Tuesday, October 16, 2012

Kanisa lingine la Kipentekoste Kigoma lachomwa moto


Kanisa la Pentecoste [MMPT] lililopo Buronge katika Manispaa ya Kigoma/Ujiji   liisa hilo,mabechi 14, ubao wa kufundishia, mikeka 3 na mlango 1 viliteketea kwa moto.Jumla ya mali zilizoteketea kwa moto ni Sh.Milioni 1,337,000.Kamanda huyo alisema “kiini cha tukio hili bado kufahamika, hakuna madhara kwa binadamu, upelelezi wa tukio hili unaendelea ili kuwabaini wahalifu hao kwa hatua za kisheria”alisema.

Picha hii inaonyesha Mchungaji wa kanisa la Pentecoste [MMPT] Emanueli Simoni [49] akiwa amesimama  ameshika kechi kwenye kanisa hilo lililoteketea kwa moto usiku wa kuamkia jana majira ya saa 4 usiku eneo la Buronge katika Manispaa ya Kigoma/Ujiji

Mchungaji wa Kanisa la Pentecoste [MMPT] Emanueli Simoni [49] alisema,”mimi nilipata taarifa kuwa kanisa langu limeteketea kwa moto, nilikwenda polisi Sentro kutoa taarifa, ndipo tulikwenda eneo la tukio tukakuta kanisa lote limeteketea kwa moto”alisema.

Eliasi alisema tukio hilo lilitokea jana majira ya saa 4 usiku katika eneo la Buronge katika Manispaa ya Kigoma/Ujiji.Alisema katika kanisa kulikuwa na Mabechi 14, Mlango 1, Vilago 3, Sanduku za kutozea sadaka na ubao wa kufundishia.Vyote vikiwa na thamani ya Sh. Milioni 1,337,000 mali ya kanisa hilo.Alisema ajui watu waliochoma kanisa hilo, wala hakuna mtu anayeshikiliwa na polisi kuhusiana na tukio hilo.

Mchungaji huyo anaiomba serikali iangalie sana matatizo ya uchomaji wa makanisa sasa yanaenea nchi nzima. Pia amelitaka Jeshi la polisi Mkoani hapo kufanya doria kwenye makanisa wakati wa usiku ili kukomesha vitendo vya uchomaji wa makanisa.
Alisema kanisa ni taasisi ya jamii hivyo anaomba serikali ichangie gharama ya ujenzi wa jengo hilo ili wananchi wanaohabudu katika kanisa hilo wapate sehemu ya kuabudia.


No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...