Wednesday, April 25, 2012

Diana Madida Muimbaji mtanzania anayemtumikia Mungu nchini Uingereza



Diana Madida Kihayile
Diana Madida Kihayile ni jina jipya baada ya kuolewa mwaka 2006 na Mr Bubele E Kihayile.kabla ya hapo amekuwa akijulikana kwa jina la Diana Madida.Diana amezaliwa na kukulia jijini Mwanza Tanzania,kwa sasa anaishi jijini Birmigham nchini Uingereza.Yeye pamoja na mumewe Mungu amewajalia watoto wawili wa kike,Rina Jodiah mwenye miaka miwili, na Jaina Sasha mwenye miaka mitano, kwa sasa Diana pamoja na familia yake wanasali katika kanisa la El Shadai International christian centre la jijini Birmigham nchini Uingereza.

Kimasomo Diana toka kidato cha kwanza mpaka cha sita amesomea shule ya sekondari Mwanza, wakati akiwa mdogo alikuwa anashiriki katika michezo ya  utamaduni,ngonjera na kwaya ya shule.Pamoja na kushiriki kote huko lakini alikuwa bado  ni mtu mwenye aibu nyingi japokuwa alikuwa anasikia furaha sana pindi  akifanya kitu na watu wakafurahi.Ambition yake kubwa toka akiwa mdogo ilikua kuwa sister wa kanisani na mcheza netball.

Diana akiwa na mumuwe Bubere na mtoto wao
Diana alimpa Yesu maisha mnamo  june 1997 kupitia mkutano wa Dr Moses Kulola na kuanzia hapo akaamua kujiunga na kanisa la E.AG.T  IMANI  lililo chini ya  mchungaji Juliana Nyanda maeneo ya Pasiansi jijini Mwanza napo ndipo safari yake kihuduma ilipoanza rasmi.Mwaka 1998,Diana alijiunga na kwaya ya kanisa iitwayo FAITH AMBASSADORS ya kanisani kwao na baada ya muda alianza kuimbisha baadhi ya nyimbo. 

Mwaka 1999 aliendelea kukua kiroho na kihuduma akaanza kulead ibada za kusifu na kuabudu ndani ya kanisa hilo na mwaka 2000 alijiunga rasmi na Kihayile band.
Mwaka 2003 alitoa solo album aliyeipa jina la “MIMI NAJUA KWAMBA YESU ANANIPENDA” na ilisambazwa na MAMU. Baada ya kutoa album hiyo mwaka uliofuatia yaani 2004 baada ya kumaliza kidato cha sita  Diana aliondoka nchini na kuelekea jijini Birmingham kuendelea na masomo ya juu hivyo Mamu hakuendelea tena kuisambaza album hiyo.  

Diana on stage
 Alipofika nchini Birmingham Diana aliendelea na huduma ya kusifu na kuabudu katika kanisa la Lighthouse chapel. Mwaka 2008 kwa msaada wa Mumewe Mr. Bubele aliweza tena kutoa album ya pili  aliyoiita MILELE, album hiyo  ilikuwa na nyimbo kama Uwe karibu nami,Tumeahidiwa ufalme mwema na milele iliyobeba jina la Album.Album hii Diana aliingiza sokoni nchini Uingereza na aliweza kuituma nyumbani kwenye baadhi za vituo vya redio.

Baada ya hapo,Diana M Kiyahile  aliweza kuunganisha plan zake kihuduma na mumewe ambapo ni jambo la kumshukuru Mungu kwani  kwa mujibu wa Diana mwenyewe anasema “naamini mmoja anaweza ua elfu ila wawili makumi elfu.Mr bubele Kihayile is the perfect match from heaven to me,ni mentor wangu,mwalimu wangu,mtunzi wa nyimbo na muziki wote wa nyimbo zetu na mtumishi mwenzangu katika huduma”. Kwa sasa wana kihayire hao wanesharekodi nyimbo nne kati ya hizo wamerekodi video moja ya wimbo unaitwa Africa yetu.Kwa kipindi hiki Bubere na Diana wameanzisha  huduma iitwayo Diana & Bubele Music ministries na kwa sasa wanaanda album ya kwanza ikiwa kama  huduma kamili.

Marajio yao  makubwa ni kuona ufalme wa Mungu umetukuka duniani na wanasisitiza “we are created to worship and to usher his people into his presence. Ni matarajio yetu kuongeza uamsho wa kusifu na kuabubu kwanza nyumbani kwetu Tanzania,Africa na duniani kote kwa ujumla,pia kwa kutumia muziki wa Africa kuleta uamsho ndani na nje ya afrika yetu.kwa kuwa Mungu ametupa instrument ambayo ni sauti na utunzi wetu tutaitumia kuyafanya mapenzi yake popote na kwa vyovyote atakavyo tuongoza,hatimaye tungependa tuwe mfano na daraja kwa watumishi wenye wito kama huu” 

Mr and Mrs Bubere Kihayire
Hosanna Inc: Ni Changamoto gani ambazo mtu aliyeokoka anakutana nazo akiwa Uingereza ambazo asingeweza kuzikuta akiwa Tanzania?
Diana:Mhh,kikubwa ni kubalance muda wa maisha kwa ujumla na huduma,kwa hapa kila mtu yuko na wajibu wa kufanya kazi na kuedesha maisha yake ambapo unakuta kila saa counts.Maisha ya UK kwa ujumla yanahitaji commitment ambapo ili uweze kuwa sawa na kusurvive inabidi uwe na descpline ambapo ni tofauti na Tanzania.Unaweza ukawa na muda wa kutosha kwenye huduma na maisha yakaendelea kawaida,ila nisikufiche kwa hapa there is no chance ya kwenda church five times a week! kama nilivyokuwa nafanya Tanzania.

Hosanna Inc: Artist gani wa injili ambaye kwa muda mrefu umekuwa ukimfatilia na amekuhamasisha sana katika kumtumikia Mungu?
Diana:Nimekua namsikiliza Cece winans kwani ni mwanamke ambaye naamini ni kipenzi cha Mungu,anampresent Mungu katika uzuri na utukufu wake kwa kina kinachoigusa mioyo ya wasiliklizaji wa nyimbo zake.Pia Yolanda adams ni kiboko kwa kuitumia sauti yake kumtukuza Mungu.

Wito wake kwa kanisa la Tanzania
Ni vyema kuishi maisha yanayomwabudu Mungu,na kuedelea kuuboresha uhusiano wa mtu na Mungu mbali na huduma anayomfanyia Mungu,watumishi wengi wanasahau kuwa huduma sio uhusiano,pia inapokuja kwenye huduma wasidharau calling walizonazo na kutamani za wengine,kile Mungu alichomwekea mtumishi ndo portion yake na ukikitendea kazi Mungu atapanua hema yako na maisha yako yatakamilika.


Her  Favourite Colour.
White/Cream
Inaonyesha usafi na ni rahisi kuspot uchafu,pia inapendeza.

 Nje ya Huduma ya uimbaji Diana ni
Mwinjilist mwalimu wa watoto(suday school)


What is ur Favourite Gospel Song kwa Tanzania
Unajibu maombi-Upendo Kilahiro
Her Favourite Gospel Song nje ya Tanzania
My redeemer lives (Nicole C Mullins)


What is your Favourite Gospel Hym{Tenzi}
Bwana Mungu nashangaa kabisa .

Her Favourite Bible verse
Mathew 7:7
Ombeni nanyi mtapewa,tafuteni nanyi mtaona,bisheni nanyi mtafunguliwa,
God has been faithful to me tangu nimeokoka nimeusimamia huu mstari na ninaendelea kuona matunda makuuubwa sana.



1 comment:

  1. MUNGU AWABARIKI HAWA WATUMISHI WA MUNGU KAZI YAO KTK BWANA SIO BURE WATALIPWA NA BWANA,ASANTE KWA INFO.UBARIKIWE

    ReplyDelete

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...