauti tunapokusanyika kufanya maombi tena wengine sauti ya kupayuka kabisa?kwa nini kila mtu asisali kimoyomoyo bila kutoa sauti ?



Top of Form
Emmanuel Ivan Msamba ULOKOLE NI UFARISAYO MAMBO LEO!


Emmanuel Destiny Man Huu nao ni uchanga wa kiroho.




Emmanuel Ivan Msamba ‎.1 Samuel 3:7-11
7 Now Samuel did not yet know the LORD: The word of the LORD had not yet been revealed to him.

8 A third time the LORD called, “Samuel!” And Samuel got up and went to Eli and said, “Here I am; you called me.”

Then Eli realized that the LORD was calling the boy. 9 So Eli told Samuel, “Go and lie down, and if he calls you, say, ‘Speak, LORD, for your servant is listening.’” So Samuel went and lay down in his place. .

Denn'o Franco kupayuka ni kuongea maneno yasiyo na maana, sio kuomba kwa sauti


Denn'o Franco kuna faida kadhaa kwanini tunaomba kwa sauti, kwanza, kuzuia interfereance ya vitu vingine kwenye maombi yako. Pia kama ujuavyo shetani hapendi watu waombe ukifanikiwa kushinda kuomba kila siku zaidi ya saa2 basi umetoboa wengi hawawezi, hivyo shetani huleta usingizi. ukiomba kimya kimya waweza jikuta umelala. na hata hukumbuki ulikuwa unaomba


Mgisa Mtebe ‎"Msipayuke-payuke" katika sala na maombi haimaanisihi "sauti kubwa" mpendwa! Ni udhaifu wa Kiswahili tu ndo unaotugonganisha hapa. Soma msatari huo katika kiingereza utaona jinsi watafsiri wanavyoweza kupotosha kanisa. King James Version Bible ametumia neno "Vain Repititions" yaani Kurudia-rudia Maneno bila maana na mpangilio. Bible nyingine ya Kiingereza imetumia Neno "Bubbling" yaani kulipuka-lipuka au kuropoka-ropoka, ikiwa na maana kutamkatamka maneno bila mpangilio unaoleta maana. Ila Waswahili waliotafsiri Bible enzi ile, walikosa msamiati sahihi, au ni wa madhehebu yasiyokubaliana na kusali kwa sauti, hivyo yamkini wali-intend kuipotezea kwa style hiyo.

Tunapokwenda mbele za Mungu, tunatakiwa tujipange kifikra ili uwe na maneno yenye maana na mtiririko mzuri hata kama unasali kimya-kimya au unasali kwa sauti. Somo la Yesu ktk mistari hii halikuhusu sauti, kwani hata Yesu mwenyewe alikuwa anasali kwa sauti na kwa machozi mpaka ikabidi awe anakwenda mlimani, ili kupata utulivu lakini pia ni ili asisumbue majirani (Waebrania 5:7) "Yeye (Yesu) katika siku za mwili wake, alimtolea (Mungu) ... maombi na dua na kulia sana na machozi." Siku ya Pentekoste, Roho aliposhuka kwa kanisa, Kanisa lilipuka kwa maombi ya pamoja na sauti kuu ikasikika mji mzima, kutoka katika kile chumba cha ghorofa. Fikiria sauti iliyowakusanya watu wa mji mzima, ni sauti kubwa kiasi gani. (Matendo 2:1-4). "...wakampazia Bwana sauti zao..." katika maombi (Matendo 4:24).

I stand to be corrected!

Emmanuel Ivan Msamba Mhhh! Denn'o Franco! Uliwahi kusoma sehemu yoyote iliyoonyesha kuwa waumini wa kanisa la mwanzo enzi za mitume walisali kama tunavyopayuka walokole siku hizi? Kama ni kwa sauti ni kwa nini basi asisali mmoja baada ya mwingine? Iko wapi ile 'NENA BWANA MTUMISHI WAKO ANASIKIA?'




Mgisa Mtebe Baada ya kusoma maelekezo hayo hapo chini, utagundua kwamba, ni lazima mtu anapotaka kwenda mbele za Mungu, ajiandae kifikra na kujipanga kumweleza Baba haja za moyo wake. Usiende mbele za Mungu na kuanza kuongea bila kufikiri. Ndio maana Mhubiri 5:1-2 "Jitunze mguu wako unapokwenda mbele za Mungu, usiwe na maneno mengi, kwasababu Yeye ni Mfalme wako na yuko juu. Ni bora uende kusikia kuliko kutoa kafara ya kipumbavu (maelezo yamefafanuliwa)". Kafara ni sadaka. Na sadaka zi lazima ile tuliyozoea. Kuna sadaka za maneno (Biblia inaita, 'dhabihu' za sifa). So usiende mbele za Mungu kuongea bila kujipanga.

Nadhani utakuwa umeshawasikia watu waliomzoea Mungu na waliozoea sana kuongea na Mungu kwa kuropoka, ni wale wanaosali asubuhi lakini katika maneno yake kwa Mungu, anajikuta amesema "Baba tunakuja mbele zako jioni ya leo" ingawa time hizo ni asubuhi. Hiyo ndio kuropoka. Ni kuongea kwa mazoea, bila kufikiri.Ndio maana Mhubiri 5:1-2 "Jitunze mguu wako unapokwenda mbele za Mungu, usiwe na maneno mengi, kwasababu Yeye ni Mfalme wako na yuko juu. Ni bora uende kusikia kuliko kutoa kafara ya kipumbavu (maelezo yamefafanuliwa)".


Saturday, January 28, 2012

Mwakasege akosoa mfumo wa elimu ya juu.


Mwl Christopher Mwakasege
Mwl Christopher Mwakasege, amesema mfumo wa elimu inayotolewa hapa nchini haiwezi kuwajenga Watanzania katika kukabiliana na ushindani kwenye soko la ajira.

Mwakasege ambaye ambaye amemaliza semina yake mkoani Kilimanjaro  kwenye uwanja wa mashujaa, Mwl Mwakasege alitoa kauli hiyo mwishoni mwa wiki katika semina maalumu iliyohusu “UELEWA WA KUSUDI LA MUNGU KATIKA MASOMO”.
Semina hiyo ilifanyika kwenye uwanja wa mpira wa Chuo Kikuu Kishiriki cha Ushirika na Biashara (MUCCoBS) na kuhudhuriwa na na mamia ya watu wakiwemo wanafunzi wa chuo hicho.

Huku mahubiri yake yakionekana kuwagusa wanafunzi wengi, Mwakasege alisema mfumo wa elimu unaotolewa hapa nchini unalenga kuandaa viongozi na si wataalamu.
Alisema Hayati Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere, alikuwa na maono kwa kuanzisha Chuo cha Kivukoni ambacho kilikuwa mahsusi kwa ajili ya kuandaa viongozi na haikujalisha kama walikuwa wamesoma sana.

Alisema kutokana na mfumo wa kisiasa kubadilika baada ya Tanzania kuridhia mfumo wa vyama vigi vya siasa, Chuo cha Kivukoni kwa sasa kimebaki kuwa cha kupika makada wa chama.

Aliwataka wasomi hao kujiuliza kwa nini wanasoma na wanafanya hivyo kwa ajili ya nani na kuongeza kuwa elimu ni mfumo uliotengenezwa kuunganisha sekta mbalimbali katika mamlaka za mataifa mbalimbali duniani.

Alisema kila taifa linao mfumo tofauti wa elimu na kutolea mfano elimu ya Marekani ambako alidai ili uwe daktari sharti usome kwa miaka saba na baada ya hapo ufanye kazi miaka mitatu ukiwa chini ya daktari mtaalamu kabla ya kuhalalishwa kuwa daktari kamili.
Mwakasege alidai kuwa tofauti na Marekani nchi nyingine ikiwamo Tanzania madaktari wanasoma miaka mitano na baada ya hapo wanakuwa madaktari kamili.

Naye mwenyekiti wa maandalizi ya semina hiyo, Paul Makonda, alisema katika semina hiyo kuwa taifa haliwezi kuendelea pasipo watu wake kufuata mafundisho ya Mungu.

Paul Makonda
Hosanna Inc ilifanikiwa kuongea na Mtumishi wa Mungu Komredi Paul Makonda ambaye ni mwanafunzi(MUCCoBS),na ni Mjumbe wa mkutano mkuu wa CCM Mkoani Kilimanjaro na pia ni Mwenyekiti wa Muungano wa wanafunzi wa vyuo vya Elimu ya juu nchini Tanzania (TAHLISO). Makonda Nini hasa kilichopelekea wanafunzi wa (MUCCoBS)  kuandaa semina hiyo na hiki ndicho alichotuhabarisha.

Paul Makonda: Kuna uhusiano mkubwa kati masomo tunayosoma vyuoni na kusudi la Mungu juu ya Maisha yetu, hivyo kwa kulitambua hivyo ikabidi tumtafute Mwalimu Mwakasege kama mtumishi wa Mungu aweze KU-LINK hilo suala, i mean uhusiano uliopo kati ya Kusudi la Mungu na Masomo tunayosoma.

Kaka skufichi Mwakasege alitisha, alielezea kwa kina akitumia Kitabu cha Daniel pamoja na Habakuki, aligusia mambo mengi ikiwemo kwa nini watu wanasoma digrii nyingi anaanza na hii kisha anabadilisha.

Source: Tanzania Daima, Hosanna Inc

William McDowell Worship Pastor aliyefanya vizuri kwenye I give myself a way


William McDowell ni mmoja kati ya watumishi wa Mungu wanaokubalika sana Duniani katika uimbaji. McDowell amekuwa maarufu sana hasa baada ya album yake ya I give myself a way kugusa mioyo ya wengi. Kabla McDowell hajaanza kuimba rasmi nyimbo zake binafsi na kuzitangaza amekuwa music Director wa Dr Ron Kenoly ambaye ni mmoja ya wakongwe wanaoheshimika sana Duniani katika uimbaji wa nyimbo za Injili.


McDowell amekuwa pia akimtumikia Mungu kama worship Pastor wa kanisa la Gathering Church ambalo linaoongozwa na  Sam Hinn mdogo wake na Benny Hinn. Katika moja ya interview zake na vyombo vya habari McDowell alisema “Mimi ni mume na baba katika familia yangu, na familia yangu ndiyo huduma yangu ya kwanza.

I give myself away ilipotoka, ilikaa kawenye chart za Billboard (gospel) kwa wiki 33. Kwa sasa McDowell anaishi Florida nchini Marekani na anamiliki studio yake binafsi iitwayo Delivery Room. Mpaka sasa wanamuziki wengi wakubwa wa injili wameshafanyia kazi zao wakiwamo  Israel Houghton Martha Munizzi, Trent Cory, Group 1 Crew, Dewayne Woods, KJ-52.

Hosanna Inc iliwahi kufanya mahojiano na Mwanamuziki wa Injili kutoka Tanzania aitwaye Miriam Lukindo na kumuuliza katika uimbaji wako unahisi wapi unafiti zaidi? Miriam alicheka kidogo kisha akasema siwezi ficha Mimi ni Worshiper. Swali hilo hilo aliulizwa Christina Shushu Mwaka jana(2011) alipoalikwa na katika kipindi cha RAUKA katika CITIZEN TV ya nchini Kenya, Shusho alisema Napenda sana kuabudu na ninapoimba nyimbo za worship nakua huru zaidi.

Swali hilo alipoulizwa McDowell alijibu “I would say that I am definitely a worshipper and that comes across in my music. I would also say that God defines what I present as a "messenger style". I am a worshipper at my core, but I do find that I deliver prophetic messages when I minister.

Kupitia Nyimbo hii ya I give myself away, McDowell alianzia Movement maalumu iitwayo “I give myself away Campaign” ikiwa na lengo la kuwasaidia mamilioni ya watu waishio kwenye mazingira magumu hususani katika kuwapatia maji safi watoto na familia kutoka sehemu mbalimbali duniani.

Thursday, January 26, 2012

Live Tele-Seminar with Mwl C. Mwakasege on Saturday Jan 28th 2012


Mwalimu Christopher Mwakasege
MANA MINISTRIES(USA) We are glad to invite you once again to the special Live Tele-Seminar in which Mwalimu Christopher Mwakasege from Arusha Tanzania will be teaching and praying live for all mainly who are in Diaspora( USA, Europe, Canada, Africa, Asia etc) on Saturday Jan 28th 2012
This seminar will be teleconferenced live all over the world. Regardless of where you are at, you can still participate.
TIME: USA & CANADA: 9am [Central time- MN/TX etc], 10am [Eastern Time], 7am-[Pacific Time]
          ASIA & RUSSIA: 5pm- Jerusalem, 8pm Karachi, 11pm Hong Kong
          AFRICA: 6pm-[East African time], 3pm [West African time], 4pm [Central African time]
          EUROPE: 3pm- London-UK, 4pm- Rome, 5pm- Sophia
         AUSTRALIA: 2am(Sunday morning)-Sydney
Teleconference: Call 218-895-2851 Pass-code: 9102011
Due to high volume of callers, would advise you log in even few minutes ahead of time in order to be there on time. You keep on logging in till you get in. Prayers will start 30 minutes before the seminar.
Should you have any question,please do not hesitate to contact MANA MINISTRIES(USA) at:
Telephone: Toll free 1888-481-6077 // 6513340163
Email: info@mikutano.com
Looking forward to seeing you on Saturday and please share these information with others!

By MANA MINISTRIES (USA)

Wananchi nchini Nigeria wamlaumu Rais Jonathan kwa ukimya wake dhidi ya Mashambulio dhidi wakristo


Askari wa Kundi la Boko Haram
Wakati Mashambulio ya magaidi nchini Nigeria yakiendelea  dhidi ya wakristo nchini humo,wanachi wan chi hiyo wamekuwa wakilaumu kila kukicha utawala wa serikali ya nchi hiyo iliyo chini ya Rais Goodluck Jonathan kwa kutochukua hatua za kutosha kuikomesha hali hiyo inayodaiwa kuendeshwa na magaidi wa kundi la Boko Haram.


Rais Jonathan ambaye ni mkristo na jina lake la kati anaitwa Ebelechukwu likimaanisha “Rehema za Mungu” amesema inawezekana kuna viongozi wa serikali yake ambao wanatumika kupeleka habari katika kundi la Boko Haram ambalo kwa muda sasa limekuwa likidaiwa kufanya mashambulio katika makanisa pamoja na ofisi za serikali. Kwa mujibu wa CNN wananchi kwa hasira wamekuwa wakitembea barabarani wakiwa mamebeba mabango na majeneza ya kebehi yakiwa na maneno yasemayo President Badluck.

Wananchi wamekuwa wakihoji kwa nini mashambulio hayo yanazidi kutokewa pasipo viongozi wa juu wa ulinzi nchini humo wakiwa hawajawajibishwa. Mashambulio hayo yanadaiwa kusababisha  kuyumba kwa umoja wa raia wa nchi hiyo. 

Mch Ayo Oritsejafor
Mch Ayo Oritsejafor ni Raisi wa chama cha wakristo nchini Nigeria (Christian Association of Nigeria's CAN),Mch Ayo amesema serikali imeshindwa kufanya maamuzi ya msingi kunusuru maisha ya wakristo. Aidha mch Ayo amesema viongozi wa Ulinzi nchini humo wamekuwa wakiwapa taarifa Boko Haram hivyo inakuwa ni ngumu kudhibiti mashambulio hayo kwa kuwa baadhi ya viongozi wa ulinzi nchini humo wameweka mbele na kuthamini udini kuliko utaifa.

Wiki iliyopita bomu moja lililodaiwa kulipuliwa na kundi la Boko haram lilipoteza uhai wa  jumla ya raia 150 katika jiji la kano nchini humo. Rais Jonathan ambaye amekuwa akitumia ukurasa wake wa facebook kutoa maoni yake kwa muda sasa amekuwa kimya huku watu wengi wakimuandikia comments za lawama kwa kutochukua hatua kali dhidi ya mashambulio hayo kwa wakristo.

Source: Christian post
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...