Tuesday, September 20, 2011

Kisima Music Awards 2011



Kisima Award ni Tuzo za Muziki zinazohoshimika sana nchini Kenya, Tuzo hizo huusisha muziki wa aina mbalimbali kwa maana ya muziki wa kumtukuza Mungu pamoja na muziki wa Dunia(Circular Music). 

Katika Tuzo hizo za Kisima kwa Mwaka Huu wa 2011 katika kategori ya Gospel Music  ambayo imeunganisha wanamuziki wa injili wa-kiume na wa kike pamoja na makundi na kuwa kategori moja. waliochaguliwa kuwania Tuzo hiyo ni kama ifuatavyo.

GOSPEL – ARTIST GROUP OF THE YEAR

• Uwezo - Adonage
• I live for you - BMF
• Tobina - Daddy Owen
• Taunet Nelel - Emmy Kosgei
• Bahasha ya Ocampo - Juliani
• Papa God Oh - MOG/Mr Seed

Rappa Juliani

Emmy Kosgei
Mvutano mkubwa katika kategori hii ni baina ya Mwanadada Emmy Kosgei ambaye ndiye Mwanamuziki Bora wa Kike barani Afrika(Kwa mujibu wa Africa Gospel Music Awards 2011) pamoja na Rappa Julianni, Juliani kwa sasa anaaminika kuwa ndiye Mfalme wa Gospel HipHop nchini humo.Juliani kwa sasa anafanya Vizuri na Nyimbo yake iitwayo Barua ya Ocampo aliyomshirikisha mwanadada Jaya.

Tofauti na Emmy na Juliani yupo pia Daddy Owen, huyu anakubalika sana nchini humo na ndiye Mwanamuziki Bora wa Muziki wa Injili Afrika mashariki(kwa mujibu wa AGMA 2011), nafasi ambayo ilikuwa ikiwaniwa na Christina Shusho wa Tanzania.Daddy Owen ndiye mwanamuziki Bora Wa Kiume nchini humo na hii ni kwa mujibu wa Groove Awards 2011.

Daddy Owen
Nchini kenya kuna kuna tuzo nyingi za Muziki ukilinganisha na hapa kwetu Tanzania ambapo tuna Tanzania Music Awards pamoja na Tanzania Gospel Music Awards pekee. Kwa Upande wa Tuzo za Muziki wa Injili nchini Kenya, Tuzo za Groove Awards ndizo zinazoheshimika sana nchini Humo.



No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...