Sunday, April 15, 2012

Ephraim Sekeleti atoa ushuhuda namna Mungu alivyomponya na Ugonjwa kipindi angali mdogo

Ephraim Sekeleti akihudumu katika kanisa la Living water kawe-Makuti
Mwanamuziki wa Injili kutoka nchini Zambia Ephraim Sekeleti, jumapili ya leo tarehe 14/04/2012 alihudumu katika ibada kwenye kanisa la Living Water Kawe Makuti.Katika ibada hiyo Sekeleti aliimba nyimbo zake maarufu ikiwemo Uniongoze pamoja na nyimbo zake nyingine zilizomo kwenye album yake mpya iitwayo Acha Kulia.

Katika hali iliyoonekana kuvuta hisia za wengi kanisani hapo, ni pale mtumishi huyo ambaye ni baba wa watoto wawili alipotoa ushuhuda wa maisha yake kwa ufupi, ambapo hadi anamaliza kuusimulia watu wengi walikuwa wakilia kwa namna ambavyo Mungu alimtetea mtumishi huyo katika Maisha yake toka anazaliwa mpaka hivi leo.

Katika ushuhuda huo kwa kifupi sekeleti alisema akiwa mdogo alipata ugonjwa uliosumbua maeneo ya shingo na mdomoni, yeye pamoja na familia yake walisumbuka sana kupata matibabu, walienda sehemu zote lakini hawakupata msaada.Ilifikia hatua walienda mpaka kwa waganga wa kienyeji lakini hawakupata msaada.

Katika haali hiyo ndipo Ephraim aliweka Agano na Mungu kuwa endapo Mungu utaniponya basi nitakutumikia katika maisha yangu yote.Kwa kuwa Mungu ni mwenye nguvu alimponya Ephraim na ndipo kuanzia hapo Ephraim Sekeleti alianza kumtumikia Mungu. Mpaka sasa Sekeleti ana jumla ya album zipatazo saba ambazo ameziimba kwa Lugha za Ki-bemba,Ki-nyanja,Kiingereza na Kiswahili.

Ephraim Sekeleti akihudumu LWC-Kawe Makuti

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...