Tuesday, April 24, 2012

Paty attah na Eucharia Anunobi Ma-staa wa Nigeria waliompokea Yesu kama Bwana na Mwokozi wa Maisha Yao




Paty Attah

Paty Attah
Paty attah ni raia wa Nigeria na mmoja kati ya wakongwe wa tasnia ya filamu nchini humo , kwa miaka ya hivi karibuni, Paty amempokea kristo kama Bwana na mwokozi wa maisha yake. Baada ya kuokoka, amekuwa akijituma katika kuwarudisha watu wengi kwa kristo kupita njia mbalimbali pamoja na kushare maneno ya Mungu katka wall yake ya Facebook na Twitter

Kwa mujibu wa vyombo vya habari vya nchini Nigeria Paty kwa sasa anaishi jijini Humburg nchini Ujerumani na tofauti na utumishi, Paty ni muigizaji wa Filamu kazi ambayo anaiendeleza nchini humo .Pamoja na hayo pia ni mwanamitindo na Mwanamuziki. Paty mpaka sasa ameshacheza zaidi ya filamu arobani zikiwemo Secret Fantasy, Final Spirit of Love, Fools in Love, More than Gold, Only Love pamoja na  Songs of Sorrow.

Eucharia Anunobi

Eucharia Anunobi
Kama kuna watu ambao waliwahi kuushangaza uma wa wanigeria kwa kauli zao kuwa wameamua kuokoka basi Eucharia Anunobi ni mmoja wao,Eucharia  maarufu kama UK, alikuwa ni mmoja wa ma-staa wa Nollywood waliojulikana sana hasa kwa mtindo wake wa kuvaa nguo huku sehemu kubwa ya kifua chake ikiwa wazi.

Kwa sasa UK ameokoka na amekuwa akihubiri na kumshuhudia Yesu pasipo kificho.Kuna habari za hivi karibuni zinasema ameamua kuwa mchungaji na amesimikwa rasmi kwa kazi hiyo hivyo kwa sasa anachunga kanisa lake.Eucharia alipata nafasi ya kuhubiri wakati wa kusimikwa u-shemasi mbunifu wa mitindo na muigizaji nguli nchini humo Clarion Chukwura’s


No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...