Tuesday, October 30, 2012

Kanisa la Mikocheni B lafanya Ibada ya Kuliombea Taifa



Mh. Dkt. Getrude Rwakatare akiwa katika ibada hiyo
 Jumapili iliyopita Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la Mlima wa Moto Mikocheni Mh. Dkt. Getrude Rwakatare akitoa Ujumbe kwa Watanzania waliohudhiria Ibada Maalum ya Kuliombea Taifa ambapo ametaka watu kutobaguana kwa misingi ya Dini, Ukabila wala Siasa na kusema pamoja na Utawala bora pia tunahitaji maombezi ili tuweze kufikia Malengo yaliyokusudiwa kulipeleka Taifa linapotakiwa kufikia.

Dkt. Rwakatare amesema nia kubwa ya kufanya Ibada hiyo ya Maombezi ni kutaka kuweka usawa kutokana na siku za hivi karibuni kuibuka kwa Matamko mbalimbali kutoka kwa watu tofauti wakiwemo viongozi wa Kitaifa, Kidini na wa baadhi ya Makundi yanayohitilafiana na kusema tukiomba kwa jina la Mungu kila kitu kitakwenda kama tulivyomuomba ili Tanzania iendelee kuwa nchi ya Amani na Utulivu kama ilivyokuwa miaka yote ambayo ni kimbilio la watu wa Mataifa mbalimbali kwa sababu Watanzania hawajui kuchukiana na wamekuwa watu wa kushikamana kwa miaka yote.


Sehemu ya waumini wa kanisa hilo







Rose Muhando alihudumu madhabahuni siku hiyo

Ibada Ikiendelea


Mama akifurahia ibada hiyo

Zigizi, Zigizi zigi,Zigizi


No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...