Tuesday, October 2, 2012

Alichokisema DNA baada ya Kumaliza-show Club Billcanas



DNA alipokuwa akiwasili nchini Tanzania mwishoni mwa wiki iliyopita
Denis Kagia mwanamuziki kutoka Kenya alimaarufu kwa jina la DNA, juzi jumapili alikuwa mmoja wa waimbaji kwenye club ya usiku ya Bilcanas iliyoko mitaa ya posta jijini Dar es salaam.DNA alipoulizwa na waandishi wa habari akiwa ndani ya club hiyo ikiwa ameacha wokovu ama laa yeye alijibu 

“ SIJAACHA WOKOVU,BADO NIMEOKOKA LAKINI NIMEBADILI MUZIKI WANGU KWA SASA NAFANYA MUZIKI WA KAWAIDA KAMA NILIOKUWA NIKIUFANYA.NILIOKOKA ILI NIACHANE NA POMBE, NA NIMEWEZA NA NIKO KWENYE IMANI BADO”

Ikumbukwe kuwa DNA aliyewahi kutamba na nyimbo ya BANJUKA, kwa sasa anatamba na nyimbo yake isemayo “MASWALI YA POLISI”. Mwaka juzi (2010) DNA aliutangazia umma kwamba ameokoka na kilichofuatia alianza kuimba nyimbo za injili.Kabla ya wokovu Denis Kagia alikuwa akisumbuliwa sana na unywaji wa pombe kupita kawaida pamoja na matumizi ya sigara.

Baada ya kuokoKa DNA pamoja na kufanya muziki wa injili pia alikuwa mtangazaji wa kituo cha One Fm cha nchini kenya.Nchini Kenya suala la mwanamuziki huyu kurudi kufanya circular music lilizua gumzo katika kanisa la kenya na kila mmoja alitafsiri alivyoweza huku wengi wakiamini jamaa ame back slide

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...