Saturday, April 28, 2012

Baada ya Kutoka Honeymoney, Kambua kusherehesha katika Groove Awards usiku wa leo.


Mwanamuziki wa nyimbo za injili na aliyekuwa mtangazaji wa kipindi cha RAUKA Kambua Manundu, usiku wa leo TAREHE 28,04.2012 anatarajia kuongoza sherehe za kutoa tuzo kwa wanamuziki wa nyimbo za injili nchini Kenya.Kambua ambaye kaTika siku za hivi karibuni Katika viwanja vya hotel ya  Windsor alifunga ndoa na Mch Jackson Mathu ambaye licha ya uchungaji Mathu pia ni mfanyabiashara mashuhuri nchini humo.

Baada ya kutoka kwenye fungate siku kadhaa zilizopita,usiku wa leo itakuwa ni mara ya kwanza kwa Kambua kusimama mbele za watu akiongoza shughuli akiwa kama mama mtumishi.

Kambua Siku ya Harusi yake

Kambua akiwa na mumuwe Mch Jackson Mathu siku ya harusi yao

Kambua akiwa na mumuwe Mch Jackson Mathu

Prestige cars down there
 Groove Awards ni tuzo zinazoheshimika sana kwa upande wa Gospel nchini humo na Afrika mashariki na kati. Kwa mwaka huu tuzo hizi zimedhaminiwa na kampuni ya simu ya Safaricom chini ya brand yake ya Safaricom skiza tone.Wanamuziki wa injili kutoka Tanzania wapatao sita nao wapo katika mchakato huo na kwa pamoja wanawania tuzo ya mwanamuziki bora wa injili kutoka Tanzania.
 

Artist Of The Year (Tanzania)
26a. Bahati Bukuku
26b. Bonnie Mwaitege
26c. Christina Shusho
26d. Neema Mwaipopo
26e. Rose Muhando
26f. Upendo Nkone


No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...