Sunday, October 14, 2012

Ndoa mbili ya Mercy Denis wa Glorious Celebration,na ya Regraa Wambura zagumza jiji week-end hii



Kwa Mtini Jifunzeni
Mmoja wa wanamuziki mahiri wa kundi la Glorious celebration aitwaye Mercy Denis siku ya jana Jumamosi alifunga ndoa na Bro Victor Langula ndoa iliyofungwa katika kanisa la EAGT Mito ya baraka lililopo Jangwani jijini Dar es salaam na baada ya ndoa kufungwa sherehe zilifanyika katika ukumbi wa New Msasani Hotel.

Ndoa hiyo iliyohudhuriwa na Ma-star wengi wa nyimbo za Injili nchini huku Mercy akipata support ya kutosha kutoka kwa wana Glorious Celebration wakiongozwa na Regraa Mabisa Emmanuel hususani kwenye Send off party iliyofanyika mkoani Morogoro ambako wazazi wa Mercy huchunga Kanisa.

Mr and Mrs Victor Langula
It Sound Waaooh
On the way from Dar es salaam Emmanuel Mgaya alifika Morogoro kwa ajili ya kumpa company Swahiba wake Victor, Masanja alisimama kama Mc wa Send off Party ya Mercy
Mr and Mrs Victor Langula
Chanda Chema



Mercy akiwa kwenye send off Party yake mkoani Morogoro

Wakati Mercy wa Glorious Celebration jana aliambatana na mumewe, usiku huu wa tarehe 14/10/2012 hapa jijini Dar es salaam Regraa Wambura kama ajulikanavyo na wengi yuko katika sherehe ya kumpongeza kwa uamuzi wake wa kufunga ndoa.Sherehe hii inafanyika katika ukumbi wa Giraffe Hotel.Tunaamini mkono wa Mungu utakuwa juu yao Mercy pamoja na Regraa
Sherehe hii ya wambura inaendelea usiku huu katika ukumbi wa Giraffe Hotel,Picha kwa Hisani ya Samuel Sasali

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...